Yanga wadhibitiwe, watazimaliza hela za Mama

Yanga wadhibitiwe, watazimaliza hela za Mama

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Tangu Rais Mama Samia Suluhu Hassan atangaze motisha ya shilingi milioni tano kwa kila goli litakalofungwa na Simba au Yanga kwenye michuano ya kimataifa, Yanga wamekuwa watu wa 'kutaka sifa'. Wamekuwa wakichota mamilioni kwenye kila mchezo.

Wakati watani zetu Simba hadi sasa wakipata milioni kumi kwa magoli mawili ya mechi mbili za Vipers, Yanga wameshatia kibindoni milioni thelathini kwa magoli sita dhidi ya Mazembe na Real Bamako. Yanga wanaelekea kumaliza kibubu cha ahadi tamu ya Mama Samia.

Natoa wito wa kuwadhibiti Yanga ili wapunguze sifa za kuvuna mamilioni ya Mama. Na naomba, ili watani zetu nao wapate chochote kitu, ahadi hii itumike pia kwa ligi ya ndani ambapo Simba aka Mnyama anaongoza kwa kufunga magoli mengi.

Wapi Baleke? Wapi Bocco? Wapi Chama? Wapi General Phiri? Wapi Sakho?
 
Kombe la mbuzi lile halina jipya, nao walikosea huwezi kutoa zawadi sawa kwa mashindano tofauti, haiwezekani wengine wanacheza kombe la waliofeli halafu unawapa zawadi sawa na mabingwa.

CAF na FIFA tunatambulika Simba Sc ndio mabingwa wa nchi hii, sisi ndio wenye nchi.
 
Kombe la mbuzi lile halina jipya, nao walikosea huwezi kutoa zawadi sawa kwa mashindano tofauti, haiwezekani wengine wanacheza kombe la waliofeli halafu unawapa zawadi sawa na mabingwa...
Simba ndiyo bingwa wa Tanzania? Kwa msimu upi? Yanga ndiye bingwa mtetezi Mkuu
 
Kombe la mbuzi lile halina jipya, nao walikosea huwezi kutoa zawadi sawa kwa mashindano tofauti, haiwezekani wengine wanacheza kombe la waliofeli halafu unawapa zawadi sawa na mabingwa.

CAF na FIFA tunatambulika Simba Sc ndio mabingwa wa nchi hii, sisi ndio wenye nchi.
Ilo kombe la mbuzi ndio lilowafanya mkaroge SA na mkapigwa faini na CAF
 
Kombe la mbuzi lile halina jipya, nao walikosea huwezi kutoa zawadi sawa kwa mashindano tofauti, haiwezekani wengine wanacheza kombe la waliofeli halafu unawapa zawadi sawa na mabingwa.

CAF na FIFA tunatambulika Simba Sc ndio mabingwa wa nchi hii, sisi ndio wenye nchi.
Kwamba CAF na FIFA wanatambua simba ndiyo bingwa wa nchi hii? angalia vizuri kama umebeba kichwa chako inawezekana umekiangusha na haujui.
 
Ilo kombe la mbuzi ndio lilowafanya mkaroge SA na mkapigwa faini na CAF
Hilo ndio kombe la maigizo tuliloenda kufanyia maigizo yetu huko, nawashangaa utopolo mnavyolikomalia🫣🫣
 
Kwamba CAF na FIFA wanatambua simba ndiyo bingwa wa nchi hii? angalia vizuri kama umebeba kichwa chako inawezekana umekiangusha na haujui.
Kichwa changu kiko vizuri sana, utopolo hamjawahi kuliletea heshima hili taifa hata siku moja, mmedumazwa na kufeli, hamna mbele wala nyuma, matokeo yake hata mkiwafunga waliofeli wenzenu mnashangilia usiku kucha[emoji1787][emoji1787]
 
Kichwa changu kiko vizuri sana, utopolo hamjawahi kuliletea heshima hili taifa hata siku moja, mmedumazwa na kufeli, hamna mbele wala nyuma, matokeo yake hata mkiwafunga waliofeli wenzenu mnashangilia usiku kucha[emoji1787][emoji1787]
Pole sana mkuu
 
Back
Top Bottom