Yutong Vs scania Vs ud


Ally's zipo wapi siku hizi?
 

Mdau umenisikitisha na poor analysis yako !!! , inaonyesha kweli unafahamu mambo kadhaa katika mabasi , lakini hujui mengi sana ,kichwa kimeniuma zaidi ulipojipa signature ya "mechanical engineer" kama ni kweli ,basi Tanzania tuna tatizo kubwa sana la wataalam.

Huwezi kulinganisha yutong na scania kwa kutumia vigezo vya aerodynamics , yutong anatengeneza bus body na chassis, scania wao wanatengeneza engine na chassis, ie yutong hatenegenezi engine na scania hatengenezi body, ukitaka kulinganisha kwa usahihi chagua official body za scania ie irrizar ,marcopollo, busscar .
Suala la stability na dynamics za mabasi ni pana sana , ila nikupe dondoo tu , steel suspension ambazo asilimia kubwa ya basi za kichina wanatumia ikiwemo yutong , sio stable kama air suspension . Fahamu pia kila mtengenezaji ana style tofauti tofauti katika kulikabili suala la safety na comfort, mfano volvo , benz man, wao wanapotumia air suspension huwa wanaeka airbag nne kwa axle, scania pekee huwa anaweka airbag mbili kwa axle.

Back to topic lengo la mtoa mada ilikuwa ni kulinganisha uwezo wa yutong na scania ikiwa katika( local body manufactures), to th best of my knowledge , yutong kupambana na scania itategemea zaidi model ya scania inayoshindana nayo, 93 au 94 sawa , lakini kama ni 114 113 au 124 yutong haiwezi, kama mdau mmoja hapo juu alivyoizungumzia 114 330 hp ,ambayo mifano yake ni basi kama allys, leina ,abood etc hizi huwezi kulinganisha hata kidogo na yutong.

kwenye suala la kudumu hapo ndo scania ipo vizuri zaidi, nikupe mfano tu production ya mwisho ya series 3 scania (93 ,113 na 143 )ilikuwa mwaka 1994 , lakini mpaka leo bado ni tool inayoaminika. Mind you hapa nina linganisha yutong latest model vs twenty years old scania ambazo Tanzania tunatumia, R 340 scania bus bado hazijaingia barabara za kwetu , ila ni habari nyingine kabisa .
 

Nimependa uchambuzi wako , nasafiri sana nchi za kusini kwa bara bara ,nikitumia sana mabasi, trust me hakuna yutong inayotoka nje ya mipaka , suala kubwa hapa ni reliability, scania inaweza safari ndefu sana ila ni heavy kwenye mafuta hasa kama kuna milima na spidi ni kubwa , nissan matajiri wanazipenda kwa kuwa ni cheap kwenye kununua ,service na mafuta , ila ni slow movers kwenye milima.

Huwa na kuwa na amani sana ninapopanda scania hasa 114, najua nitawahi safari yangu na sitachoka sana.
 

kweli kabisa mkuu..mi nshalala njian mara mbili na scandinavia miaka iyo na iyo kiswele pia. Mzee msae mabasi hayo yalimpaga short sana aisee
 

Mkuu ni kweli ulichosema ila naomba nikurekebishe kidogo twende sawa... mosi katika scania namba ya mwisho huwa ni toleo ie series , namba zinazofatia ni ujazo wa engine in litres (cc) kwa maana hiyo 94 ni engine ya cc9000 (9litres ) toleo la nne, katika series one kulikuwa na option ya engine tau tu 81 ,111na 141 (v8) seies two kulikuwa na option nne 82 ,92 112, na142(v8) , series three zlikuwa option tatu 93 ,113 na 143(v8) series four kulikuwa na engine option tano 94 ,114, 124 ,144(v8),164(v8). Baada ya series four waliamua kubadilisha naming format kulingana na cabin types na uwezo wa engine (hp) that is P ,R, G,& T series kwa maana hiyo hakuna R524 bali ipo R500, R580 n.k hope nimesaidia..
 

Mi simo katika jambo hili: kuna ubishi kuwa bus likiwa 120km/h na RAV4 130km/h, ujue basi litakuacha wewe na RAV IV yako, je wadau munasemaje? Hoja hapa ni ile Revolution ya tairi kwa gari kubwa ikiwa 120km/h ni kubwa zaidi ya ile ya gari dogo. Lakini Physics inatumbia Speed ni umbali uliotumika kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa muda uliotumika. Hivyo kwa jibu hili la Fizikia Scania Bus 120km/h=RAV4 120km/h. Lakini siku moja jaribu kuweka 120km/h kwa gari lako dogo Alteza, halafu mwenzio wa Bus aweke kama hiyo pia, taraatiiibu utaona anakuacha!

