Zacharia Isaay (Mbunge Mbulu): Serikali iache kigugumizi ieleze wazi kuhusu ugonjwa wa kupumua unaomaliza watu wa Mbulu

Zacharia Isaay (Mbunge Mbulu): Serikali iache kigugumizi ieleze wazi kuhusu ugonjwa wa kupumua unaomaliza watu wa Mbulu

Siku zote yanapo mkuta mfalume huwa anasema kuwa naitisha wazee wa Baraza kwahiyo tusubirie tena !!!!
 
Mh Mbunge Mungu akubariki sana.Rais Magufuri atambue hata akiwaondoa wapinzani Bungeni, atapata upinzani tu hata ndani ya chama chake watu wasiporidhishwa na mambo.
Ninapomwona Rais Magufuli ni mtu wa ajabu ni pale ambapo hajali uhai wa watu. Mtu wa namna hiyo ni wa ajabu sana.

Mtu mwenye Roho ya ubinadamu, hata usipokuwa na jawabu la ugonjwa, ukiona wenzako wanaangamia, angalao utawaambia wanaokuzunguka kuwa mwenzenu kuna ndugu zangu wanaumwa au wanafariki. Haiwezekana watu wako wanaugua wanakufa, halafu kwa majirani unawaambia, nyumbani kwangu ni salama kabisa.

Ndiyo maana namwona Magufuli kama mtu ambaye hajabeba roho ya ubinadamu. Nadhani ana kitu tofauti na roho ambayo binadamu huwa nayo.
 
Mh Mbunge Mungu akubariki sana.Rais Magufuri atambue hata akiwaondoa wapinzani Bungeni, atapata upinzani tu hata ndani ya chama chake watu wasiporidhishwa na mambo.
Upinzani upo mioyoni mwa watu. Huyu amejitoa mhanga kusema ukweli.
 
😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀mbavu zaaaaangu jamani.
Kumbe nchi inaongozwa na mnyama ati ee🙄🙄🙄🙄😀😃😄😀😂🤣😂🤣
 
Mbunge wa Mbulu Mjini (CCM), Zacharia Isaay ametaka Serikali ya Tanzania kueleza wazi kuhusu alichokiita ugonjwa wa kupumua ambao anasema unamaliza watu wa Mbulu.

Isaay amezungumza kwa hisia kali bungeni leo Alhamisi Februari 11,2021 akisema hawezi kuzungumzia mpango badala yake anaona bora azungumzie hali ya wananchi wake ambao kila mara anakwenda kuzika.

"Serikali iache kigugumizi jimboni kwangu watu wanakwisha Spika,nimechoka kuzika hata leo wanazika mtoto wa diwani wakati mwingine nashindwa kukuaga Spika kwenda Mbulu naamua kutoroka,"amesema Isaay.

Mbunge huyo anasema wanaopoteza maisha jimboni kwake magonjwa yao yanafanana ambayo ni tatizo la kupumua akihofia kuwa msimu wa baridi jimboni kwake utaendelea kuwaumiza.

"Jana nilikwenda hospitali ya hapa Benjamin Mkapa (Dodoma) kwa ajili ya kufanya vipimo lakini wakaniambia mitungi ya gesi imejaa,watu ni wengi sasa nimesema kama watu watanichukia basi lakini nimesema," amesema Isaay.

Mbunge huyo ameomba Serikali kuangalia namna ya kuboresha dawa za miti shamba ambazo ameeleza kuwa zinasaidia kwa kiasi kikubwa lakini akabainisha kuwa zinapatikana kwa gharama kubwa.

-----
Maoni Yangu
Tukipata wabunge watano jasiri kama huyu, Tanzania tutapona.

Juxi katibu mkuu Afya kasema ametembelea hosipitali zote hali ni nzuri. Hebu ona mbunge kaenda hosipitali anasema hali ni mbaya.
Hawa wataalam wana takiwa kunyongwa.
Kweli kama kiongozi anasimama hadharani anasema watu wasivae barakoa na anasema sio lazima kuchukua hatua kutekeleza social distancing ni mbaya sana.
 
Ninapomwona Rais Magufuli ni mtu wa ajabu ni pale ambapo hajali uhai wa watu. Mtu wa namna hiyo ni wa ajabu sana.

Mtu mwenye Roho ya ubinadamu, hata usipokuwa na jawabu la ugonjwa, ukiona wenzako wanaangamia, angalao utawaambia wanaokuzunguka kuwa mwenzenu kuna ndugu zangu wanaumwa au wanafariki. Haiwezekana watu wako wanaugua wanakufa, halafu kwa majirani unawaambia, nyumbani kwangu ni salama kabisa.

