Yanga sc inakikosi kipana lakini pengo la Khalid Aucho "the tank" limeonekana bila kificho

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
10,587
Reaction score
13,425
Kongolee kwa wanayanga kwa matokeo haya tuliyoyapata dhidi mwarabu (USM ALGER).

Nilishawahi kuleta Uzi humu wakumwaga maua kwa Khalid Aucho na kusema ndiyo namba nane Bora katika kikosi Cha Yanga na kweli leo pengo lake limeonekana bila ya kificho ijapo kuwa huwa tunashupaza mishipa ya shingo kwa kuimba Yanga Ina kikosi kipana.

Kukosekana kwa Khalid Aucho imeharibu mipango ya kocha Nabi tofauti na vile alivyozoea kumpanga Mudathr Yahya namba kumi huku Azizi kii akianzia benchi.

Ina maana kuwa Mudathir anaweza kushuka chini kusaidiana na Aucho pamoja na bangala endapo timu inapokuwa Haina mpira hicho ndicho kitu kinachompa faida Kocha Nabi.

Ujuzi wa kupiga pasi nakukaba kwa kutumia nguvu pamoja na urefu wa Khalid Aucho ilikua ni faida kubwa sana endapo angekuwepo tungeona mabadiliko makubwa dimba la Kati na timu kupata matokeo.

Pengo la Khalid Aucho pale Kati lilionekana vizuri tu na namba kumi aziz kii alikuwa hapati mipira kutoka kwa namba nane.
 
Perfect said
 
Mimi na Changaule tuliliona hili mapema sana hata kabla ya mechi kuchezwa 28/05/2023.

Mechi alizokosekana Aucho NBC PL Yanga ilipata wakati mgumu sana kushinda, ndiyomaana kwenye kikosi chochote cha mpira kuna Potential/Key Players na normal Players.


Bahati iwe nasi Yanga FC second final 03/06/2023, tupindue meza ugenini na kubeba ubingwa wa CAFCCL.

Mungu ibariki Young Africans, Mungu ibariki Tanzania na dunia yote, Amina.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Kweli kabisa mkuu sijui awam hii ya pili aanze sureboy na bangala then Mudathir Yahya acheze kumi na azizi kii aanzie benchi kwanza.
 
Tunapata nguvu ya kuyasema haya kwa sababu yanga haikushinda, nakubali Aucho ni mchezaji mzuri lakini ASMA ilikuja kucheza kimkakati zaidi, na pengine Aucho angekuwepo matokeo hangekua haya.

Yanga ilipocheza na klabu africain kule tunisia na kushinda,Aucho hakucheza, na sureboy alicheza vizuri sana siku hiyo.
 
Ndiyo mechi hiyo pekee ambayo nilimuona Sure Boy aking'aa kwenye michuano hii ya CAFCCL [emoji4]

Mechi zipi alizong'aa kiubora mbali na hiyo tu?

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Huyu Aucho aliomba Po siku Robertino anawapiga 2-0 mpaka akatolewa halftime,halafu eti kikosi kipana utopolo bhana
 
Huyu Aucho aliomba Po siku Robertino anawapiga 2-0 mpaka akatolewa halftime,halafu eti kikosi kipana utopolo bhana
Umbumbumbu ni kipaji, unadhani hata hao akina Messi wanakuwa na physically fitness per 100% kila mechi?

Unamkosoaje Mchezaji kwa mechi 1 tu, mbona ile ya ngao ya hisani alikuwepo mkafa 2-1 huiongelei?

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Na bado profesa nabi maji marefu baada ya mechi alikuwa analalamika muda wa maandalizi ulikuwa hautoshi sasa hicho kikosi chenu kipana kimetanuka wapi nyumaaa au mbelee
Kwa hiyo wewe na akili zako unadhani Kuna kocha atakosa Cha kuzungumza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…