Hakuna alie bora kati yao wote ni waathirika tu, labda mwenye afadhali.
Nipo kwenye daladala hapa Buguruni Makumbusho. Kuna mabishano kati ya konda na abiria kuhusu yupi bora kati ya mvuta sigara na mnywa pombe.
Konda anasema mvuta sigara ni bora maana akishavuta anapiga mswaki anakuwa fresh ila wanawake wanampinga wanasema mvuta sigara anaboa mana mwili unanuka sigara na ndani kuna nuka sigara.
Konda anaendelea: Mnywa pombe, pombe haishii mdomoni tu, bali mpaka chooni akienda kukojoa pombe inaonekana.
Sent using
Jamii Forums mobile app