Zamu ya Club ya Simba kupitisha bakuli la michango.

Zamu ya Club ya Simba kupitisha bakuli la michango.

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
20,137
Reaction score
26,189
Waswahili wanasema ukiona mwenzako kanyolewa zako tia maji ,na kwa hakika hawakukosea kabisaaa.


Hawa watani zetu wa jadi Simba SC walitucheka sana kipindi kile Manji alivyopata matatizo ambapo kwa kiasi kikubwa kuliathiri maendeleo ya timu yetu na kusababisha kukosa ubingwa.

Kipindi ambacho timu yetu ilikuwa inapitisha mara kwa mara bakuli la michango ili kusaidia maendeleo ya timu yetu.

Sasa kibao kimewageukia wapinzani wetu, wajiandae kisaikolojia kwa ukata utakaoanza muda sio mrefu ndani ya Club yao.
 
Waswahili wanasema ukiona mwenzako kanyolewa zako tia maji ,na kwa hakika hawakukosea kabisaaa.


Hawa watani zetu wa jadi Simba SC walitucheka sana kipindi kile Manji alivyopata matatizo ambapo kwa kiasi kikubwa kuliathiri maendeleo ya timu yetu na kusababisha kukosa ubingwa.

Kipindi ambacho timu yetu ilikuwa inapitisha mara kwa mara bakuli la michango ili kusaidia maendeleo ya timu yetu.

Sasa kibao kimewageukia wapinzani wetu, wajiandae kisaikolojia kwa ukata utakaoanza muda sio mrefu ndani ya Club yao.
Mkuu umeniwahi nilitaka kusema..
Hapo ndo utajua mpira kuendelea Tanzania ni kazi ngumu sana..

Tukutane mtaani, tugawane mitaa na kupeana zamu ya kutembeza bakuli
 
Bado naamini Mo atapatikana na ataendelea kuwekeza simba! Ila viongozi, wanachama na wapenzi wa simba wanapaswa kupunguza au kuacha dhihaka dhidi ya Yanga! Hakuna aijuae kesho yake!
 
Adui muombee njaa.
Tukiombeana, njaa, kwa mtindo huu wa kuwateka wanasaodia vilabu, nchi haitakalika.

Jali utu wa mtu kwanza, sioni sababu Ya nyie kufurahia hali hii. Mo halionyesha njia kwenye soka letu, yeye alianza kupitia Simba, mwingine angefuata kupitia Yanga.
Alafu ya Manji yalikua nafuu, alikua anajulikana yupo wapi, sasa huyu hajulini, kama sababu ni hiyo bora mumlazimishe aachane na kuisaidia Simba, Mumuachie Uhai wake na uhuru wake.
 
Usijeshangaa kina kagere,Chama,Okwi wanasepa,maana mlipaji hayupo tena, sijui manara siku akiwa anatangaza namba ya michango atavaa mask?? Maana alitusema vibaya sana Yanga

BRING BACK OUR MO
 
Simba The Greater
Hawana Tatizo Sasa Bakuli La Nini
 
Back
Top Bottom