Zamani sie watu wa mikoani asilimia kubwa tulikuwa tunajua hawa jamaa wanaishi Dar.

Zena na Betina walikuwa wanazibuana Sanaa.
 
Sokomoko mnywa gongo

Kipepe muwindaji ila Hakuna windo anapata kutwa yeye majanga

Pimbi huyu anatongoza ila ambulii kitu

Professor ndumilakuwila yaani huyu ni mwizi Atari toka aende dar mwaka 1982 mpaka Leo analala chini


Sukununu huyu sometimes ni mmbea mpekunyuzi


Kifimbo cheza huyu mzee ni mnoku sana alifanya wahuni wasiongee kwa amani maana alikuwa anavizia maskani na fimbo zake anawasikiliza mkiaribu lugha mtakipata ila aliacha baaada ya kuvamia sipo unajua alifanyaje? Basi fatilia

Madenge huyu dogo sio bure atakuwa anavuta bangi si kwa vituko vile mda wote anatembea na manati yake ameivaa shingoni

Lodilofa huyu jamaa anajikuta sana na kigari chake kile kitakuwa ni ist ana majibu ya shombo namfananisha na jamaa Fulani humu jamvini unajua ni Nani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…