Hayo ndiyo madhara ya kukatisha mkataba na Zahera...huyo mkongo bado ana contacts na wachezaji wa Yanga ...anawasiliana nao na bila shaka amewaambia wafanye hivyo ili kuikommoa Yanga...Ukifanya jambo kubwa kama kukatisha mkataba wa kocha ni lazima uwe umejipanga vizuri kwa kufanya tathimini kuhusu madhara na kuweka mikakati ya kupangua madhara hayo...Uongozi wa Yanga ulipaswa ulifahamu hilo na kujipanga tayari kwa mapigo...Zahera alirejea Dar kufanya hilo kuwashawishi wachezaji waachane na klabu ili kuitikisa klabu ...Miaka ya 70 kocha Tambwe Leya naye wa DRC aliibomoa Yanga kwa kuwafukuza wachezaji wanne na kuleta mgogoro mkubwa ulioigawa Yanga na kuzaa Pan Africa....Uongozi wa sasa wa Yanga ulipaswa uwe umejipanga vilivyo kwa kuhakikisha wachezaji hawarubuniwi na Zahera...Pamoja na hayo binafsi namhurumia mno Zahera kwani kama bado TZ usalama wake uko shakani...nashauri polisi walione hili na kumpa ulinzi Zahera ili aondoke salama...Madhara kwa zahera itakuwa ni jambo baya pia kwa klabu ya Yanga...Viongozi wa Yanga lazima wawe makini na suala hili kwani siyo dogo kama wanavyoweza kufikiri au kudhani ...Wajipange na wawe proactive na siyo kukaa na kusubiri tu...