Ndiyo maana namwona Magufuli kama mtu ambaye hajabeba roho ya ubinadamu. Nadhani ana kitu tofauti na roho ambayo binadamu huwa nayo.
Roho ya mnyama isiyo na utashi wa kibinadamu
 
Mtaalam katembelea hospitali zote ila Mbunge katembelea hospitali moja lkn wewe unamuamini Mbunge kuliko Mtaalamu maana unachopenda kukisikia kikufurahishe ni hicho cha Mbunge
Mtu aliyeokotwa jalalani unadhani akili zake zikoje.
Mbunge hajaokotwa alichaguliwa na watu timamu
 
Now you can see how naive and stupid most people are. Na watu watakwisha kwelikweli maana kama tunasubiri matamko, tutasubiri sana

Tamko la Chief Medical officer ni kwamba mnapaswa kuanza desturi ya kunawa mikono na kufanya usafi kwa ujumla ili msipate kipindupindu na Typhoid🙂
Rudi majalalani hakukufai huku ni kwa ma great thinkers
 
Rudi majalalani hakukufai huku ni kwa ma great thinkers
But you are not among those GTs. Wewe kaa ukisubiri tamko la kuvaa barakoa au kunawa kwa sabuni ili corona isikupate

GTs are always proactive and not reactive.
 
Kusema kitu ambacho kiko wazi ni ujasiri? Mbona tunashusha viwango wa mtu kuitwa jasiri namna hii? Tanzania watu wanatetekea kwa corona. Mtu akisema watu wanakufa kwa corona (jambo ambalo ni kweli ) ni ujasiri? Tena basi ameogopa hata kuutaja ugonjwa! Tuache woga ndugu zangu.
Namuita Jasiri. Kama angetaja corona mwanzo wa mchango wake washenzi wange kata mawasiliano. Kama umebahatika kusikiliza clip yake alipo taja neno corona walikata mawasiliano na kumuambia muda umekwisha. Sifa ya mtu apewe. Nani mwingine kwenye hicho kikao cha Ccm hapo Dodoma amethubutu kuongea???
 
Namuita Jasiri. Kama angetaja corona mwanzo wa mchango wake washenzi wange kata mawasiliano. Kama umebahatika kusikiliza clip yake alipo taja neno corona walikata mawasiliano na kumuambia muda umekwisha. Sifa ya mtu apewe. Nani mwingine kwenye hicho kikao cha Ccm hapo Dodoma amethubutu kuongea???
Awe ametaja neno corona au hajataja, hoja yangu ni kuwa watu wamekuwa na woga wa kijinga mpaka kufikia hatua ya kuogopa kutaja mambo yaliyopo. Kwangu mimi huyo siyo jasiri bali ametimiza wajibu wake. Hata kama wengine wameogopa lakini hakumfanyi awe jasiri.
 
Mbunge wa Mbulu anasema jimboi kwake amefriki watu wengi wenye waliokuwa na dalili za Corona kiasi kwamba kwa sasa amekuwa akipokea taarifa za misiba na kuzipotezea

Ameendelea kusema pia Serikali imeshauri watu kutumia dawa za miti shamba lakini watu wamkuwa wakinywa tu kama gongo sababu hakuna muongozo maalumu

Pia amesema ametembelea Hospitali ya BW Mkapa na kuambiwa mitungi yote ya Oksijeni imeisha na kutahadharisha kuwa watashindwa hata kuwalinda wataalamu wa afya na kumba Serikali kuongeza miungi hiyo.

 
Hongera kwa mh.Mbunge.Unaweza kufanya watu kuonekana wajinga kwa kipindi fulani lakini si wakati wote. Pia wapo wabunge wengi hawakuhitaji mabegi na walichukizwa sana kuonekakana wamebebwa na kishindo , ipo siku wataweka wazi.
 
Mbunge wa Mbulu anasema jimboi kwake amefriki watu wengi wenye waliokuwa na dalili za Corona kiasi kwamba kwa sasa amekuwa akipokea taarifa za misiba na kuzipotezea

Ameendelea kusema pia Serikali imeshauri watu kutumia dawa za miti shamba lakini watu wamkuwa wakinywa tu kama gongo sababu hakuna muongozo maalumu

Pia amesema ametembelea Hospitali ya BW Mkapa na kuambiwa mitungi yote ya Oksijeni imeisha na kutahadharisha kuwa watashindwa hata kuwalinda wataalamu wa afya na kumba Serikali kuongeza miungi hiyo.


Upinzani wa kweli umeanza
 
Back
Top Bottom