huu mpango lazima vyombo vya ulinzi na mifumo yake ilikuwa inaujua. viongozi wakuu ngazi ya Trump sio wa kuachiwa matundu dhaifu ya kuruhusu wahalifu watimize azma yao ovu kirahisi hivyo. tukiacha uchochezi na misimamo yaje dhidi ya utawala, yeye ni rais mstaafu-itifaki za ulinzi zilitimizwa? Trump kama mgombea machachari; suala la ulinzi wake waliachiwa walinzi binafsi pekee?
BBC kuna shuhuda aliona na kutoa taarifa mapema kwa vyombo, alimuona mlengaji akimnyooshea bunduki mzee Trump bado ikaachwa ilivyo.
sijui uchambuzi wa masuala ya usalama lakini kwa kiki za US na ubora wao kiteknolojia kama wanavyoutambia ulimwengu; tunajipa uhuru kuwananga au kuwashuku huu mpango 'ulisukwa'
Wanafunzi wa demokrasia kutoka Afrika, Latin America, Bara Asia (USSR, KIDUKU) wamejifunza nini kwa 'baba wa demokrasia' duniani? vipi ni wakati sahihi kwao kuyapuuza na kuyaona kama uonevu yale matamko ya kulaani na kuweka vikwazo kwa maafisa au serikali nzima zinazohatarisha usalama, haki za binadamu?