YES Tunahitaji Apartments Tanzania Lakini si kila Mkoa


Sielewi ni kwa nini tunashindwa kuelewana ZeMarcopolo? Nina wasiwasi hoja yangu umeitafsiri tofauti, kama nilivyomjibi Koba hapo juu, Mimi sijasema ni mwiko kujenga apartments Tunduma na Katavi, no! Hoja yangu zikijengwa leo zitalipa ati kisa zinalipa Dar es Salaam? Tatizo la Chalinze ni maghorofa na location pia
 

Nashukuru umeanza kuielewa hoja yangu mkuu, bila shaka ZeMarcopolo akisoam uzi huu ataelewa nilichomaanisha maanake huenda sikueleweka vizuri katika thread yangu! Thanx MKATA KIU
 

Hapo umesahau kuwa kuna taaluma inaitwa MARKETING.

Ila siwashangai kufikiria hivyo kwa sababu hata Ulaya wapo watu wengi wanadhani si sahihi kufanya biashara Afrika.

By the way, apartments maana yake ni nyumba nyingi kwa pamoja. Ukisema kujenga apartments si sahihi unamaanisha kwamba kuna maximum number ya nyumba per investor zinazoweza kulipa? Je ni ngapi? Na kwanini zikiwa under one roof iwe tatizo?
 
Wakiendelea hivyo Oysterbay kutakuwa kama Kariakoo...

It will. Tusubiri miaka 20 ipite maana nasikia eti "waliouziwa" zile nyumba "waliuziwa" on the condition that wasiziuze ndani ya miaka 20.

Sina uhakika na hili, ila kama ni kweli then baada ya miaka michache ijao Oysterbay will no longer be the one we used to know.
 

Zaidi ya mwaka sasa, Mh. Waziri ametoa katazo la undelezaji na ubadlishaji matumizi! Kunalimitation ya kujenga ghorofa katika maeneo ya Oysterbay na Msasani Peninsula, sio free style kama ilivyokuwa hapo awali na ndio maana hata bei za viwanja kidogo zimepoa
 

Sikubaliani na hoja yako ikiwa Africa ndiyo imeifanya Ulaya iendelee, kasome historia!

Hoja yangu niliongelea apartments kwa maana ya vertical development au flats ukipenda! Definition yako unamaanisha nyumba nyingi kwa pamoja ambazo kitaalamu zinaitwa town house, villas, detached homes, strata n.k! Ni tofauti na nilichokuwa nakiongelea! Ndio maana ninasema inawezekana hujaelewa msingi wa hoja yangu! Hivi mimi nimesema kujenga apartments si sahihi? Unaonaje urudie kusoma hoja yangu uielewe vizuri au ni para ipi haikueleweka labda, maana noana unajadili na kung'ang'ania hoja ambazo haziko katika theme ya thread yangu!
 

Iwe appartment za ghorofa, ama nyumba za chini etc, nyumba yeyote kwa ajili ya biashara tukifata cost benefit analysis kujengwa kwenye baadhi ya mikoa sio sahihi.. Labda kama unajijengea tu uonekani nawe unamiliki appartment..

Wewe mikoani utampangisha nani kwa kodi ya kuridhisha, au unajijengea tu mradi uwe na appartment, walioweka cost benefit analysis sio wapumbavu, business yeyote lazima ifate kanuni za kibiashara ambayo mojawapo ni demand analysis, cost benefit, target customer uwe nao, na mengineyo, sasa huko mikoani target customer wa hizo appartment ni kina nani? Walimu, polisi, wafanyakazi wa halmashauri, NMB au Tanesco maana hao hio ndio working class iliyojaa mikoa yote
 
Hapo umesahau kuwa kuna taaluma inaitwa MARKETING.
Kuna MARKETING lakini usisahau kuna SALES pia! Unaweza kufanya marketing (awareness creation) ya kutosha lakini ukashindwa kubreak through, SALES (persuasion) ikawa ishu!
 

ZeMaecopolo hataki kukubali kwamba kuna business na ecomomics principles!! Hivi vitu haviepukiki mkuu!
 
Hilo katazo halitakaa milele. Wengine watafika mahali wata ignore hilo katazo. Unafiki sehemu nyingine amabazo zimejegwa kiholela hakuna hayo makatazo?
 

Inashangaza kuona bado mpo mnaoamini kuwa nyumba ina thamani Dar tu. Kwahiyo mikoani mnashauri kusijengwe?
 

Hivi mkuu sheria gani inayoruhusu kumuuzia mtu property na kumkataza kuiuza. Hii mbona iko unconstitutional?
 
Sikubaliani na hoja yako ikiwa Africa ndiyo imeifanya Ulaya iendelee, kasome historia!

