DOKEZO Zahanati ya Mtamaa (Singida) isaidiwe, Watumishi ni wachache, mazingira ni mabovu hasa kwa Wanaoenda kujifungua

DOKEZO Zahanati ya Mtamaa (Singida) isaidiwe, Watumishi ni wachache, mazingira ni mabovu hasa kwa Wanaoenda kujifungua

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Mliogwa

Member
Joined
Jun 6, 2024
Posts
37
Reaction score
37
WhatsApp Image 2024-12-16 at 07.49.24_0f6decb1.jpg

WhatsApp Image 2024-12-15 at 17.05.30_257a75a4.jpg

WhatsApp Image 2024-12-15 at 17.05.11_a70ac291.jpg
Eneo la Mtamaa lililopo Kilomita 20 kutoka Manispaa ya Singida kuna zahanati ambayo inahudumia wakazi wa eneo hilo ambayo inatambulika kwa jina la Zahanati ya Mtamaa.

Nimefanikiwa kufika mara kadhaa katika Zahanati hiyo na kugundua mambo ambayo ni vizuri nikishea na Wana JF inaweza kuwa na faida kwa Jamii kwa maana ya mamlaka husika kuchukua hatua ili kusaidia wanaopata huduma n ahata wanaotoa huduma hapo:-

Zahanati hiyo ina Daktari mmoja, Muuguzi mmoja na Daktari wa Maabara mmoja inafanya kazi siku na saa za kazi tu.

Mnamo Desemba 9, 2024 nilifika eneo hilo na kukuta kina mama wakisubiri huduma ya Kliniki ya Watoto, pia kulikuwa na Mzee mmoja ambaye alikuwa na jeraha usoni.

Siku hiyo hakukuwa na huduma kwa vile ilikuwa Sikukuu, alipigiwa simu Muuguzi hakupokea, baada ya saa kadhaa akaja Daktari wa Maabara akawakuta wahitaji hao ambao walipouliza kama wanaweza kupata msaada akasema kuwa siku hiyo ni mapumziko huduma hadi kesho yake.

Desemba 14, 2024 nilirudi kwa mara nyingine katika Zahanati hiyo na kukuta mama mjamzito akiwa chumba cha Leba anasubiri kujifungua.

Daktari aliyekuwepo alimuona Mwanamke huyo baadaye akaaga kuwa anaelekea Mnadani, nilifanikiwa kuingia humo ndani na kuzungumza na Mwanamke huyo.

MAZINGIRA
Pamoja na kwamba Zahanati hii imejengwa kwa takriban miaka 20 iliyopita, mazingira ya sasa ni duni mnoo.

Kuna uchakavu wa vifaa tiba vingi ikiwemo mpira wanaolalia Wajawazito wakienda Kliniki.

Mazingira ya chumba cha kujifungulia yanahuzunisha sana, kitanda kimoja tu, endapo kuna wamama zaidi ya mmoja wanatakiwa kujifungua kwa wakati mmoja wanafanyaje?


Sehemu ya kujifungulia iko wazi sana ni rahisi sana mtu wa nje kufuatilia linaloendelea ndani, pazia iliyopo imechanika n ahata watu wanapokuwa ndani ya Chumba cha Leba mazungumzo yao yote yanaweza kusikika kwa wale waliopo nje.

Mfano kuna muda nikiwa nje ya chumba hicho, mwanamke aliyekuwa anasubiri kujifungua alikuwa akigugumia maumivu nilimsikia na nilihisi anahitaji msaada, nikamsikia anatapika nikaingia kumsaidia huku nikimwita ndugu yake aje kumpa msaada wa karibu.

WAHUDUMU
Zahanati hii ina wahudumu wachache, kwa mfano mama mjamzito niliyemkuta Desemba 14, 2024 alikuwa akihudumiwa na Daktari huku nesi hakuwepo.

Mbali na kutoa huduma hiyo, Daktari pia alikuwa na mishe zake, hivyo hakuweza kukaa hapo muda wote kusubiria hadi mama huyo ajifungue, alimuacha na yeye akaendelea na mambo yake kwa maelezo kuwa atarudi kumuona baadaye. Sasa je akipata dharura atasaidikaje?

