Yuko wapi Mr Paul?

Yuko wapi Mr Paul?

kwa watakaopenda kumfahamu zaidi mr paul...

tuliwahi kufanya mahojiano na Mr Paul, Mr.Paul ambaye jina lake kamili ni Paul Mbena hivi sasa anaishi nchini Australia akiwa ameoa na ana mtoto mmoja, pia ni muajiriwa anafanya kazi kama Case Manager katika Brain Injury Rehabilitatioun Unit, Liverpool hospital huko huko Australia na bado anaendeleza muziki akiwa na kundi la Okapi Guitars, safari hii tulitaka kujua mengi kuhusu kundi hili ndipo nilipomuuliza Okapi Guitars na akina nani na wameanza lini kazi ya muziki?


Okapi Guitars imeanza lini?

Mr Paul: The Okapi Guitars ni Afropop bendi ya muda mrefu (since 1990s) hapa Sydney. Mimi nilijiunga nayo mwishoni mwa mwaka jana November 2011 nikiwa mwaka wa mwisho Melborune University. Okapi Guitars wana historia ya muda mrefu katika medani ya muziki wa Kiafrika. Wamekuwa wakipiga Zimbabwean chimurenga to Kenyan classics, to West African hi-life and afrobeat. The Okapi Guitars, kabla ya mimi kujiunga nao, wame-share stage na bands kama the Mahotella Queens (South Africa), Tchico Tchicaya (Congo), na Oliver Mtukudzi na Thomas Mafumo (Zimbabwe)
Hivyo kujiunga kwangu na the Okapi Guitras ni nafasi kwangu kutangaza muziki wa Kiswahili toka Tanzania.

Kuna wananmuziki wangapi?
Mr Paul: The Okapi Guitars ina jumla ya manamuziki watano, pamoja na mimi kama lead singer. Wengine ni:
· John-Rhythm guitar
· Bernhard – Lead guitar
· Sigi- Bass guitar
· Chris- Drummer..


mr paul himself..

sundeck-paul.jpg
 
Dah leo nimetupia album ya Mr Paul (Ndani ya love) kwenye gari nikielekea shamba.. Album hii nilinunua kipindi nipo form one, nimeitunza mpaka leo. Album inanyimbo tamu sanaaa,,, zote ni tamuu hakika nimekuwa nikiisikiliza miaka yote lakini nyimbo za jamaa hazichoshi masikioni mwangu kamwe!

Potepote ulipo Mr Paul tambua yakuwa tumekumiss sana ndugu zako,,, rudi kwenye muziki kama utaweza bro... RnB za kiswahili wewe ulikuwa ndio Mfalme kaka!

Rudi mkuu... Rudi mkuu....
 
Duu wengine church, wengine kula debe, wengine kujulia hali ndugu na jamaa, wengine week end kwenda kutembelea mashamba nice mkuu jamaa namkubali sana haswa ile remix aliyopiga.

Ilikuwa asubuhi namapema jua linachomoza ooh mama...

Aaah kitu cha Zuwena . Ila ndo ivo kizuri hakidumu. Km vp arudi aje kuahindana nakina jux, ben...
 
Penzi ibilisi
Nilijimix
Kwako moyo niliuweka
Ikawa dili
Nikawa sikosi
Blue palm billz mambo niko nawe
Oh no ukaniona buzi.
 
Lakini kweli jamaa nyimbo zake zilikuwa tamu sana!! Na yule mama yao yuko wapi tena!!
 
Katika waimbaji wa RnB bongo, jamaa hana mpinzani wa sauti, anaimba sauti ya ukweli haswa.
 
Ooh Zuwenaa!! Ooh Nitampata wapi...
Eeeh zuwena!! Zuwenaa Nitampata wapi..!!
Mtoto aliyeumbika,tabia za kupendezaa..
Zuwenaa! Zuwenaa!! Kweli nakupenda
 
Back
Top Bottom