tata mvoni
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 534
- 81
kweli mkuu hata mimi nakumbuka.ni enzi zetu zileee za kudanganyana.thanks to whoever invented google....ila mimi napenda kujua alipo mwanamziki GATO.ilivumishwa miaka ile eti alikutwa na madawa ya kulevya na akafungwa.nam google ila info zake ni kama hazipo.
African Ball, wimbo wa Loketho Group chini ya Aurlus Mabele, gitaa alilopiga Dally Kimoko alibadilisha mipigo mara33, mipigo na beats tofauti zote 33 zikiwa kali na hazifanani. Kiukweli Dally Kimoko anasifika kwa kupiga mpini(gitaa). Tumia You tube au kama una CD-VCD-DVD cheza huo wimbo -African Ball- Loketho Group& Aurlus Mabele halafu sikiliza kwa makini mipini ni hatari.
extra ball solo imepigwa na mchawi wa nyuzi Diblo Dibala Machacha .huu wimbo hata dally kimoko mwenyewe aliyoosha mikono kwa diblo
Sanaaaaaaa na Imenibamba mwenzangu,, naenda kinshasa kwa miguu ndo kwanza nipo bujumbura sijui ntafika lini!!!!!!!!!!!
oooh Toweli nini tinna cute?
wewe!!!!!!!!!!!!
nini tena..........
Kwan DIBLO na DALLY KIMOKO nan zaid?
CHAZA......
Uzuri wa Diblo unadhihirika kwenye nyimbo nyingi.....Naomba nikuwekee hizi mbili hapa chini Tobina, Matchatcha Laisser Passer(ambao kuna sehemu gita linapigwa utafikiri limemwagiwa maji) na Extra Ball.......Kisha nikuombe uweke nyimbo ambazo unadhani Dally Kimoko amemshinda Diblo Dibala......
Mimi naona kwa kizazi chao hakuna anayemfikia Diblo Dibala mkuu wangu....Diblo yupo juu halafu wanamfuatia akina Dally Kimoko, Lokassa Ya Mbongo, Nene Tchakou, Allain Makaba 'Prince' , na Roga Roga (wa Congo Brazaville)......
Ni sawa na useme Gode Lofombo alikuwa ni zaidi ya Ngouma Lokiti katika kulikung'uta gitaa zito la bass.....
Diblo ni mchawi wa gitaa Africa hii.
Diblo ni mchawi wa gitaa Africa hii.
wabongo aisee, swali moja majibu kibaaaooo
Mtu kaulizia Yondo sister, kama kawaida wakware tunashusha data za akina diblo, sukus sijui na nini na nini
aisee:A S-confused1::A S-confused1::A S-confused1::A S-confused1:
Kwani kuna ubaya gani? Au imekuuma?!wabongo aisee, swali moja majibu kibaaaooo
Mtu kaulizia Yondo sister, kama kawaida wakware tunashusha data za akina diblo, sukus sijui na nini na nini
aisee:A S-confused1::A S-confused1::A S-confused1::A S-confused1:
Kaka, hivi nani alipiga mpini wa nyimbo hizi: Evelyne-Aurlus Mabelle, Missete- Lucien. Leo pia tuwaguse Wenge BCBG. Kuna watu mi huwa wananikuna sana hasa album tatu za Wenge Musica BCBG chini ya Jean Badel Mpiana. Album hizo ni Titanic- Internet na Toujours Humble(TH) .Watu wenyewe wa kwanza ni Jules Kibens( le' professior), Alain Mpella( Afande), Aimelia Lyesse Demingongo, Chai Ngenge, Rio, Burkinafasso, Titina Alcapone ambae ni mpiga drums, lakini kwenye album ya Titanic alitunga wimbo uitwao Tour Eiffel(ule mnara maarufu wa pale jijin Paris). Nyimbo zifuatazo zina ladha tamu kuzikiliza kutoka kwa wenge bcbg! Nyimbo hizo ni: TH, Education, 48 Heures Gecoco,Walay Danico( hizi kutoka Album ya TH), Liberation, Tour Eiffel,Champion Kapangala, Omba( Album Titanic) na Internet, le' spo'ir de Chicago na love force za album ya Internet. Japo album za nyuma ambazo Wenge ilikuwa imetimia zilikuwa nazo ni nondo. Nyimbo kama pile ou face, no comment shenghen, Filandu, ndombolo, hi ho ha, kalayi boeing, masuwa, conse'il patcho, banalunda na feu'x d' la' mour utakubali jamaa walikuwa poa.
Champion Kapangala moto wa kuotea mbali,wakati huo Emelia anatisha, BCBG moto wa kuotea mbali
Pamoja mkuu. Mi ni mpenzi wa Wenge BCBG ya JB M'piana. Wenge Maison Merre mi siwakubali kiivyo, japo Werrason na Didier Masella , bila kumsahau Adolph Dominguez ndo hasa magwiji wa mwanzo kuanzisha Wenge, wakamwita JB M'piana nae kaifanya Wenge iwe juu. Ila ubinafsi wa JB M'piana wa kutunga yeye nyimbo karibia zote na kuimba yeye karibia nyimbo zote album ya Feu'x d' l'mou'r na mkwanja karibia wote kutia kapuni pekeyake kuliwakasirisha sana wenzake, na hivyo kuamua kujitenga. Werrason akaanzisha Wenge Maison Merre na kutunga album na wimbo: Force de Intervention Rapide( Jeshi la uvamiz linalokuja kwa kasi) na Wenge BCBG ikaja na Titanic kumaanisha meli ile iliyozama! Hapa utagundua walitumia Music kutupiana madongo
mkuu sio ubinafsi wa Jb mpiana, bali ilikuwa ni makubaliano kuwa kila mwanamuziki wa wenge bcbg atoe solo albam. ndipo jb akaanza kutoa project yake ya albam ya fex de lamour wimbo uliompa tuzo nyingi. albam hii maarufu kama ndombolo ya solo ikauza sana kuliko hata albam za wenge bcbg walizozitoa kama kundi, kwa kuwa alishirikisha baadhi ya wana wenge, wakataka waifanye albam ya kundi na wagawane mapato, jb akakataa, ndipo zilipoanza futina na zikiongozwa na werason ngiama makanda wa meison mere, akazushiwa jb ni mshirikia alienda hadi kwa mganga akanyweshwa damu ya mtu ili apendwe zaidi. na hii iliwauma baadhi ya wana bcbg hasa wale waliokuwa ndio waasisi wa bendi waliomkaribisha jb kisha kuja kuwa kinara zaidi yao. mwisho watu wakagawana mbao,meli ikazama, wengi ikamegika vipande, marie paul akaanzisha bendi ya wenge el paris, werason akaanzisha wenge meison mere,baadaye adolf domingize akaanzisha wenge tonyatonya,blaize bula nae akatoka kivyake.
ila kiukweli bendi zilizitakana na wenge bcbg ziliziweza kusimama mpaka sasa ni ya wenge ya werason na jb mpiana.
sasa kati ya wera na jb, wera son akabaki kuwa sio mtunzi mzuri wala muimbaji mzuri bali ni muandaaji wa show nzuri,kwa masebene tu na uchezaji wako vizuri kuliko wenge ya jp mpiana. kwa upande wa wenge ya jb, jb mpiana ameendelea kuonyesha kuwa yeye ni mtunzi na mwimbaji bora na imethihirika wazi kuwa yeye ndiye aliyekuwa anaibeba wenge bcbg 4x4 by far kabla haijavunjika kiumbaji na kimpangilio wa muziki.jamaa ni mpangiliaji mzuri saana wa muziki na mwinbaji mzuri. tafuta show ya jb live at kinkole ndio utajua jb ni nani