Zama hizi za Internet, serikali kuminya uhuru wa taarifa ni kujidanganya

Zama hizi za Internet, serikali kuminya uhuru wa taarifa ni kujidanganya

Huko youtube na facebook wamejaza jeshi la mtandaoni la vijana la kutukana na kukejeli wapinzani huku wakisifu sana ishu za Magufuli na serikali. Lengo ni kushape public opinion.

Hata hivyo waliowengi wenye kuipinga serikali hawathubutu kucomment huko kwa sababu ID zinakuwa wazi, watu wanaogopa usalama wao!
Wameshindwa nini kuwajaza na hapa jf?
 
Kwa mujibu wa Taarifa za TCRA ambazo zimenukuliwa katika mtandao maarufu wa Wikipaedia, idadi ya Watanzania wenye kumiliki vyombo vya mawasilaino kwa maana ya Simu ni milioni 43.5 kati ya wananchi milioni 53.8

Hii inamaanisha kuwa takriban asilimia 80.8 ya wananchi wanaweza kupashana habari na kuwasiliana kupitia simu.
Wakati huo huo Wananchi wenye kuaccess Internet ni milion 22.3 sawa na asilimia 41.4 ya wananchi wote

Kwa hiyo hii inamaanisha kuwa wananchi wanao uwezo wa kupata taarifa za ndani ya nchi na nje ya nchi kupitia mtandao hata kama serikali inabana magazeti na television

Hii inakuonyesha kwa nini Rais Magufuli amewahi kutoa kauli ya kutamani malaika washuke wafungie mitandao. Hata hivyo pamoja na kuleta sheria za mitandao na kujaribu kabana content zitolewazo mitandaoni bado wananchi wanaweza kupata access ya taarifa mbadala

Kwa hiyo CCM na serikali yake wasijidanganye kuwa wanaweza kubana Taarifa au kueneza propaganda kiasi kwamba wakaweza kuwadanaganya watanzania muda wote

Cha msingi ni kwamba Wapinzani waandae strategy na wawekeze katika internet na mitandao ya kijamii, itawasaidia sana kufikisha ajenda zao kwa umma

Kwa taarifa zaidi juu ya hali ya matumizi ya Internet nchini unaweza kuipata hapa:

List of mobile network operators in Tanzania - Wikipedia.

Tanzania internet users hit 23 million; 82 percent go online via phones: regulator
Inasemekana Lissu ataruhusu tena kupata watanzania kupata habari kwa wakati iwapo atashinda
 
Umeongea vyema. Lakini swali langu, kwanini kila siku mnayalilia magazeti, redio na televisheni hazitangazi habari zenu?


TUKUTANE OKTOBA 28!
Una taarifa kwamba,huko Namtumbo mkoani Ruvuma vijana wa CDM walitaka kumkafini ndugu yenu aliyempora mgombea wa CDM fomu za udiwani akiwa ametumwa na mwenyekiti wenu wa UVCCM???

Bado kidogo mtaanza kutuelewa
 
Wameshindwa nini kuwajaza na hapa jf?
Hapa JF wanakutana na watu wenye hidden ID's wanawajibu bila kuhofia kupotezwa ndiyo maana kila wakijaribu hapa JF wanafeli.
Kule kwingine watu wanawaacha tu maana wanahofia usalama wao kutokana na IDs zao kuwa wazi
 
Internet nayo itafungwa mpaka baaada ya uchaguzi
Then wataendeshaje shughuli za serikali ikiwemo makusanyo ya mapato mfano control number,
Mzungu ana akili Sana kuleta control namba afrika
 
Hakuna chama cha upinzani ambacho kimejiandaa kuunda serikali coz kushinda uchaguzi vyama vya upinzani hasa kwa nchi za Africa ni mchakato mrefu na mipango ya muda mrefu kitu ambacho hakuna chama cha upinzani Tanzania wameshafanya hata robo nadhani wao wanagombania kuwa ni chama gani kitakuwa chama kikuu cha upinzani

"Wananchi wenye kuaccess Internet ni milion 22.3 sawa na asilimia 41.4 ya wananchi wote " Hahahaaaa ulishajiuliza Tanzania ni mambo gani au vitu gani vinafatiliwa au kugoogle sana kwenye Internet utashangaa sana nikwambie kitu watanzania hawafatilii siasa kwenye mitandao ni asilimia chache sana hata ukifanya utafiti utagundua ni Twitter tu ndo wanafatilia siasa but sehemu au mitandao mingine nadhani unajua nn kinafatiliwa sasa jiulize Twitter ni watanzania wangapi wana account huko??

