ZAIDI: Tribute Kwa Kina Mama Wote. Tafadhali Pitia Na Mnipe Maoni Yenu

ZAIDI: Tribute Kwa Kina Mama Wote. Tafadhali Pitia Na Mnipe Maoni Yenu

Trophic

Member
Joined
Jun 8, 2020
Posts
11
Reaction score
8


Hello JamiiForums,

Hii itakua thread yangu ya pili humu Jukwaani toka nijiunge kama member June, 2020. Mimi ni Producer, Composer & Songwriter. Ndani ya miaka mitatu nimekua nikijaribu kuendeleza craft yangu kiujumla na ningependa muweze kuipitia na kunipea genuine feedback, your support and maybe be fans. Sijawahi sikia nyimbo iliyotembea kisa JF, sio mbaya hii ikiwa ya kwanza 🤞🏾

Anyways, nyimbo yenyewe ni Zaidi/Mama na ni tribute kwa kina mama wote, especially mama angu mzazi. Kikwetu kwetu, ni ngumu/nadra sana kwa watoto wakiume kuwaambia wazazi wao wanavyowapenda, sikuwahi kumtamkia mama angu neno hilo na mwaka jana, 2022 nlimpoteza ikawa one of my biggest regrets. Mziki ni namna yangu ya kudeal na stress, depression and the likes. Hivyo, in her honor, na kwa kina mama wote, nimeandika huu wimbo.

P.S. Kama mama ako uko nae bado, nadhani ni vyema kumwambia ni namna gani una mu appreciate, when you still have the time.

 
ZAIDI (MAMA) LYRICS

[Verse]
Mama, najivunia kila sekunde ilopita nikiwa na we,
Uwepo wako maishani ni sababu nisipotee,
Nlikua kadogo nimekua umekuza asante!
Nakuimbea kwa mola daima we akukumbuke—

Maana, sijui ingekuaje mimi nisingezaliwa nawe,
Au ingekuwaje ungeondoka unitupe,
Sidhani kama ntaweza nkisema nikulipe,
Niwazavyo shukuru haitoshi—

[Pre Chorus]
Maana hata nikisema, niimbe, hizi mambo mama,
Bado nashindwa, maana, maneno hakuna—
Ila nataka, ujue, unapendwa sana,
Na ni ZAIDI, ya vyote, chini ya jua!

[Chorus]
Niki... Ni...Hizo mambo mama,
Bado na...Maneno hakuna—
Ila nataka...Unapendwa sana,
Na ni ZAIDI, ya vyote, chini ya jua!

[Verse 2]
Mama, nilivyo hivi leo ni malezi yako we,
Mazuri mabaya yamepita me nibaki eeh!
Salama yangu nimeipata kwako we,
Nakuombea kwa mola daima akukumbuke we!

Tena, nlipokua vibaya uliniweka sawa,
Kwenye upendo wako Mungu nimemuona,
Sidhani kama ntaweza nkisema nikulipe,
Niwazavyo shukuru haitoshi—
 
Cover Art​
PicsArt_01-08-05.27.23.jpg
 
Back
Top Bottom