Yesu hakuwa na Kanisa wala pesa, hakuacha hata hao wakristo. Je, hawa wanapata wapi haya wanayofanya?

Yesu hakuwa na Kanisa wala pesa, hakuacha hata hao wakristo. Je, hawa wanapata wapi haya wanayofanya?

Father of All

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
7,672
Reaction score
9,039
Kwa waliosoma na kuelewa habari za Yesu watakubaliana nami yafuatayo:

Mosi, alikuwa maskini au lofa wa kawaida mwana wa seremala ambaye kama angerudi leo na kukuta wanaomhubiri na utajiri wao haramu, angezimia mbali na kuwakaripia hata kuwachapa.

Pili, hakuwahi kuwa na wala kuingia kanisani.
Tatu, aliingia kwenye masinagogi na kuhubiri humo.
Nne, aliacha wanafunzi na si wakristo.

Tano, hadi anaondoka, hakuwahi kusikia neno ukristo.
Sita, hakujitangaza kuwa alikuwa akitenda miujiza kama hawa majizi wa sasa wanaomtumia na kumsingizia.

Saba, alisema wazi kuwa alikuja kwa ajili ya kabila 12 za Israel ingawa tapeli Sauli baadaye Paulo alikuja na kugeuza kila kitu kiasi cha kuunda dhehebu ndani ya dhehebu.

Nane, hakupenda sifa wala ujiko kama haya majizi ya sasa yanayotumia runinga kuwaibia mazwazwa.

Tisa, hakuwahi kushirikiana na serikali kwa vile alijua uhovyo na uovu wake.

Kumi, hakuacha uislam ambao nao ulimdandia kujifanya unamtambua ili kuwanasa wakristo.

Kumi na moja, alipenda kukaa na watu wa tabaka la chini na siyo wakwasi na wenye madaraka.

Kumi na mbili, hauandika wala kuacha biblia.

Je wewe unasemaje?
 

Warumi 8:14-17​

Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu. Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba. Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.

He wewe mleta mada unaongozwa na roho yupi?
 
2 Wakorintho 8:9
[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

For ye know the grace of our Lord Jesus Christ, that, though he was rich, yet for your sakes he became poor, that ye through his poverty might be rich.


Shabanii wewe shabanii!
Hudhuria Vikao... Kikao cha Mwisho Hukuwepo
 
Matthew 17:24-27 inasema yesu alimwambia peter adake samaki, alafu afunue mdomo wake atakta hela akalipe ushuru.
Na pia yeye mahitaji yake yote alikua akiangalia mbinguni akimuomba baba yake yaani mwenyezi Mungu ampe hitaji la moyo wake, ila hakua akitembea na pesa.
Na hajawahi kuomba mtu pesa.
Luke 8:3. Inaelza yesu alikua akipata msaada wa kifedha kupitia ministry yake. Wapo watu walikua wakimsupport kwasababu ya preaching
 
Aliwaambia msitoke yerusalemu mpaka mtakapopokea nguvu. Walipopokea nguvu wakatoka yerusalem kwenda kuhubiri injili yudea, samaria na miisho ya dunia. Ukristo ulianzia antiokia, wakristo maana yake wafuasi wa kristo, hapo ndipo kanisa lilipoanzia ingawa kanisa lipo tangu kale na bado halijanyakuliwa itakapofika siku ya unyakuo
 

Warumi 8:14-17​

Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu. Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba. Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.

He wewe mleta mada unaongozwa na roho yupi?
Maneno haya kazungumza mwenyewe yesu ama?
 
Mosi: yupo macho, na anawaona na alitoa unabii kuwa wangekuwapo(mathayo7:15)
Tatu: alihubiri kwenye masinagogi yao, barabarani, na nyumba kwa nyumba.
Sita : kazi iliyo mleta haikua kufanya miujiza, ilikua ni kuhubiri/kufundisha kuhusu ufalme wa Mungu (luke 4:43)
Saba : alikuja kuboresha kutoka waisraeli kua watu wamungu nakua wenye imani(watu wote) kuwa watu wamungu. Pana mjadala mrefu hapa boss.
Tisa : alikuja kutufundisha kuhusu ufalme wa Mungu, serikali itakayo tawala wanadamu kwa amani na haki (danieli 2:44)
Kumi na mbili : Biblia aliikuta, aliitumia kufundisha ingawa ilikua bado inaandikwa.

Kristo aliaacha wanafunzi, wafuasi wake ambao aliwapa kazi moja tu, kuendelea kuhubiri habari njema kuhusu ufalme wa Mungu kwa watu wote,ulimwenguni pote(mathayo 28:19-20)
Watu hao wanatoka katika makabila na jamii tofauti, lakini wameungana nakua kikundi kimoja ulimwenguni pote na alama yao ni upendo(Yohan13:35)
Watu hao hawajihusishi na siasa kwa namna yoyote ile kama alivokua yeye.
 
Ukishakuwa muumini tu basi, hapo tayari umeshakuwa wewe ni kichwa boksi
Unashikiwa akili na unaowaamini
 
Kwa hiyo ulitaka tuseme nini sasa kupitia haya maelezo yako? Si umeshasema wewe mfuasi wa Mtume, inatosha?
Wapi nimesema kama siyo kuniweka maneno mdomoni mwanangu? Soma kipengee cha kumi utajua nisivyo na mafungamano na huu usanii.
 
Sasa mbona hicho kipengele cha 10 hakina uhusiano na swali langu! Au unafikiri hapa duniani kuna Mtume mmoja tu!
Sijui kama umeelewa unachojibu na kudai. Maana, inaonekana hata hicho kifungu hujakielewa.
 
Shida yako kubwa unataka kila mtu anayechangia huu uzi wako, basi achangie kwa mtazamo unaoutaka wewe. Na hapa ndipo kwenye tatizo kubwa.
Si kweli. Kwani wangapi waliozusha na kuzua wamelalamika kama wewe? Unategemea ni kubali kuwa mimi ni muumini wa hizo dini zenu? Ukizua au kupokoma nikubali tu mwanangu?
 
Watu wengi hawajui wanacho kosoa hawajasoma Biblia na wakisoma hawaelewi basi kutokuelewa inakuwa tatizo..

Kasoma tena Biblia hakikisha unajua haya;
》Yesu ni nani
》Alikuja duniani kufanya nini
》Nini maana ya Kanisa
 
Watu wengi hawajui wanacho kosoa hawajasoma Biblia na wakisoma hawaelewi basi kutokuelewa inakuwa tatizo..

Kasoma tena Biblia hakikisha unajua haya;
》Yesu ni nani
》Alikuja duniani kufanya nini
》Nini maana ya Kanisa
Tupe elimu ya bure basi mwanangu kama nawe unajua.
 
Mtoa mada umejitambulisha kuwa ni mbumbumbu

Marko (Mar) 9:41
Kwa kuwa ye yote atakayewanywesha ninyi kikombe cha maji, kwa kuwa ninyi ni watu wa Kristo, amin, nawaambia, hatakosa thawabu yake.
 
Back
Top Bottom