Tanzania bado main stream media(TV,Magazeti,Radio) bado zinanguvu sana na bado zinafatiliwa na watu wengi kwa sababu kupata taarifa huko ni free au cheap kulinganisha na mitandaoni ambapo lazima uwe na bando kitu ambacho mtu wa mikoani hawezi kununua GB 4 eti kumuangalia Tundu Lissu akiutubia You tube nazungumzia nchi kwa ujumla si mijini tu CCM si wajinga kuwabana huko wanajua nini wanafanya hapa ungewashauri wafungue vyombo vyao vya habari kama Radio na TV ambazo watakuwa na mamlaka navyo hata kwa wenzetu ambapo Dunia imeamka bado TV ,Magazeti na Radio zina nafasi kubwa sana ktk Ulingo wa kupashana habari pia kwa mfumo uliopo ni mpumbavu pekee anayeweza kusema Lissu au upinzani utachukua nchi ktk miaka hiii 10 au 15 ijayo bado sana .
Tv- ni kuona na kusikia
Radio- ni kusikia zaidi
Mitandao ya kijamii - utafute habari uisome

Sasa utaona huku kwetu tv na radio vinagusa watu wote.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuja wanaukimbiza upepo, niwashauri upinzani waongee na tv binafsi za Kenya wanunue airtime ziwarushie matangazo yao live stream au recorded mfano citizen hizi zipo kwenye decoder zote hii itasaidia watz wengi kupata taarifa za mikutano yao pasipo haja ya citizen kulazimika kuja nchini kuripoti.
Hawa wakuja wenye mawazo ya kijima watatushinda vipi akili, hawana uwezo wa kuzibiti habari zisisambae, yaani wadhibiti Bluetooth, flash, cd na nk. Wao wabakie na media zao sie twende na za nje
 
Mojawapo ya sifa za utawala usiokubalika na wengi (dikteta) ni kuminya vyombo vya habari.

Kwa hofu waliyo nayo CCM na Magufuli wao, sitashangaa wakiamrisha internet izimwe nchi nzima!

Siku ya kufa nyani miti yote huteleza...
Haisaidii kitu tutatumia Bluetooth,flash,cd, VPN,pia hicho kitu cha kuzima internet hawawezi means watakusanyaje mapato kupitia control number, hawawezi media control Hawa wakuja.
Wanavuna walichopanda anga limeshawakataa
 
Tanzania bado main stream media(TV,Magazeti,Radio) bado zinanguvu sana na bado zinafatiliwa na watu wengi kwa sababu kupata taarifa huko ni free au cheap kulinganisha na mitandaoni ambapo lazima uwe na bando kitu ambacho mtu wa mikoani hawezi kununua GB 4 eti kumuangalia Tundu Lissu akiutubia You tube nazungumzia nchi kwa ujumla si mijini tu CCM si wajinga kuwabana huko wanajua nini wanafanya hapa ungewashauri wafungue vyombo vyao vya habari kama Radio na TV ambazo watakuwa na mamlaka navyo hata kwa wenzetu ambapo Dunia imeamka bado TV ,Magazeti na Radio zina nafasi kubwa sana ktk Ulingo wa kupashana habari pia kwa mfumo uliopo ni mpumbavu pekee anayeweza kusema Lissu au upinzani utachukua nchi ktk miaka hiii 10 au 15 ijayo bado sana .
Nimeongea sana hili suala uliloandika hapa.
Watu wenye kufanya kampeni au wenye mahaba au wasiojielewa watakupinga hadharani au watakutukana kabisa lakini huu ndiyo ukweli wa mambo.

Wasubirie October 28, 2020 wataona uhalisia labda beberu atie mkono wake kama sehemu zingine walikotia mkono na kupi ndua meza kibabe.
Lissu au Membe labda watasaidia tu kuokoa viti angalau vitatu au vinne vilivyokuwa viende kwa CCM ndani ya bunge.
 
Hakuna chama cha upinzani ambacho kimejiandaa kuunda serikali coz kushinda uchaguzi vyama vya upinzani hasa kwa nchi za Africa ni mchakato mrefu na mipango ya muda mrefu kitu ambacho hakuna chama cha upinzani Tanzania wameshafanya hata robo nadhani wao wanagombania kuwa ni chama gani kitakuwa chama kikuu cha upinzani

"Wananchi wenye kuaccess Internet ni milion 22.3 sawa na asilimia 41.4 ya wananchi wote " Hahahaaaa ulishajiuliza Tanzania ni mambo gani au vitu gani vinafatiliwa au kugoogle sana kwenye Internet utashangaa sana nikwambie kitu watanzania hawafatilii siasa kwenye mitandao ni asilimia chache sana hata ukifanya utafiti utagundua ni Twitter tu ndo wanafatilia siasa but sehemu au mitandao mingine nadhani unajua nn kinafatiliwa sasa jiulize Twitter ni watanzania wangapi wana account huko??

