Zanzibar: TRA yatoa zawadi kwa vilabu vya kodi

Zanzibar: TRA yatoa zawadi kwa vilabu vya kodi

TRA Tanzania

Senior Member
Joined
Jul 16, 2022
Posts
128
Reaction score
370
dc zanzibar 2.jpg

Naibu Kamishna Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA - Zanzibar Bw. Saleh Haji Pandu amesema wataendelea kuvilea vilabu vya kodi mashuleni ili kuwaandaa watoto kuwa walipokodi wazuri wa baadae na kuwa mabalozi kwa jamiii juu ya ulipaji kodi kwa hiyari.

Bw. Pandu ameyasema hayo tarehe 23/11/2024 kabla ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa shindano ya vilabu vya kodi kwa shule za sekondari za Unguja Zanzibar ambapo Skuli ya Sekondari ya Haillesellasie imeshinda nafasi ya kwanza katika uwasilishaji wa mada , Skuli ya sekondari ya Biashara imeshinda nafasi ya kwanza katika Maswali ya papo kwa papo, Skuli ya Zanzibar Feza imeshinda nafasi ya kwanza katika ukusanyaji wa risiti za kielecroniki na skuli ya Trifonia Academy imeshinda nafasi ya kwanza katika uandishi wa Insha.

Washindi hao walitunukiwa zawadi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Desktop Comouter, Jezi za mpira, tuzo, rimu za karatasi, mabegi pamoja na chupa zenye nembo ya TRA.
dc zanzibar 1.jpg
dc Zanzibar.jpg
 
Kumbe kuna TRA Zanzibar imeanza lini sijui hui.maana nilikuwa najua ile Bord ya mapato Zanziba ZRB.halafu kwa nini kuna kodi tofauti ya forodha kati ya Bara na Zanzibar?
 
Kumbe kuna TRA Zanzibar,imeanza lini sijui hui.maana nilikuwa najua ile Bord ya mapato Zanziba ZRB.halafu kwa nini kuna kodi tofauti ya forodha kati ya Bara na Zanzibar?
TRA ipo Zanzibar kitambo kwani ni Mamlaka ya Mapato Tanzania. Toka kuanzishwa kwake 1996 ilikuwepo. Kodi ya forodha ni moja sababu sheria inatumika ya Afrika Mashariki.
 
TRA ipo Zanzibar kitambo kwani ni Mamlaka ya Mapato Tanzania. Toka kuanzishwa kwake 1996 ilikuwepo. Kodi ya forodha ni moja sababu sheria inatumika ya Afrika Mashariki.
Sasa hii ikoje.Maana TRA iko chini ya wizara ya fedha,na wizara ya fedha siyo ya Muungano.yaani zanzibar wanayo wizara yao ya fedha.so hayo mapato yanayokusanywa yanapelekwa wapi
 
Hivi TRA huwa inalipa kodi kwa nani?, maana ni taasisi taxable kama taasisi zingine..
 
Back
Top Bottom