Yule Mfungwa aliyemshtaki Askari kwa Magufuli anaendeleaje?

Yule Mfungwa aliyemshtaki Askari kwa Magufuli anaendeleaje?

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
4,016
Reaction score
6,759
Takriban Miaka 3 iliyopita Rais aliyekuwa madarakani (hayati JPM) alitembelea gereza la Butimba, Mwanza kwa ajili ya kukagua maendeleo katika gereza hilo. Naam alijitokeza kijana mmoja ambaye alikuwa na mfungwa na kutoa tuhuma kadhaa dhidi ya askari fulani gerezani hapo.

Tuhuma zile zilimletea askari yule tafrani na kumfanya akabiliane na maswali kadhaa toka kwa hayati JPM, ilipelekea chupuchupu bwana huyo apoteze kazi yake. Baada ya hapo mfungwa yule aliomba Rais aondoke na askari huyo kwani akibaki, atamfanya kitu mbaya. JPM alimwambia abaki hapo na atamuhakikishia usalama wake (HATAMFANYA MBAYA).

Naam siku zimekwenda. Je, yupo wapi mfungwa huyo, hali yake inaendeleaje huko alipo? Mwenye taarifa za Afande yule pia anisaidie kunijuza.
 
Avatar ya mkuu Stuxnet ina picha ya huyo askari magereza. Watu mnafukunyua sana hizi picha mnazotumia hapa JF.
 
Ila yule jamaa ni mwamba kweli kweli kuweza kubishana na jiwe bila kutetereka.

Nakumbuka alisema umekuja kuniinua [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom