Za kuambiwa, tuchanganye na zetu

Za kuambiwa, tuchanganye na zetu

Ahabu - mke 1

Herode - mke 1

Anania - mke 1

Pontio Pilato - mke 1

Yeroboamu - mke 1

Nebukadreza. - mke 1

Hamani - mke 1​

Na wote walipotea njia na kumsaliti Mungu.

1. Ibrahimu - wake 2

2. Yakobo - wake 4

3. Daudi - wake 4

4. Sulemani - wake 700

5. Rehoboamu - wake 18

6. Abiya - wake 14

7. Elikana - wake 2

8. Lameki - wake 2​

Na wote wakapata kibali machoni pa Bwana.

Lakini wachungaji wanatuambia kuwa kuoa wake wawili ni dhambi kwa Mungu.

Something somewhere is not right.
Unataka kuhalalisha uhuni wako.
 
Hii sio amri ya Mungu bali ni ushauri wa mtume Paulo.Mtu anahukumiwa kwa kuvunja amri za Mungu na sio kwa kutofuata ushauri wa mitume na manabii.
Kwenye 1Wakorintho 7:1 mtume Paulo anashauri ni bora watu wasioe au kuolewa, lakini leo wakristo wanaoa na kuolewa kwasababu wanajua kilichoandikwa kwenye hiyo aya sio amri ya Mungu bali ni ushauri wa Paulo.
Hakuna sehemu yoyote kwenye Bible ampapo Mungu amekataza ndoa ya wake wengi.
ni kweli kabisa hujakosea hapa ktk wakorintho paulo anashauri kwa habari ya ndoa kama Yesu pia alivyoshauri kwa habari ya ndoa ktk mathayo..

hebu tusome mathayo 19:3-12
Mathayo 19:3-11
[3]Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu?
[4]Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,
[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
[6]Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
[7]Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
[8]Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.
[9]Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.
[10]Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.
[11]Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.
[12]Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee.
 
Cite a biblical verse please.
mathayo 19:4-6
[4]Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,
[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
[6]Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
 
mathayo 19:4-6
[4]Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,
[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
[6]Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
Mkuu genius, kuoa mke wa pili au zaidi haibadilishi agano la kuwa mke na mme watakuwa mwili mmoja.1wakorintho 6:16 inaeleza kuwa mtu akilala na kahaba wanakuwa mwili mmoja,kwahiyo nikilala na makahaba 10 ninakuwa mwili mmoja na hao makahaba.Kahaba mmoja akilala na wanaume 10 anakuwa mwili mmoja na hao wanaume.
Kwa msingi huo naweza kuwa na wake wawili au zaidi na bado nikawa mwili mmoja na wao japo kwa maagano separate,kama ambavyo mfanyabiashara anaweza kuwa na partners 5 kwenye biashara moja kwa makubaliano tofauti.
Tuendelee kujifunza.
 
Back
Top Bottom