Wonderful
JF-Expert Member
- Apr 8, 2015
- 7,347
- 5,986
Yanga imefanikiwa kupitisha jina la mshambuliaji wa zamani wa Zesco, Winston Kalengo.
Kalengo ametua Yanga baada ya jina lake kuwasilishwa katika nusu saa ya mwisho kabla ya dirisha ya usajili.
Taarifa zinaeleza, Yanga imepitisha jina hilo la Kalengo anayechukua nafasi ya Mzambia, Obey Chirwa.
Yanga imemrudisha Chirwa FC Platnums kwa mkopo, safari hii akiwa analipwa nusu mshahara na Yanga na Wazimbabwe hao watamlipa nusu mshahara.
Mjadala mkubwa kuhusiana na hilo, ndiyo ulichelewesha Yanga kuwasilisha jina hilo katika hatua za mwisho na imeelezwa Yanga wameliwasilisha katika majina ya wachezaji wao saa 5:36, ikiwa ni dakika 24 kabla ya usajili huo wa dirisha dogo kufungwa.
Pamoja na kufanya vizuri Zambia akiwa na Zesco, Kalengo aliwahi kucheza soka la kulipwa nchini Congo Brazaville na anaelezwa kuwa mkali wa kupiga mashuti, mwenye njaa ya mabao.
UP DATES:
Uongozi wa FC Platinums ya Zimbabwe, umegeuza dili la mshambuliaji Winston Kalengo kutua Yanga baada ya kukataa kulipa mshahara wa Obey Chirwa.
Yanga ilikubaliana na FC Platinums kuwa itampeleka Chirwa kwa mkopo kwa kuwa ilimtoa hapo ili Wazimbabwe wawe wanamlipa mshahara na kama ikitokea dili, wanaweza kumuuza.
“Kweli mwisho ikawa safi na Yanga ikaanza mipango ya kumsajili Kalengo. Kila kitu kimeenda safi na jina limepelekwa lakini inaonekana poa. Lakini mwisho FC Platinums wamekataa kulipa mshahara, sasa inakuwa vigumu kulipa watu wawili.
“Maana Chirwa aende FC Platinums tumlipe, Kalengo naye awe Yanga tumlipe. Imekuwa vigumu na uongozi umetaka kulipa mchezaji mmoja tu, hii imechangia Chirwa kubaki,” kilieleza chanzo.
Yanga ilikuwa imekubaliana kila kitu na Kalengo pamoja na Zesco na lengo lilikuwa ni kuongeza nguvu katika ushambulizi, jambo ambalo linaonekana limekwama