Zamaradi ataja ujio wa filamu yake aliyoiandaa kwa Milioni 200

Zamaradi ataja ujio wa filamu yake aliyoiandaa kwa Milioni 200

Ijumaa ile iliyopita nilikuwa samaki samaki masaki nikaonyeshwa gari ya sebastian ndege ile discovery nikaambiwa mumewe zama ndio kaipiga rangi...mbona rangi yenyewe mbaya vile. Hii hela angewekeza kwny gereji ya mumewe tu


Sent using Jamii Forums mobile app
Una majungu baba wewe 🤣🤣[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Jamani acheni kuponda nimeangalia trailer hiyo movie inaonyesha ni nzuri mno. Ipo level za juu. Kuanzia camera, soundtracks, story. A bit action. Kajitahidi kwa kweli. Angalieni trailer kwanza.sio za kimapenzi mwanzo mwisho
 
Ijumaa ile iliyopita nilikuwa samaki samaki masaki nikaonyeshwa gari ya sebastian ndege ile discovery nikaambiwa mumewe zama ndio kaipiga rangi...mbona rangi yenyewe mbaya vile. Hii hela angewekeza kwny gereji ya mumewe tu


Sent using Jamii Forums mobile app
Kwaio mara mia angepeleka kwa mnyawezi ommy_painter gari ingekua kama mpya...sio...
 
Dada Zama muda huu anaongea na Waandishi wa habari kasema kuwa kuna ujio wa filamu yake yenye mapigano ndani ambayo ameiandaa kwa millioni miambili
====

Mtangazaji maarufu nchini Tanzania, Zamaradi Mketema amekuja na filamu iliyomgharimu Sh200 milioni katika kuitengeneza huku akieleza kuwa filamu hiyo imekuja kuleta mapinduzi katika sekta ya filamu.

Filamu hiyo inayoitwa 'Cop's Enemy' aliyoanza kuitengenezwa tangu mwaka 2016 na prodyuza John K, imechezwa katika nchi tatu ikiwemo Tanzania, Australia na India.

Wakati wasanii walioshirikishwa wamo Wema Sepetu, Stanlenley Msungu na Aunt Ezekiel kutoka Bongo, Van Vicker wa Ghana na wengine kutoka Nigeria, India na Australia.

Zamaradi ambaye aliwahi kuongoza filamu ya Kigodoro Kantangaze na Nzowa, akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Februari 4, 2019 amesema utengenezaji wa filamu hiyo ya gharama umelenga kuleta mapinduzi katika tasnia ya filamu hapa nchini ambayo imeonekana kushuka.

Amesema kutokana na hilo hakuhofia gharama watakazotumia kwani shida ilikuwa wafanye kitu kizuri kitakachorudisha heshima ya filamu nchini Tanzania.

Kwa upande wa waongozaji yupo Neema Ndempayo na John K kutoka nchini Australia ambaye pia ni mmoja wa wahusika katika filamu hiyo.

Sent using Jamii Forums mobile app

Chanzo cha mapato yake ni kipi huyu dada, Au wadhamini ndio wametoa mshiko mrefu ivyo.
 
Back
Top Bottom