Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,984
Chama Cha Mapinduzi Kwa miaka zaidi ya mitatu walifunga milango ya fahamu waliyopaswa kutumia kuwasiliana na Mwenyenzi Mungu kumwombea hekima wakamruhusu shetani atumie ndimi zao kupandikiza chuki baina ya wanaomwamini Mungu na wanaoamini madaraka. Viongozi kadhaa wakiwemo UVCCM walitoka adharani kusema Tundu Lisu ni Msaliti na afutwe Ubunge, asipewe fedha zake na Wala asihudumiwe Kwa chochote. Kwa tafsiri nyingine walitamani asiwepo Duniani wakiunga mkono risasi alizopigwa.
Leo Mhe. Rais ameonyesha Kwa mara ya pili Kwamba anamcha Mungu. Ameonyesha Kwa mara ya pila kwani mara ya kwanza alikwenda Nairobi. Ni Marais wachache wanaoweza kukutana na wapinzani wao nje ya nchi, ni Marais wachache wanaoweza kuacha madaraka na ushauri wa wanaomzunguka wakafanya maamuzi ya Kiraisi Kwa maslahi mapana bila kujali washauri wake watamfanya au watamsema vipi. Ashukuriwe huyo aliyepaza sauti kwa Mungu akaufanya moyo wa mama usiwe mgumu.
Jambo la pili, Nadhani vijana wanapaswa kujifunza kunyamaza Kwenye baadhi ya mambo? Wapo watu kama kibajaji unaona namna wanavyoweza kuwa katili, Wapo wakina Makonda na Sabaya, Yupo Mnyeti na akina Muro, Yupo DC wa Ubungo pamoja na akina Kakurwa. Hii ni sample ya below 55 yrs ambayo ilionyesha wazi Kuishi Kwa Lisu siyo hitajio lao ila Mungu alifanya tofauti.
Hapo ujazungumzia wenye Dola, lakini tujiulize huyu Mama anavyofanya upatanisho,ambavyo atumii wasiojulikana Kuna maendeleo yamekwama? Kwamba Ili tuendelee lazima Taifa liwe na wasiojulikana?
Nirudi Kwa Mhe. Mbowe, niwaulize watu walewale Bado wanaamini Mbowe ni Gaidi? Kama ambavyo Mhe. Rais asingeweza kukutana na Msaliti ndivyo atakavyokwenda kudhiitisha Kwamba Mbowe siyo Gaidi. Hatuwezi tukaendelea Kwa kufanya ukatili,taifa linaendelea kwa maridhiano.
Mwisho, Mhe Zito anasafari ndefu Kwenye siasa ila tu kufika kwake kutategemeana na atakavyoweza kuamua kuwa mwanasiasa Bora awe na madaraka au asiwe na madaraka. Zitto apaswi kushirikiana na watesi wa wenzake bila mkataba unaoeleweka. Lisu kasaini mikataba mitatu Leo Kwa wale tunaojua siasa. 1. Kwanza kapata fursa ya kuruhusu wale wote waliokuwa wamechukia mfumo waanze kuungana naye kusamehe.
2. Ameruhusu Mwenyekiti atoke bila masharti tofauti na Zito alivyopanga kufanya
3. Amesaini Mkataba wa vyama vya siasa kuanza upya siasa.
Kwa misimamo hii dhidi ya watawala ipo siku tutapata katiba Mpya.
Leo Mhe. Rais ameonyesha Kwa mara ya pili Kwamba anamcha Mungu. Ameonyesha Kwa mara ya pila kwani mara ya kwanza alikwenda Nairobi. Ni Marais wachache wanaoweza kukutana na wapinzani wao nje ya nchi, ni Marais wachache wanaoweza kuacha madaraka na ushauri wa wanaomzunguka wakafanya maamuzi ya Kiraisi Kwa maslahi mapana bila kujali washauri wake watamfanya au watamsema vipi. Ashukuriwe huyo aliyepaza sauti kwa Mungu akaufanya moyo wa mama usiwe mgumu.
Jambo la pili, Nadhani vijana wanapaswa kujifunza kunyamaza Kwenye baadhi ya mambo? Wapo watu kama kibajaji unaona namna wanavyoweza kuwa katili, Wapo wakina Makonda na Sabaya, Yupo Mnyeti na akina Muro, Yupo DC wa Ubungo pamoja na akina Kakurwa. Hii ni sample ya below 55 yrs ambayo ilionyesha wazi Kuishi Kwa Lisu siyo hitajio lao ila Mungu alifanya tofauti.
Hapo ujazungumzia wenye Dola, lakini tujiulize huyu Mama anavyofanya upatanisho,ambavyo atumii wasiojulikana Kuna maendeleo yamekwama? Kwamba Ili tuendelee lazima Taifa liwe na wasiojulikana?
Nirudi Kwa Mhe. Mbowe, niwaulize watu walewale Bado wanaamini Mbowe ni Gaidi? Kama ambavyo Mhe. Rais asingeweza kukutana na Msaliti ndivyo atakavyokwenda kudhiitisha Kwamba Mbowe siyo Gaidi. Hatuwezi tukaendelea Kwa kufanya ukatili,taifa linaendelea kwa maridhiano.
Mwisho, Mhe Zito anasafari ndefu Kwenye siasa ila tu kufika kwake kutategemeana na atakavyoweza kuamua kuwa mwanasiasa Bora awe na madaraka au asiwe na madaraka. Zitto apaswi kushirikiana na watesi wa wenzake bila mkataba unaoeleweka. Lisu kasaini mikataba mitatu Leo Kwa wale tunaojua siasa. 1. Kwanza kapata fursa ya kuruhusu wale wote waliokuwa wamechukia mfumo waanze kuungana naye kusamehe.
2. Ameruhusu Mwenyekiti atoke bila masharti tofauti na Zito alivyopanga kufanya
3. Amesaini Mkataba wa vyama vya siasa kuanza upya siasa.
Kwa misimamo hii dhidi ya watawala ipo siku tutapata katiba Mpya.