Yusuph Manji achukua fomu za kugombea uenyekiti wa Yanga!

Yusuph Manji achukua fomu za kugombea uenyekiti wa Yanga!

Ochu

JF-Expert Member
Joined
May 13, 2008
Posts
976
Reaction score
47
Yusuph Manji achukua fomu

04/06/2012


Taarifa rasmi na za uhakika alizozipata Shaffi Dauda kutoka makao makuu ya klabu ya Dar Young Africans almaaruf Yanga Sports Club, zinasema mwanachama maarufu na tajiri wa klabu hiyo, mfanyabiashara Yusuph Mehebob Manji amechukua fomu za kugombea nafasi ya Uenyekiti wa klabu hiyo.

Manji ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa akiisadia Yanga kiuchumi zaidi, alikwenda kwenye makao makuu ya klabu hiyo na kuchukua fomu za Uenyekiti bila kuweka wazi kama ni kwa ajili yake au amemchukulia mtu kwa ajili kugombea nafasi hiyo.

Kwa siku kadhaa sasa kumekuwa na taarifa juu ya Manji kutaka kugombea nafasi hiyo japo mwenyewe bado hajathibitisha, ingawa kitendo chakecha leo kimezidi kuupa nguvu uvumi wa kwamba anataka kugombea nafasi ya kuwa bosi wa Yanga.

Wakati huo huo taarifa nyingine zinasema kuwa aliyekuwa mjumbe Kamati ya Mashindano ya klabu ya Yanga, Abdallah Ahmed Binkleb naye muda wowote kutoka sasa atadondoka makao ya Yanga kwa ajili ya kuchukua fomu za kugombea umakamu mwenyekiti.

Mwanachama mwingine maarufu wa klabu hiyo Issac Mazwile naye ameshachukua fomu za kugombea nafasi ya ujumbe wa kamati ya utendaji.

Naye Mkuu wa wilaya ya Handeni, bwana Muhingo Rweyemamu amechukua fomu ya kuwania nafasi ya ujumbe katika uchaguzi huo uliopangwa kufanyika Julai 15, 2012. Katibu wa kamati ya uchaguzi ya Yanga Francis, Kaswahili amemwambia Dina Ismail kwamba jana kwamba wanachama hao wanafanya idadi ya wagombea waliochukua fomu za kuwania nafsi mbalimbali za uongozi katika klabu hiyo kufikia 10 (baada ya taarifa hapo juu ya Manji kuchukua fomu, sasa idadi itakuwa 11).

Mbali na hao, wanachama wengine waliochukua fomu ni pamoja na John Jambele anayewania Uenyekiti, huku Ayoub Nyenzi akiwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti, "Waliochukua fomu kuwania ujumbe wa kamati ya Utendaji mbali na Muhingo na Binkleb ni Isaac Chandi, Jumanne Mwamwenye na Salehe Hassan," alisema.


Source: wavuti - wavuti
 
so wat? fisadi kupata umaarufu kupitia timu yangu ya yanga?
 
so wat? fisadi kupata umaarufu kupitia timu yangu ya yanga?

ww utakuwa yanga mamluki tu.Huyo ndio abromovic bwana,amekuja kusawazisha bao zenu 5 za kishirikina,na kuchuana na azam kimaendeleo,nyie mtabaki na "simba tv" yenu hapohapo na uwanja hewa
 
Habar zilizoenea mitaa ya twiga na jangwani, ni kwamba mfanyabiashara maharufu tanzania , na mdhamin wa yanga, Yusuph Manji kachukua form za kugombea nafasi ya uenyekiti yanga. Yalisemwa, na yanaelekea kutokea!
 
Kugombea uwenyekiti ni haki ya kila mwanachama, lakini taarifa hizo zilikanushwa na mwenyekiti wa kamati ya uchahuzi.
 
Huyu ndo ataibadili yetu, wana yanga tuwe wavumilivu ili aifanye kampuni tumiliki hisa kupitia mahela yake.
 
Huyu ndo ataibadili yetu, wana yanga tuwe wavumilivu ili aifanye kampuni tumiliki hisa kupitia mahela yake.
yap, mahela yake ya ufisadi. no wonder hata tiketi za kuingilia uwanjani alishawahi kuamuru ziandikwe maandishi ya kuran, akifikiri wana yanga wote ni waislam....
 
Sasa ni rasmi yanga itaongozwa na fisadi kama CCM.................

kwani manji anacheo gani serikalini, hadi umuite fisadi babu?!! Kama manji fisadi na bakhresa fisadi pia
 
so wat? fisadi kupata umaarufu kupitia timu yangu ya yanga?

Hakuna mwana yanga mwenye akili chafu kama wewe,so just stay away pls,baki na simba yako na utuachie yanga yetu gosh!
 
anajisafishia ufisadi wake kupitia mgongo wa yanga, ninavyoipenda yanga, nikisikia jina la huyo mtu huwa nachefuka natamani hata kuhamia simba.

au uliwahi kumpa tigo alafu hela alizokulipa ukazipoteza bila kutmia hata jero?!!!
 
au uliwahi kumpa tigo alafu hela alizokulipa ukazipoteza bila kutmia hata jero?!!!
samahani manji kama nimekuudhi, punguza hasira, ulileta mada yako hapa ili upate publicity, mambo ya tigo yanaendana vipi na wewe kuchukua form....nani asiyejua hapa tz kama wewe ni fisadi papa mkubwa kabisa, unazipeleka pesa hizo za ufisadi yanga? huoni unaidhalilisha timu? sisi wanayanga inatuuma kuona wewe unajificha kwenye kichaka cha yanga, ingekuwa vizuri ukanyamaza kimya usilete hii mada...ukileta lazima tu tutakuchambua, hii ndo jamii forums...punguza hasira, ukubali ukweli utakusaidia...ok bwanamdogo? kama wewe unatoaga tigo usifikiri kila mtu huwa anatoa iyo tigo.....endelea kutoa tigo kama ndo tabia yako lakini pesa za walipa kodo wetu uziache...
 
siamini kama jamiin forums ni eneo zuri kwa mafisadi kujisafisha na kupata publicity, ukija hapa kama wewe ni fisadi utatolewa kama kunguru wa zenji.....kawaulize wenzio, au nyamaza kimya manake hapa wengine wakianza nao kukukurupua, utakimbia bila nguo mtaani wakushangae...
 
Hakuna mwana yanga mwenye akili chafu kama wewe,so just stay away pls,baki na simba yako na utuachie yanga yetu gosh!

achana nae, shoga huyo,amejiunga leo kutoka fbook!!
 
Hivi Rage sio fisadi Mkuu? Yanga daima mbele, nyuma mwiko....
ni wale wale tu mzee, hizi ndo timu zetu za kibongo, kimekuwa kichaka cha wahalifu ndo maana hata hatuendelei......tunapigwa mabao na matimu ya nchi zingine kila mwaka...kila kocha anayekuja kufundisha hapa anasema hatufundishiki, na akiondoka anaapa kutorudi tena tz....kamwuliza maximo.....aliumiza kichwa hapa akachanganyikiwa hadi akaingia kuigiza filamu za kibongo....wachezaji wetu wamemchanganya...
 
Back
Top Bottom