CAGvsSPEAKER
JF-Expert Member
- May 16, 2019
- 1,339
- 5,048
Mimi ni mwanaYanga tena Yanga kweli.
Yanga bado ni mbovu. Tukubali hilo kwanza. Pia, viongozi na muhamasishaji wetu wasiwajengee mashabiki hisia za kuonewa.
Kweli Yanga ingekuwa imara ilikuwa ya kutoa suluhu na Gwambina? Na tukubali tu kuwa muelekeo ulianza kupotea pale.
Tuliitukuza mechi na mtani tukaacha kujihakikishia pointi tatu kutoka kwa Gwambina, matokeo yake mechi mbili tukaambukia pointi 2 kitu ambacho tungeshinda ya Gwambina na kutoa sare na mtani zingekuwa ni point 4.
Jana tumesare na Mbeya City, analaumiwa refa yale mashuti alokuwa anapiga Sarpong huko mawingini tulitaka refa aite mpira kati?
Timu bado ni mbovu nashangaa mashabiki wanaingia kwenye mtego wa viongozi wa kuwalaumu marefa uyo Saido ni pancha tupu, Kalinyos ndo usiseme, Yakuba pancha na kocha anatumia kilichopo siwezi kumlaumu.
Tukubaliane kuwa,timu yetu bado ni mbovu. Jana walicheza hovyo kuliko hovyo nyingine zote. Mbeya City waliwalazimisha kucheza walivyotaka. Ilikuwa puu paaa utadhani huo mpira una moto.
Badala ya viongozi kuwaambia mashabiki ukweli, wao wanawaaminisha kuwa refa ndo tatizo. Hizi timu mnazozidharau zilikuwa busy kujiandaa na raundi yapi......sisi tulikuwa busy kwenye vyombo vya habari kusaji na media sijui nini.
Nihitimishe, WanaYANGA,mtani hayupo mbali na sisi ubingwa tunaweza kuendelea kuusikia tena kama viongozi hawatakuwa serious.
Pia ni wakati sasa wa Fredrick Lugano Mwakalebela kujitafakari kama anaendelea kutosha katika kiti anachokalia sasa. Tarehe 12 Feb imepita hatujasikia yeye au kiongozi yoyote wa Yanga alokwea ndege kwenda CAS kusikiliza kesi ya Yanga na Morison.
Wala si Morison au kiongozi yoyote wa Simba aliyekwenda CAS kwa shauri hilo.
Niendelee kuimbea Yanga yetu ule muujiza wa kutaka Ubingwa na ubovu tulionao utimie msimu huu walau na sisi tufurahi kidogo.
Tukutane tarehe 17 na Kagera ambao nao sidhani kama watakuja kushangaa Mfugale au Ubungo interchange.
Mungu awe nasi.
Yanga, DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO.
Yanga bado ni mbovu. Tukubali hilo kwanza. Pia, viongozi na muhamasishaji wetu wasiwajengee mashabiki hisia za kuonewa.
Kweli Yanga ingekuwa imara ilikuwa ya kutoa suluhu na Gwambina? Na tukubali tu kuwa muelekeo ulianza kupotea pale.
Tuliitukuza mechi na mtani tukaacha kujihakikishia pointi tatu kutoka kwa Gwambina, matokeo yake mechi mbili tukaambukia pointi 2 kitu ambacho tungeshinda ya Gwambina na kutoa sare na mtani zingekuwa ni point 4.
Jana tumesare na Mbeya City, analaumiwa refa yale mashuti alokuwa anapiga Sarpong huko mawingini tulitaka refa aite mpira kati?
Timu bado ni mbovu nashangaa mashabiki wanaingia kwenye mtego wa viongozi wa kuwalaumu marefa uyo Saido ni pancha tupu, Kalinyos ndo usiseme, Yakuba pancha na kocha anatumia kilichopo siwezi kumlaumu.
Tukubaliane kuwa,timu yetu bado ni mbovu. Jana walicheza hovyo kuliko hovyo nyingine zote. Mbeya City waliwalazimisha kucheza walivyotaka. Ilikuwa puu paaa utadhani huo mpira una moto.
Badala ya viongozi kuwaambia mashabiki ukweli, wao wanawaaminisha kuwa refa ndo tatizo. Hizi timu mnazozidharau zilikuwa busy kujiandaa na raundi yapi......sisi tulikuwa busy kwenye vyombo vya habari kusaji na media sijui nini.
Nihitimishe, WanaYANGA,mtani hayupo mbali na sisi ubingwa tunaweza kuendelea kuusikia tena kama viongozi hawatakuwa serious.
Pia ni wakati sasa wa Fredrick Lugano Mwakalebela kujitafakari kama anaendelea kutosha katika kiti anachokalia sasa. Tarehe 12 Feb imepita hatujasikia yeye au kiongozi yoyote wa Yanga alokwea ndege kwenda CAS kusikiliza kesi ya Yanga na Morison.
Wala si Morison au kiongozi yoyote wa Simba aliyekwenda CAS kwa shauri hilo.
Niendelee kuimbea Yanga yetu ule muujiza wa kutaka Ubingwa na ubovu tulionao utimie msimu huu walau na sisi tufurahi kidogo.
Tukutane tarehe 17 na Kagera ambao nao sidhani kama watakuja kushangaa Mfugale au Ubungo interchange.
Mungu awe nasi.
Yanga, DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO.