Yuko wapi FaizaFoxy wa JamiiForums?

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Wasalaam bibie FaizaFoxy popote pale ulipo.

Kwakweli mimi binafsi nimeu-miss (kama tunavyosema vijana wa kileo) mchango wako humu jamvini!

Siyo kawaida yako kuacha kuisifia serikali yako pendwa ya chama chako pendwa cha CCM ila kwa sasa mmh! Upo kimya sana bibie! Nini tatizo?

Najua unau-miss sana utawala wa rafiki na kaka yako kipenzi Dr. Jakaya Mrisho Kikwete lakini ndo hivyo tena, umeshapita! Kumbuka kuwa mtu akiwa anakimbiza sakafuni basi mwisho wa mbio zake ni ukingoni mwa sakafu!

Nitakuwa sina busara na hekima nisipo kupa pole kutokana na sekeseke lililoikumba sehemu yako kuu unayopata ugali wako na familia yako!

Jana nilipita maeneo ya Ilala na nikapokea taarifa kuwa nyumba zote za Ilala kuanzia kule Jangwani hadi karibu kabisa na zilipo nyumba za NHC karibu na Ilala Boma zinapigwa tingatinga! Hapa nikawaza tena kama mpendwa wangu huyu hatakuwa kapata janga la pili kweli?

Ninaipenda CCM #mbelekwambele
#Sinywi sumu sijinyongi
#Acha waisome namba
 
Ngoja waje wazee wa kuisoma namba watakujib
 
Nasikia vijana wote mlio karibu ma babu slaa mnatimuliwa chadema! Karibuni sana ccm, chama pendwa Tanzania
 
atakuwa kapata uwaziri wa magufuli au ni mmoja wa watu walioisoma namba. sasa kafunga domo kaya lake.
 
Nasikia vijana wote mlio karibu ma babu slaa mnatimuliwa chadema! Karibuni sana ccm, chama pendwa Tanzania
Watatimuliwa sana hawa misukule. Chama kibaki na mafisadi tu na mawakala wao
 
bibi faiza foxy vibanda vyake vyote vya town vimepigwa x nasikia.... alafu na kule kijijin kwake hali si swari maana nasikia alijenga kwenye eneo la wazii...huko alipo presha imemshuka kama wastara sajuki....uwiii steph curry njoo umpe pole bibi etu...
 
Mbona kiama tumuombeee asije akajinyonga
 

Asalaam Alaikum.

Ahsante kwa kuni miss. Nipo ingawa kasi imepungua kiasi.

Kwa wale wanaonisoma humu, wengi wao wanaelewa miezi hii huwa kasi yangu ya kuingia JF inapungua sana kwa sababu za ukulima. Moja kati ya kazi zangu nizipendazo ni shamba, na huu ni msimu wa kutayarisha mashamba basi nnakuwa busy kupita kiasi.

Nipo sana.

Mengine ntajibu baadae.

#HapaKaziTu
 
Tukiacha ushabiki wa kivyama mie huwa nakukubali sana #FaizaFoxy
 
Unafaa uwe kwenye blog za udaku special.

Nashukuru, kuanzia majumba ya urithi mpaka ya kujenga mwenyewe hakuna lililopo bondeni na hakuna lililoathirika na ikitokea siku kuwa lipo litalobomolewa kwa kupitisha maendeleo basi ntakula mkwanja mzuri tu na sinto-sita kuachia kwa ajili ya maendeleo.

Shamba au niseme mashamba nna maeneo ya kulima mpaka mengine nilitoa offer humu JF kwa atakae kulima aje kulima na waliochukuwa fursa hiyo sasa wanafaidika, mambo swaaafi kabisa.

AlhamduliLlah nipo tena nashukuru nipo fit kabisa na hivi nipo busy kijijini natayarisha mashamba, ndiyo msimu wake huu.

Karibu maembe dodo, msimu ndio unamalizikia, huku kwetu embe dodo moja lilikuwa shillingi 200 sasa yamefika 300. Njooni fursa hiyo, Dar yanafika mpaka 1,000 kwa reja reja.
 
Last edited:
shikamoo bibi... nilikumiss nikaona nichezee kidevu chako kwa kukutania... nitakutafuta bibi yangu unipe japo heka moja nilime na kufuga kuku... heri ya mwaka mpya bibi...
 
Mkuu leo ni mojawapo ya siku ulizojibu kwa Hekima, bila kejeli wala Hasira.
 
Sasa Nikutakie Heri ya Mwaka Mpya shoga yangu Faizafox unayejulikana JF huenda kukliko hata Mzizimkavu na Mshana JR
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…