Yanga warekebishe namna wanavyoanza mechi pale Kwa Mkapa

Yanga warekebishe namna wanavyoanza mechi pale Kwa Mkapa

Mechi nyingi walizocheza nyumbani wamekuwa na makosa mengi hasa ya kiulinzi, kukosa kujiamini na ubunifu wa kupanga mashambulizi. Inawachukua zaidi ya dakika 15 kuanza kuwa makini na kufanya mipango ya hatari. Mechi na Ruvu, Biashara, Kagera, Geita gold, Mbeya city na hata KMC hawakuanza vizuri. Ni bahati yao timu hizo zina errors nyingi kuweza kuwaadhibu. Yanga wamekuwa na mwanzo mzuri wakicheza na Simba tu. Possibly wanakamiaga sana derby. Pia wanacheza vizuri ugenini.
Ushauri: Wakafanyie kazi jambo hili haraka iwezekanavyo, ipo siku watalia

Binafsi sioni cha kurekebisha. Wachezaji wanajitahidi kadiri ya uwezo wao. Tuendelee kuwatia moyo. Timu zote za ligi kuu zimejiandaa, na zina sifa ya kushinda.

Hivyo kuelemewa kwa Yanga katika michezo yake, ni jambo la kawaida! Maana haichezi na maveterani wa simba! Inacheza na timu shindani za ligi kuu, na ambazo nazo zimejiandaa kimbinu kama Yanga. Hivyo muhimu kwetu kwa sasa ni pointi 3 muhimu kwenye kila mechi.
 
Mechi ya simba beki awe farid musa naona mmeanza kumsifia sasa yule ndo anatakiwa aanze halafu akutane na Morrison au sakho ndo akili zitawakaa sawa
 
Ukiona hvyo ndo ujue wanajiamini.. Timu hizi ndogondgo sijui Simba, Azam, KMC hazitupi shida sisi wanaume tunawachezea kwa Dharau na bado tunawakunguta.. subirini April 30 tunaua kolo pale kwa Mkapa
 
Umesahau wakati wanaaza kuazisha hutoa nje mpira timu opponent warushe hii inakaaje
 
Back
Top Bottom