Zanzibar wanatumia mpira wa miguu kunung'unika.

Zanzibar wanatumia mpira wa miguu kunung'unika.

Sasa nimekuelewa. Kwamba unataka kwenye kusherehekea ushindi kila shabiki awe mstaarabu, muungwana, mzalendo na mnyenyekevu kwa kadri unavyohisi wewe ni sahihi. Hilo haliwezekani popote pale duniani. Unapaswa kusikiliza maoni na matamshi ya wahusika wakuu wa timu inayoshangilia. Laiti kauli hizo zilizokuudhi zingetolewa na Kocha (aliyewashukuru Watanzania wote) na/au viongozi wengine, ungekuwa na hoja. Ni lini Simba na Yanga zinapofungana umesikia mashabiki wa aliyeshinda wakimpa pole mtani wake mitaani? Umepata kusikia shangwe za mtani aliyeshinda zisimnange mpinzani wake? Wakati wa kusherehekea ushindi, aliyeshindwa anapaswa kujua, kujiandaa na kustahamili kauli za maudhi, ambazo mara nyingi ni mfululizo wa kutambiana kulikoanza kabla ya mpambano. Simba kuitwa wa mchangani/matopeni hajatukanwa na Yanga. Yanga kuitwa gongowazi hajatukanwa na Simba. Kama pilipili inavyonogesha ladha ya chakula licha ya kuwasha, ndivyo utani kama huu unavyonogesha ladha ya mpira licha ya kuwa haumpendezi aliyeshindwa.
Jibu hilo hapo chini
"Machogo" sio matusi ni utani wa zamani sana watu wa Unguja walikuwa wanawaita watu kutoka Mrima(Tanganyika aka Tanzania Bara aka Bongo), vile vile watu wa Unguja walikuwa wanawaita Wapemba "Vibuwa",vibuwa ni samaki wanaovuliwa kwa wingi

""Chogo" maana yake ni kichwa kilicho vimba nyuma...alikuwepo mchezaji mmoja maarufu sana wa simba yeye alikuwa na jina la utani "Chogo chemba"

Hakuna matusi hapo isipokuwa utani wa zamani umerudi,wasiojua wanaona matusi
 
Hii shida haitokwisha bila kukubali katiba ya Mzee warioba. CCM wanajifanya kutoelewa lakini ni sawa na kufunika moto kwa blanket, moto utakuja kuwaka tu tunauchelewesha tu. Wanzanzibari hawatokubali kuendelea kukosa baadhi ya haki zao kama hiyo migao ya FIFA simply because hawatambuliki.

Mi sielewi kwa nini CCM wanaogopa Serikali tatu, hili ndo suruhisho pekee la kupata muungano wenye nguvu. Hata wazanzibari mwenyewe wengi wanapenda muungano lakini wanapenda wawe huru. Sijui mwisho wake nini kuendelea kushikilia watu kwa kutumia mabavu huku wenyewe hawaridhiki.
 
Hakuna Mpemba hata mmoja anayepandikiza chuki hapa. Tatizo wenzetu Tanganyika (sisemi ni wote) mumegeuka mbuni, munahisi mikisha kujificha kichwa basi kwa vile wewe hutoaki kuyaona matatizo basi hakuna anyeyaona.
Muungano huu unamatatizo tokea kuanzishwa kwake. Wapeni watu Uhuru waujadili, na wanapoona panakaso parekebishwe. Vyenginevyo watakuja vijana wengine sisi Hatupo, watafanya wanavyotaka wao.
Hata Marekani kama watapewa fursa leo ya kuujadili muungano wao utavunjika. Waingereza walipewa fursa hiyo ya kuujadili muungano wa Ulaya, ona kilichotokea. Ona kule Catalonia Hispania kilichotaka kutokea. Muungano haujadiliwi, unaboreshwa humo kwa humo ndani kwa ndani. Siri kubwa ya kudumu kwa muungano ni kuongeza uhuru kwa wanandoa kujiamulia mambo yao madogomadogo ya kila siku.
 
Hata Marekani kama watapewa fursa leo ya kuujadili muungano wao utavunjika. Waingereza walipewa fursa hiyo ya kuujadili muungano wa Ulaya, ona kilichotokea. Ona kule Catalonia Hispania kilichotaka kutokea. Muungano haujadiliwi, unaboreshwa humo kwa humo
Usifananishe Muungano wa marekani na huu wa Tanzania, Au Ujerumani na Tanzania.
Wenzetu Kila nchi ina Serikali yake Na Mamlaka yake, halafu ndio kuna Serikali ya Muungano ambayo nayo ina Madaraka yake na hayaingiliani. Ndio maana ukaona Marekani kama United States wanaruhusu ndoa za jinsia moja. Lakini humo marekani kuna nchi ambazo wamepiga marufuku, na Adhabu ya kifo ni Hivyo hivyo.
Wazanzibari hawajasema hawautaki Muungano, wazanzibari wanataka Muungano wa Haki. Kwanza ijitokeze Hiyo Serikali ya Tanganyaika, ijuilkane chanzo chake cha Mapato. Halafu ndio tuseme Hii ndio hiyo Serikali ya Muungano na itaendeshwa vipi? Sio kufanya Mambo kiujanja ujanja hivi, kua hiyo hiyo ni serikali ya Tanganyika wakati huo huo ni ya Muungano.
Munakataa nini? Semeni tu huu ni Ukoloni. Na Wazanzibari wanaelewa hilo tu
 
Hayo ndo mambo yenu Wabara, Zanzibar ipo kabla ya Tanzania na insha Allah itaendelea kuwepo baada ya Tanzania kwanini mnaing'ang'ania Tushasema zaidi ya mara Alfuu hatutaki tuachieni nchi yetu. Mnabaki kusema znz sisi wamoja, umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, mukitubagua sisi na nyie mtabaguana. Ebu iacheni Zanzibar yetu tuwe nchi Jirani. Kwa sababu mnaendelea kuing'ang'ania popote tutakapopata fursa iwe kwenye soka, msiba, harusi na chengine chochote tuta express feeling zetu kwamba hatukubaliani na MUUNGANO huu
Halafu unaweza kukuta wakati unaandika haya yote upo bara,nyie wapemba akili zenu mnazijua wenyewe!
 
Hii shida haitokwisha bila kukubali katiba ya Mzee warioba. CCM wanajifanya kutoelewa lakini ni sawa na kufunika moto kwa blanket, moto utakuja kuwaka tu tunauchelewesha tu. Wanzanzibari hawatokubali kuendelea kukosa baadhi ya haki zao kama hiyo migao ya FIFA simply because hawatambuliki.

Mi sielewi kwa nini CCM wanaogopa Serikali tatu, hili ndo suruhisho pekee la kupata muungano wenye nguvu. Hata wazanzibari mwenyewe wengi wanapenda muungano lakini wanapenda wawe huru. Sijui mwisho wake nini kuendelea kushikilia watu kwa kutumia mabavu huku wenyewe hawaridhiki.
Dawa halisi ya muungano ni serikali ya majimbo yanayojiendesha kwa aina fulani, hivyo kutakuwa na jimbo la Tanga lenye mikoa kadhaa, jimbo la Zanzibar, n.k. vinginevyo huu muungano tulionao sasa ni kiinimacho kweli, unadumishwa kwa mbinde, mizengwe na gharama kubwa za kificho na za waziwazi.

Unaonaje kama Rais na Makamu wake na waziri Mkuu wote wangekuwa wanatoka tanganyika? Kuna kujifunza kwingi sana kunakotuchelewesha sana kama Rais au Makamu atatokea Zanzabar.
 
Back
Top Bottom