Kutoka kwenye kusikilizia maumivu ya kuukosa ubingwa wa ligi kuu na ule wa shirikisho, kutokana na kusajili washambuliaji butu!
Mpaka kujitoa ufahamu na kuanza kumshangilia kwa nguvu nyingi mchezaji mzawa wa timu ndogo tu na changa kabisa ya Geita Gold, na aliyeibuliwa kuwa mfungaji bora na kocha mzawa Felix Minziro (mchezaji mahiri wa zamani wa timu ya wananchi Yanga)!! Kwa kumuamini na kumpa nafasi kwenye kikosi chake cha kwanza (maana alikuwa na uwezo wa kumbania kama afanyavyo yule msaidizi wa juju fc kwa wale wachezaji wasiompa 10%)!!
Hakika mashabiki wa Mudi fc wanastahili kabisa kuitwa mbumbumbu. Yaani badala ya kuangalia mapungufu ya timu yao! Wamegeuka na kuwa mashabiki wa George Mpole!!!!!