Ni Godfrey Mwashiuya ambae hapo awali alitaka hiyo Mimba itolewe lakini Mwanamke akakataa kisha akawa anamtishia huyo Mwanamke kuwa asipoitoa atamuacha lakini bado huyo Mwanamke akakomaa hadi alipojifungua Mtoto ambaye kwakweli anafanana kila kitu na Mwanandinga huyo ambaye usajili wake kwenda Yanga SC kutoka huko Mbeya katika Klabu yake ulitia ' Fora ' ambapo alisajiliwa kwa Tsh 300,000/ huku Karatasi yake ya Usajili ikisema amesajiliwa kwa Tsh 15,000,000/.
Kwa mujibu wa huyo Mwanamke ni kwamba Mchezaji huyo hakuwa na msaada wowote Kwake baada ya Kujifungua Mtoto wake huku akiwa na maneno ya dharau mno kiasi kwamba kilimsababisha Yeye ( Mwanamke ) kuwa katika wakati mgumu wa maisha kupelekea kutokupata mahitaji ya Kiuzazi yaliyosababisha Mtoto wao huyo aitwae Judy Kuugua ghafla na Kufariki dunia hivi leo ikiwa ni siku ya 22.
Mchezaji huyo alipofuatwa kuulizwa juu ya Mpenzi wake huyo aitwae Jacky ( au Mama Judy ) na kwamba kwanini mwanzo aliikataa Mimba kisha baadae Mtoto alipozaliwa akaikubali japo alikuwa hatoi huduma hadi kupelekea ' umauti ' wake jibu alilotoa ni kwamba kwa sasa hivi Wachezaji wa Yanga SC wana hali mbaya ya Uchumi kwani hata Chai yao tu kama Wachezaji wa Yanga SC ni tatizo na muda mwingi wanashinda na njaa huku wakipata msaada kutoka kwa Wachezaji wa Simba SC ambao wao muda mwingi ' accounts ' zao huwa ' zinacheka ' tu kwa ' Midola Midola ' wanayoioga kila siku.
Kwa mujibu wa huyu Mpenzi wake Mchezaji wa Yanga SC Godfrey Mwaishuya aitwae Jacky ( Mama Judy ) ni kwamba ana ushahidi wote tena wa ' meseji ' zake kwani ameharibiwa sana maisha na huyo Mchezaji hivyo anapanga kumfungulia mashitaka ila kama Yanga SC watamsaidia basi anaweza akayamaliza Kistaarabu tu.
Nawasilisha.
Source ya taarifa hii ni SHILAWADU na Clouds tv.