brave one
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 4,879
- 7,386
YANGA imedai kwamba iligoma kuuza haki za matangazo ya Televisheni za mechi yao na BDF XI ya Botswana kwa vile Azam
TV haikufika dau.
Katibu wa Yanga, Jonas Tiboroha, ameweka wazi kwamba mechi zao wanaanza kuuza kwa dau la dola 10,000 (Sh 18 milioni) dau ambalo hakuna chombo chochote nchini kilichoweza kulifikia.
"Tulikuwa na mazungumzo na baadhi ya TV, lakini hawakuweza kufika kiwango chetu tukakacha biashara hiyo kwani haikuwa na manufaa kwetu, hivyo tukaona bora kusubiri mapato ya mlangoni," alisema kiongozi huyo mwenye uelewa wa mambo ya ufundi wa soka uwanjani.
Alitolea mfano wa tathimini ndogo waliyofanya kwamba waligundua kuwa kitendo cha kuonyesha mechi kinapunguza watu kwenda uwanjani kuangalia mchezo hivyo kupunguza pato.
Alifafanua kwamba kama Azam TV wangeonyesha mechi hiyo, kampuni mama ya kituo hicho ingefaidika mara mbili kwani matangazo ya biashara zake za unga, juisi na lambalamba yangeonekana mbali na kuzidi kupata wateja huku Yanga ikiambulia kidogo.
"Mlango upo wazi kwa TV inayotaka kuonyesha mechi zetu, lakini kwa kuzingatia dau linalotakiwa kulingana na uzito wa mechi," alisema na kudai kwamba Azam iliweka Sh8 milioni mezani ambazo ni kiduchu. Tiboroha alisema soka ni biashara, hivyo lazima wazingatie masuala ya uchumi ambayo ndio misingi ya kuleta maendeleo ya kufika mbali.
MwanaSpoti
TV haikufika dau.
Katibu wa Yanga, Jonas Tiboroha, ameweka wazi kwamba mechi zao wanaanza kuuza kwa dau la dola 10,000 (Sh 18 milioni) dau ambalo hakuna chombo chochote nchini kilichoweza kulifikia.
"Tulikuwa na mazungumzo na baadhi ya TV, lakini hawakuweza kufika kiwango chetu tukakacha biashara hiyo kwani haikuwa na manufaa kwetu, hivyo tukaona bora kusubiri mapato ya mlangoni," alisema kiongozi huyo mwenye uelewa wa mambo ya ufundi wa soka uwanjani.
Alitolea mfano wa tathimini ndogo waliyofanya kwamba waligundua kuwa kitendo cha kuonyesha mechi kinapunguza watu kwenda uwanjani kuangalia mchezo hivyo kupunguza pato.
Alifafanua kwamba kama Azam TV wangeonyesha mechi hiyo, kampuni mama ya kituo hicho ingefaidika mara mbili kwani matangazo ya biashara zake za unga, juisi na lambalamba yangeonekana mbali na kuzidi kupata wateja huku Yanga ikiambulia kidogo.
"Mlango upo wazi kwa TV inayotaka kuonyesha mechi zetu, lakini kwa kuzingatia dau linalotakiwa kulingana na uzito wa mechi," alisema na kudai kwamba Azam iliweka Sh8 milioni mezani ambazo ni kiduchu. Tiboroha alisema soka ni biashara, hivyo lazima wazingatie masuala ya uchumi ambayo ndio misingi ya kuleta maendeleo ya kufika mbali.
MwanaSpoti