Queen V
JF-Expert Member
- Jan 19, 2012
- 775
- 1,332
Timu ya Soka ya Young Africans “Yanga” imetoa taarifa ya kutoshiriki Kagame Cup mwaka 2019 kutokana na changamoto mbalimbali.
Changamoto zilizotajwa ni pamoja na
1. Wachezaji wengi kumaliza mkataba
2. Wachezaji wachache wenye mikataba walisharuhusiwa kwenda kwenye mapumziko ya mwisho wa msimu.
3. Baadhi ya wachezaji na mwalimu watakuwa kwenye ushiriki wa AFCON nchini Misri.
4. Wachezaji ambao timu ipo kwenye taratibu za kuwasajili bado hawajamaliza taratibu za mwisho kwenye vilabu vyao.