Tanzania bado main stream media(TV,Magazeti,Radio) bado zinanguvu sana na bado zinafatiliwa na watu wengi kwa sababu kupata taarifa huko ni free au cheap kulinganisha na mitandaoni ambapo lazima uwe na bando kitu ambacho mtu wa mikoani hawezi kununua GB 4 eti kumuangalia Tundu Lissu akiutubia You tube nazungumzia nchi kwa ujumla si mijini tu CCM si wajinga kuwabana huko wanajua nini wanafanya hapa ungewashauri wafungue vyombo vyao vya habari kama Radio na TV ambazo watakuwa na mamlaka navyo hata kwa wenzetu ambapo Dunia imeamka bado TV ,Magazeti na Radio zina nafasi kubwa sana ktk Ulingo wa kupashana habari pia kwa mfumo uliopo ni mpumbavu pekee anayeweza kusema Lissu au upinzani utachukua nchi ktk miaka hiii 10 au 15 ijayo bado sana .
Why mpo bize kuuwa upinzani,plus sheria kandamizi kila siku.
Habari zitawafikia tu watu,sio kila mtz ana mawazo ya kijima,zitatumika hata tv za nje iwe live au recorded na sio lzm waje nchini watatumiwa habari watarusha je mtazuia na decoder zote, mtazuia Bluetooth,cd,flash nk.
Kuzuia habari Ni sawa na kuzuia upepo usisambae.
Hotuba yote ya Lisu ipo citizen Kenya vipi mtazuia na media za nje zisiripoti wakiwa kwao pasipolazimika waje nchini kuchukua habari,
 
Why mpo bize kuuwa upinzani,plus sheria kandamizi kila siku.
Habari zitawafikia tu watu,sio kila mtz ana mawazo ya kijima,zitatumika hata tv za nje iwe live au recorded na sio lzm waje nchini watatumiwa habari watarusha je mtazuia na decoder zote, mtazuia Bluetooth,cd,flash nk.
Kuzuia habari Ni sawa na kuzuia upepo usisambae.
Hotuba yote ya Lisu ipo citizen Kenya vipi mtazuia na media za nje zisiripoti wakiwa kwao pasipolazimika waje nchini kuchukua habari,
Mkuu unapozungumzia Ushindi wa uchaguzi si ushindi wa kubet au ushindi wa Yanga na Simba uchaguzi ushindi wake unaamua maslai mapana na muelekeo wa nchi ktk kipindi cha miaka 5 pia unatakiwa kujua kuna wakt Democrasia inaweza kuzuiwa nikupe mfano tu kuwa waandamanaji walipigwa tena mbele ya Ikulu ya Rais wa US ambae wote tunaamini ni Baba wa haki za binadamu na Democrasia unajua walipigiwa nini ?

Wamepigwa kisa Donald Trump apate kupita kwenda kupiga Picha mbele ya kanisa huku ameshika bible
 
Mkuu unapozungumzia Ushindi wa uchaguzi si ushindi wa kubet au ushindi wa Yanga na Simba uchaguzi ushindi wake unaamua maslai mapana na muelekeo wa nchi ktk kipindi cha miaka 5 pia unatakiwa kujua kuna wakt Democrasia inaweza kuzuiwa nikupe mfano tu kuwa waandamanaji walipigwa tena mbele ya Ikulu ya Rais wa US ambae wote tunaamini ni Baba wa haki za binadamu na Democrasia unajua walipigiwa nini ?

Wamepigwa kisa Donald Trump apate kupita kwenda kupiga Picha mbele ya kanisa huku ameshika bible
Demokrasia Ina mipaka yake sio kila kitu ni huru lkn huwezi wanyima wengi haki kwa maaslai ya wachache
 
Ccm Ni chama Cha zamani, nyakati hizi lazima kipate wakati mgumu kukabili hoja kinzani. Wao wanaishi miaka ya nyerere Kule, wananchi wanaishi miaka ya kidigitali. Sishangai ccm na serikali yake kuhangaika na redio na TV Yani hawajui kabisa hivyo vyombo kwa Sasa Dunia inaviacha na walimwengu(watanzania) sio wale wa 1960s
 
Hawana ujanja huo sababu awazimiliki media,hizi ni zama za dotcom sio zama za zidumu fikra za mwalimu hichi ni kizazi huru.
Tuliwaonya ccm msizuie wapinzani kufanya siasa hawakusikia wao wametamba miaka mitano pekee yao,leo wananchi wanataka wasikie wapinzani watasema nini,wanawazuia.Ccm hawna jipya la kuongea kwa wananchi yoote washaongea kwa miaka 5 ZAIDI YATAKUWA NI MARUDIO TU nayo ni mabeberu,sgr,ndege,flyover,stiglers kipi kipya wanacho zaidi ya hivo.Huku wapinzani wanazvyo zaidi ya 70 vya kuongea
 
CCM hawana Jipya, ni marudio tu ya SGR, Ndege, Stieglers

Wananchi wameyachoka hayo wanataka kusikia upande wa pili wa shilingi
 
Back
Top Bottom