Tukirudi kwenye topic; Scania ni bora kwa uimara kuliko Yutong.Lakini kwa Speed Yutong ni 140 na zingine 160km/h wakati Scania ni 120 km/h. Bei ya Scania bus jipya kwa sasa ni 450-500million pesa za Kitanzania, wakati yutong atleast kwa bei hiyo ya Scania unapata mbili hivi. Kwa Speed Yutong yuko juu, ila kwa Luxury body Scania( haya ya kisasa kama aliloweka mdau la picha nyekundu ni comfortable kuliko Yutong, hata nafasi ndani ya Scania la viti vya 2x2 ni kubwa, wakati Yutong nafas ni ndogo, viti ni vidogo kwa kufuata shape za Wachina, japo kwa kweli Yutong wanajitahidi. Mwanzoni walileta Yutong engine nyuma, zile zilishindwa mapema sana, kila siku linachemsha engine kwa kuwa nchi zetu hizi za joto engine inatakiwa ipoe sana, sasa ukiweka nyuma ni majanga. Wachina walipogundua hilo wameleta hizi za engine mbele. Naamin baadae watarekebisha mfumo wa diff ambao unaleta shida, Wachina ni wazuri kustudy soko, kila mapungufu huyastudy na kurekebisha
 
Weeeweweeee Scamia kupandisha mlima acha bwana, yaan ikikubali inapandisha kama inashusha waulize madereva wanayokanyaga utapata jibu abaake.
Scania zinakuwa nzito sana hasa kwenye kupandisha milima/milimani....lakini kwenye flat road...dah usipime!! Yutong ni laini mno na zinapepea kama karatasi, it is good by then!!
 

scania ziko vizuri zaidi na speed ni kubwa. mf. leina tours bus ni hatari inaenda kahama yutong haifuati


hii basi wanaiogopa. pia kuna bus inaitwa city boy nayo inaenda kahama ni hatari. mm nilisafiri na new force ni u tong mpya hawa jamaa wawil hapo juu waliitesa sana hii yutong. soscania na yutong ni vitu viwil tofauti na tofauti inaonekana yanapopanda mlima
 

Uko sahihi kwa asilimia 100.
 
kulinganisha Scania na Yutmg ni kuchekesha walionuna.
Matajiri wengi walionunua Yutonga wanajuta ni gari ambayo haiwezi kaa barabarani zaidi ya 2yrs , wanachofanya wanunua Yutong na wanaweka engine za Scania.
Na uimara wa body ya U tong haifikii hata nusu yd uimara wa body ya marcopolo ambazo zinatumika kwenye magari ya Scania.
Matajiri walimbilia kwenye U tong sababu ya bei .
 
Scania ni moto wa kuotea mbali esp scania kuanzia 94,114 na 124..uliza abiria wa kahama na mwanza watakuambia leina tours ni bus au jet…
 
Yutong baada ya miezi sita unaanza kuunganga undugu na mafundi
 

Mkuu yutong za sasa nitofauti na za kipindi cha nyuma mchina anatengeneza vitu vyote isipokua engine na mfumo wote wa breki engine inatengenezwa na mmarekani na mfumo mzima wa breki ni mjerumani kwa kiasi fulani wameboresha product ya sasa na za nyuma kunautofauti mkubwa
 
Hebu toka tunduma mpaka Dsm mzee wanjia ni scania Abood T 530 AZE. wazee wa IT wanaijua. Nenda Mbeya Arusha mzee wa njia ni Hood. Toka Harare Zimbabwe to Dsm hapo unamkuta Taqwa na falcon. ukipeleka youtong njia hizi uone kama itadumu. Kwa njia ya Dsm mbeya namba moja unamkuta Happy Nation sauti ya manka hiyo ina uwezo wa kuingia Dsm saa kumi toka mby. pia kumbukeni speed ya youtong mwisho ni 120 tu.


selfish
 
Falcon na spider mwanzoni njia ya mwanza dar via nairob ilikua ni nissan diesel,tambarare zinatembea lakini zinasinzia sana kwenye kipando,vipi hizi?
 
Haya wakuu,hembu tuambiane sasa mabasi yaendayo kasi Dar yatakuwaje.
Na aina gani ni nzuri na bei zake zipoje
 
hapa kuna kitu sijaelewa hasa kuhusu speed mana kuna wengne wanasema yutong ina 120km/hr mara wengne zaid mara wengne wanadai scaniad ndo 120km/hr so nashindwa kuelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…