Yanga walienda kumjulia hali au kumlilia hali Manji katika Mahakama ya Kisutu?

PROSPER 05

JF-Expert Member
Joined
Oct 14, 2013
Posts
226
Reaction score
217
Suala la nahodha wa Yanga, Nadir Haroub Ally maarufu kama Cannavaro kukutana na Mwenyekiti wa zamani wa Yanga, Yusuf Manji limezua mjadala mkubwa.

Wako wanaoamini kuwa Cannavaro ambaye aliongozana na benchi la ufundi, walikwenda kumjulia hali Manji katika mahakama ya Kisutu.

Wako Wengine wamekuwa wakiamini kwamba Wanajangwani hao walikwenda kumlilia shida kwa kuwa mambo yao si mazuri.

Wewe Unafikiri nini Kuhusu hili?
 
Mie Nina swali moja tu,wakat yupo ghetto walienda kumuona?????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…