Yuko wapi msanii mkongwe Norbert Chenga?

Jaylee

Member
Joined
Apr 15, 2009
Posts
66
Reaction score
96
Wale wapenzi wa sanaa na hasa ngoma za asili kipindi cha miaka ya 80 hadi 2000 bila shaka watamkumbuka Norbert Chenga na kikundi chake cha Muungano Dancing Troupe aliyejizolea umaarufu kutokana na uwezo wake wa kuchezea nyoka. Je msanii huyu kwa sasa yuko wapi?

Kipindi hiki vikundi vya Kibisa na wengineo waliwika sana katika tasnia ya ngoma za utamaduni, sarakasi, mazingaombwe na kadhalika.
 
Kaka umenikumbusha mbali... Nilikuwa siwakosi pale kijiji cha makumbusho kijitonyama na silent inn mwenge. Never miss... Ilikuwa burudani sana; umenikumbusha kina Small wangamba, alwatan minyugu, God, pili, na wengine wengi. Kwa kweli naimiss sana burudani hii.
 
Pumzika Kwa amani Small Wangamba,Pacha wako Majuto amekufuata.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…