Maendeleo ya Ulaya hayajasababishwa na Africa. Huko usiingie kabisa kwa sababu ni mada nyingine na ndefu. Nilichokuwa nasema ni kwamba Ulaya wapo watu wengi tu wanaoamini kuwa Africa huwezi kufanya biashara ya nyumba kwa sababu wanafanya assumption kuwa kila mtu masikini. Hivi hujawahi kukutana na mtu akakuuliza nchini kwenu nyumba zikoje? Mnakula nini? etc
 
Sikubaliani na hoja yako ikiwa Africa ndiyo imeifanya Ulaya iendelee, kasome historia

Hebu tupe brief ya hiyo historia uliyosoma, au at least list ya vitabu nikapige shule ya histori.

Kwenye historia upande wa Afrika, mie nilisoma "How Europe Underdeveloped Africa" by Walter Rodney.

Mwandishi aliandika kitabu hiki miaka 1960s mara tuu baada ya nchi za Kiafrika kujipatia uhuru wao.
 

Hivi kweli unaamini Europe ilii-underdevelop Africa? Mimi naona hicho kitabu cha bwana Rodney kimekaa kipropaganda zaidi kuliko kiuhalisia.

Africa ilikuwa underdeveloped hata kabla Europeans hawajaja.
 
Hivi mkuu sheria gani inayoruhusu kumuuzia mtu property na kumkataza kuiuza. Hii mbona iko unconstitutional?

Zipo sheria zinazoweza kuzuia siyo tuu kuuza nyumba bali hata kufanya marekebisho yanayobadilisha mwonekano wa hiyo nyumba.

Sheria za aina hiyo zinatumika sana kwenye listed buildings or heritage/historical buildings kama njia mojawapo ya kulinda majengo muhimu.

A listed buildings (hasa majengo ya Grade 1) hayawezi kubomolewa, kupanunuliwa, kufanyiwa marekebisho au hata kuuzwa bila idhini maalumu kutoka planning authority.
 
Hivi kweli unaamini Europe ilii-underdevelop Africa? Mimi naona hicho kitabu cha bwana Rodney kimekaa kipropaganda zaidi kuliko kiuhalisia.

Africa ilikuwa underdeveloped hata kabla Europeans hawajaja.

Inategemea una maana gani by the term "underdevelopment".

Kilichosabisha African underdevelopment ni complex issue, but Europe imechangia pia.

Whether or not hicho kitabu ni propaganda, inategemea na approach yako kwenye suala zima la uhusiano kati ya Europe na Afrika.

Basically, zipo three major views, Eurocentric approach, Afrocentric approach and historical approach.

Inadaiwa hiki kitabu ni baadhi ya vitabu vichache ambavyo at least vimejaribu kuangalia suala from the historical point of view.

Having said that Waafrika nao wamechangia na bado wanaendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa tuu to their own underdevelopment. Maana tokea uhuru, we are still underdeveloping

 
Last edited by a moderator:
Inategemea una maana gani by the term "underdevelopment".

Kwani wewe kwako hilo neno linamaanisha nini?

Kilichosabisha African underdevelopment ni complex issue, but Europe imechangia pia.

Kama Europe imechangia basi mchango wake ni mdogo sana. Na kwanza sielewi hata imechangiaje wakati kulikuwa hakuna lolote la maana kabla wazungu hawajaja.

Whether or hicho kitabu ni propaganda, inategemea na approach yako kwenye suala zima la uhusiano kati ya Europe na Afrika.

Basically, zipo three major views, Eurocentric approach, Afrocentric approach and historical approach.

Hicho kitabu kimeandikwa kutoka kwenye mtazamo wa Afrocentric, kwa maoni yangu.

Inadaiwa hiki kitabu ni baadhi ya vitabu vichache ambavyo at least vimejaribu kuangalia suala from the historical point of view.

Hmm...nani anadai hivyo? Maana mimi naona ni kana kwamba kinataka kuaminisha watu kwamba Afrika ilikuwa sawa na Ulaya kwa kiwango cha maendeleo wakati watu wa hayo mabara mawili walipokutana. Mimi hiyo dhana sikubaliani nayo kabisa. Kama tulikuwa sawa kimaendeleo iweje wazungu waje watu bamboozle kiasi hicho?

Having said that Waafrika nao wamechangia kwa kiasi kikubwa their own underdevelopment. Maana tokea uhuru, we are still underdeveloping.

Siyo tokea uhuru tu. Hata kabla ya uhuru hakukuwa na lolote la maana hadi wazungu walipokuja na kuanza kusomesha watu wetu maana sisi wenyewe hatukuwa hata na shule za maana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…