Zanzibar: Rais Samia alikutana na Viongozi wa ACT Wazalendo kwa mazungumzo

Zanzibar: Rais Samia alikutana na Viongozi wa ACT Wazalendo kwa mazungumzo

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,358
Katika Hali ya kushangaza Chama Cha ACT Wazalendo kupitia Makamo wa Rais Zanzibar kimefichua kupata mwaliko wa kuonana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri Samia Suluhu Hassan.Hayo yamefanyika huku Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe alibambikwa kesi ya Ugaidi na wakuu wa Serikali wakionekana wazi wazi kuingilia mhimili wa Mahakama kuhusu kesi hiyo.

Ifuatayo ni habari iliyochapishwa na gazeti la Mwananchi Kama alivyonukuliwa Makamo wa Rais Zanzibar Othman Massoud.....

Rais akutana na ACT na kufikia muafaka huku akipiga danadana kuonana na CHADEMA

Makamo wa Rais Othman Massoud afichua Siri hiyo

Alisema walipata wito wa Rais Samia wa kuonana naye Unguja na alikwenda yeye, makamu mwenyekiti wa chama hicho, Zanzibar Juma Duni Haji na Naibu Katibu (Zanzibar), Nassor Ahmed Mazrui.

Wengine ni Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa chama hicho, Salim Biman na mwanasheria wa ACT-Wazalendo Omar Said Shaaban.

“Tukamueleza kuwa hatukukwama labda hatukueleweka. Tukamwambia njia na hoja zetu ni hizi kama tulivyoeleza Pemba hatuna cha kubadilisha.

“Tulifikia mwafaka kuwa watakwenda kukaa na kuchukua hatua, hatua ndiyo hii mliyoiona, operesheni imefanywa tumesema tulieleze hili pengine hakukuwa na haja ya kulizungumza. Lakini tunasema ili dunia itusikie,kama ni changamoto za kifamilia sawa,” alisema Othman.

Maoni ya Wananchi baada ya Rais kukutana na ACT kisiri Unguja

Ni vyema Ikulu ikaweka hadharani mazungumzo haya na kilichoamuliwa kwani Kama si Makamo wa Rais Zanzibar kufichua Siri isingejulikana.

Pili wananchi hasa upande wa bara wanaweza kuhisi upendeleo fulani wa kieneo kwa sababu kwanini Rais aende kisiri kukutana na ACT huko Unguja na kutatua mtanziko wa kisiasa lakini kwa upande wa Bara kiongozi wa Chama kikuu anafunguliwa mashtaka ya kubambika ya Ugaidi.

Kuna mambo mengi ya kujiuliza lakini Ni vyema Ikulu wakaondoa hofu hii mapema
 
Kinachotuponza waAfrika ni kuaminiamini kila mchezo,huwezi kuitenganisha serikali na mbowe kwani ni mtu na mwajiri wake kinachofanyika ni kuugeuza ubongo wa waAfrika up side down na kuwahamisha kutoka katika MADA nyeti.
 
Asanten Sana ACT maana nyie mnaweza kuwa wanasiasa wenye kujali amani hao wapumbavu CHADEMA wafutwe tu

Chama kimejaa magaidi
USSR
 
N jambo zuri kwa mstakabali wa SUK. Kwa upande wa Mboye mchakato wa mahakama uheshimiwe mahakama itatoa haki.
 
Mazungumzo ndio silaha kubwa ya ukombozi wa matatizo yetu. Na vile vile ni nafasi nafasi ya kuwasemea hata hao walioshtakiwa. Rais wetu SSH ni msikivu, twende naye pole pole.
 
Asanten Sana ACT maana nyie mnaweza kuwa wanasiasa wenye kujali amani hao wapumbavu CHADEMA wafutwe tu

Chama kimejaa magaidi
USSR
Nyie na vyama vya mifukoni mwenu wote ndio watesi Wa wa Tanzania.
 
Ingekuwa kulalamika na uongo ndio sera na ilani wanazozihitaji watanzania, basi chadema kingekuwa ikulu siku nyingi. Lkn kwa vile malalamiko na uongo sio kipaumbele cha watanzania, ndio maana haishangazi kuona uongo wote, malalamiko na propaganda chovu za chadema na wapinzan kwa ujumla zimeshindwa kuwapatia hata wabunge watatu achilia mbali uraisi. Hata huu uongo na propaganda vilivyoandikwa na mleta mada vitapita kama vilivyopita vingine, na uchaguzi mkuu ukifika wataangukia pua kama ilivyo desturi yao.
 
Back
Top Bottom