Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,584
- 6,136
Wachangiaji,
Nimekuwa napita na kusoma kuwa Tanganyika imekuwa ikiibia pesa Zerikali ya Zanzibar. Misaada ikija kwa Tanzania, inapelekwa Tanganyika tu. Pesa za kodi zikikusanywa na Wazanzibar, zinapelekwa Wizara ya fedha ya Muungano na wao hawapati kitu. Pesa za utalii, karafuu nk zinakusanywa na zinapelekwa Tanganyika na kuwa za Muungano. Hapo wao hawapati kitu kwani serikali ya Muungano ni kwa Tanganyika tu na serikali ya Zanzibar inabaki kujihangaikia kutafuta visenti vyake vyenyewe. Kama ni kweli basi kweli Zanzibar wameonewa na kuibiwa kwa miaka 40. Na kweli inasikitisha.
Maswali yangu hapa ni kama ifuatavyo:-
1: Hivi tunachangia wizara ngapi?
2: Hizi wizara ambazo hazimo katika Muungano, je wanagawana vipi majukumu? Tuseme wizara ya Utalii, ipo ya Zanzibar na Muungano. Hawa jamaa kazi zao zikoje?
3: Kama wizara ya fedha tunachangia, kwa maana hiyo hata TRA tunachangia sasa Zanzibar wakikusanya pesa zao kodi zinakwenda wapi?
4: Wizara zisizo katika Muungano yaani zipo Zenji tu, je wanapata wapi fedha kujiendesha?
5: Wizara za Muungano, zinalipiwa na Watu wote au ni Watanganyika tu (ukiacha ya fedha). Hapa tuseme Wanajeshi, Polisi, magereza, Mabalozi nk.
6: Mgawanyiko wa fedha ukoje? Hapa ni hii wizara ya fedha.
Naomba kama mchangiaji atakuwa na ya kuongeza basi ntashukuru sana. Nataka kujua kwa nini tugawane mafuta. Kama hii itakuwa ni pato la taifa basi si kuwa pesa zinakwenda Wizara ya fedha na huko tunagawana wote? Kama fedha za Madini, Gas, Utalii nk zinakwenda TRA na huko tunagawana wote, kwa nini Wazenji wanasema wao hawapati? Wizi huo hutokea wapi? Pia kama Gas ikishaanza kutumika majumbani, Tanzania bara wananchi si watauziwa? Mafuta hata kama yakipatikana Zanzibar, sisi wananchi wa kawaida si tutauziwa? Fedha zote zinakwenda katika kapu moja. Naomba ufafanuo wa hayo maana naona naelewa vitu nusunusu au sielewi kabisa.
MODS: Naomba muiache kwa muda na baadaye ichanganye kwenye ile ya Mtaalam aliyedai ZNZ hakuna mafuta akabidhi ripoti kwa SMZ!!
Nimekuwa napita na kusoma kuwa Tanganyika imekuwa ikiibia pesa Zerikali ya Zanzibar. Misaada ikija kwa Tanzania, inapelekwa Tanganyika tu. Pesa za kodi zikikusanywa na Wazanzibar, zinapelekwa Wizara ya fedha ya Muungano na wao hawapati kitu. Pesa za utalii, karafuu nk zinakusanywa na zinapelekwa Tanganyika na kuwa za Muungano. Hapo wao hawapati kitu kwani serikali ya Muungano ni kwa Tanganyika tu na serikali ya Zanzibar inabaki kujihangaikia kutafuta visenti vyake vyenyewe. Kama ni kweli basi kweli Zanzibar wameonewa na kuibiwa kwa miaka 40. Na kweli inasikitisha.
Maswali yangu hapa ni kama ifuatavyo:-
1: Hivi tunachangia wizara ngapi?
2: Hizi wizara ambazo hazimo katika Muungano, je wanagawana vipi majukumu? Tuseme wizara ya Utalii, ipo ya Zanzibar na Muungano. Hawa jamaa kazi zao zikoje?
3: Kama wizara ya fedha tunachangia, kwa maana hiyo hata TRA tunachangia sasa Zanzibar wakikusanya pesa zao kodi zinakwenda wapi?
4: Wizara zisizo katika Muungano yaani zipo Zenji tu, je wanapata wapi fedha kujiendesha?
5: Wizara za Muungano, zinalipiwa na Watu wote au ni Watanganyika tu (ukiacha ya fedha). Hapa tuseme Wanajeshi, Polisi, magereza, Mabalozi nk.
6: Mgawanyiko wa fedha ukoje? Hapa ni hii wizara ya fedha.
Naomba kama mchangiaji atakuwa na ya kuongeza basi ntashukuru sana. Nataka kujua kwa nini tugawane mafuta. Kama hii itakuwa ni pato la taifa basi si kuwa pesa zinakwenda Wizara ya fedha na huko tunagawana wote? Kama fedha za Madini, Gas, Utalii nk zinakwenda TRA na huko tunagawana wote, kwa nini Wazenji wanasema wao hawapati? Wizi huo hutokea wapi? Pia kama Gas ikishaanza kutumika majumbani, Tanzania bara wananchi si watauziwa? Mafuta hata kama yakipatikana Zanzibar, sisi wananchi wa kawaida si tutauziwa? Fedha zote zinakwenda katika kapu moja. Naomba ufafanuo wa hayo maana naona naelewa vitu nusunusu au sielewi kabisa.
MODS: Naomba muiache kwa muda na baadaye ichanganye kwenye ile ya Mtaalam aliyedai ZNZ hakuna mafuta akabidhi ripoti kwa SMZ!!