johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 97,869
- 171,716
Kuna wakati Zitto akiwa Chadema aliwaeleza madhara ya kuweka kanuni inayomfanya mwenyekiti wa Chadema kuwa KUB iwapo ni mbunge na chama kimepata ridhaa ya kuunda kambi rasmi ya upinzani.
Madhara yake ndio haya tunayoyashuhudia sasa. Binafsi sikumbuki kama kuna kikao halali iwe halmashauri kuu au kamati kuu kilikaa na kuamua wabunge wa Chadema waende kwenye karantini wakati bunge likiendelea.
Lakini jana mh Mnyika amedai wabunge waliofukuzwa na wale waliotakiwa kujieleza walikiuka maagizo ya chama kuwataka wajitenge kwa siku 14.
Ikumbukwe kuwa KUB hatoi maagizo ya chama bali anatoa maagizo ya kambi rasmi ya upinzani bungeni.
Wabunge wanaoendelea kuhudhuria bungeni hawajakiuka maagizo yoyote ya chama bali wameshindwa kukubaliana na kiongozi wao wa kambi na wanapaswa kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za kambi ambazo zipo kwa mujibu wa kanuni za bunge iwapo kweli wamefanya makosa.
Ni vema Mbowe akafahamu ipo tofauti ya MSINGI kabisa kati ya yeye kuwa KUB na yeye huyo huyo kuwa Mwenyekiti wa Chadema.
Mungu awape wepesi makamanda.
Maendeleo hayana vyama!
Madhara yake ndio haya tunayoyashuhudia sasa. Binafsi sikumbuki kama kuna kikao halali iwe halmashauri kuu au kamati kuu kilikaa na kuamua wabunge wa Chadema waende kwenye karantini wakati bunge likiendelea.
Lakini jana mh Mnyika amedai wabunge waliofukuzwa na wale waliotakiwa kujieleza walikiuka maagizo ya chama kuwataka wajitenge kwa siku 14.
Ikumbukwe kuwa KUB hatoi maagizo ya chama bali anatoa maagizo ya kambi rasmi ya upinzani bungeni.
Wabunge wanaoendelea kuhudhuria bungeni hawajakiuka maagizo yoyote ya chama bali wameshindwa kukubaliana na kiongozi wao wa kambi na wanapaswa kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za kambi ambazo zipo kwa mujibu wa kanuni za bunge iwapo kweli wamefanya makosa.
Ni vema Mbowe akafahamu ipo tofauti ya MSINGI kabisa kati ya yeye kuwa KUB na yeye huyo huyo kuwa Mwenyekiti wa Chadema.
Mungu awape wepesi makamanda.
Maendeleo hayana vyama!