Yanga uwanja mmeshindwa kujenga, fanyeni basi ukarabati wa jengo lenu

mpimamstaafu

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
4,445
Reaction score
4,707
Hakika Yanga yenye umri wa miaka 85 kila mmoja wetu angeamini ilipaswa iwe na mafanikio makubwa sana lakini ni kinyume chake. Yanga bado ipo kwenye mfumo wa kizamani cha uongozi. Yanga imeshindwa kabisa kuujenga upya uwanja wake wa Kaunda licha ya kuwa nao miaka kadhaa, jengo la Yanga halijafanyiwa ukarabati toka lilopojengwa, rangi zimepauka, jengo limechoka na kuchakaa.Tunaushauri uongozi wa Yanga fanyieni ukarabati jengo lenu linakera sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Punguza hasira najua hata hizi droo na yule Mtembea na Mpira vyote vinakuudhi angalia hali ya Kaunda Sports CentreView attachment 1367911

Sent using Jamii Forums mobile app
Piga picha mpya. Halafu mbona mikia kutwa kwenye jengo la Yanga wakati lenu mnafupia pale popo. Pale Msimbazi ukipita unaweza kulia machozi mekundu kwa majengo ya simba yalivyochakaa. Kama unabisha aliye karibu na Msimbazi hapo apige picha ilo tufananishe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kimya kimya, hatunaga kelele,hii picha ya leo hii we mkia, halafu fanya ustaarabu upite pale klabuni kwenu ukakusanye vyupa na mifuko ya nylon wanayotumia watu kujisaidia pale msimbwaziii.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Viongozi wanafuga vitambi tu pale, siku zinaenda hamna kipya walichokifanya. GSM wanapambana kuisaidia yanga isimame ili plan zao za kuuza bidhaa za yanga zisifeli, timu ya under 17 jez za mazoez hawana, mipira utata, watoto wanatia huruma wale...wao ni wanachokijua ni kuunda kamati tu...mambo ya kamati yashapitwa na wakati. Watu wasomi ila hawana strategies za kuinufaisha timu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…