Tutawezaje kumaliza hatari ya kupoteza mama na mtoto ikiwa mama hapati uangalizi wa kutosha akiwa anasubiri kujifungua?

Barabara yenyewe kufika eneo hilo la Zahanati ni changamoto, usafiri wa uhakika uliopo ni bodaboda tu.

HITIMISHO
Tunajua Serikali ina macho ya kufuatilia na masikio ya kusikia yote yanayoendelea nchini. Naomba watupe jicho lao kwenye Zahanati hii kwa kuisadia kuongeza wahudumu wa afya, vifaa tiba na majengo mengine kwa manufaa ya Wananchi wake wa Mtamaa.
WhatsApp Image 2024-12-15 at 17.05.05_b2dfd68f.jpg

WhatsApp Image 2024-12-15 at 17.05.10_43ec646f.jpg

WhatsApp Image 2024-12-15 at 17.05.11_973bcc4e.jpg

WhatsApp Image 2024-12-15 at 17.06.24_5922dd75.jpg
 

Attachments

  • 20241214_120915.mp4
    46.1 MB
Umeleta taarifa iliyopangwa na ikapangika vizuri pamoja na picha.
Nakuombea usalama huko uliko.
 
Wewe ni muandishi wa habari chanzo gani? Nani aliyekupa ruhusa ya kuingia chumba cha kujifungulia?Je wewe ni me au ke? Huko hakuna uongozi je ulienda kwenye uongozi hawakukupa ushirikiano?Je wewe ni muasisi wa chama gani cha siasa?Kwanini ulitembelea zahanati ya tamaa?Ulipojibiwa leo sio siku ya kazi ulichukua hatua gani?Je hatua uliochukua ipo kisheria?Ulipo muona muhudumu anamuacha mama mjamzito ulichukua hatua gani?Je hatua hiyo ipo kisheria? Je unaweza kutaja ni maeneo gani yameruhusiwa kupiga picha na ambayo hayajaruhusiwa kupiga picha?Je unajua maana ya uhuru bila mipaka maana yake? Majibu tafadhali..ahasante kwa taarifa mimi mpita njia tu.
 
Wewe ni muandishi wa habari chanzo gani? Nani aliyekupa ruhusa ya kuingia chumba cha kujifungulia?Je wewe ni me au ke? Huko hakuna uongozi je ulienda kwenye uongozi hawakukupa ushirikiano?Je wewe ni muasisi wa chama gani cha siasa?Kwanini ulitembelea zahanati ya tamaa?Ulipojibiwa leo sio siku ya kazi ulichukua hatua gani?Je hatua uliochukua ipo kisheria?Ulipo muona muhudumu anamuacha mama mjamzito ulichukua hatua gani?Je hatua hiyo ipo kisheria? Je unaweza kutaja ni maeneo gani yameruhusiwa kupiga picha na ambayo hayajaruhusiwa kupiga picha?Je unajua maana ya uhuru bila mipaka maana yake? Majibu tafadhali..ahasante kwa taarifa mimi mpita njia tu.
Ama kweli MONEY IS NOT EVERYTHING sometimes we just need brain.
 
Mheshimiwa wa Trap na Trab na wawakilishi wote Singida wanasemaje?
 
Wewe ni muandishi wa habari chanzo gani? Nani aliyekupa ruhusa ya kuingia chumba cha kujifungulia?Je wewe ni me au ke? Huko hakuna uongozi je ulienda kwenye uongozi hawakukupa ushirikiano?Je wewe ni muasisi wa chama gani cha siasa?Kwanini ulitembelea zahanati ya tamaa?Ulipojibiwa leo sio siku ya kazi ulichukua hatua gani?Je hatua uliochukua ipo kisheria?Ulipo muona muhudumu anamuacha mama mjamzito ulichukua hatua gani?Je hatua hiyo ipo kisheria? Je unaweza kutaja ni maeneo gani yameruhusiwa kupiga picha na ambayo hayajaruhusiwa kupiga picha?Je unajua maana ya uhuru bila mipaka maana yake? Majibu tafadhali..ahasante kwa taarifa mimi mpita njia tu.
Hovyo kabisa. Hayo maswali kamuulize mkeo.
 
Back
Top Bottom