Zanzibar: Watalii wanne kutoka Israeli watimuliwa Hotelini kwa kulalamika kuhusu gari kuandikwa "Free Palestine"

Sishabikii wala kutoa maoni yoyote kuhusu yanayoendelea huko mashariki yakati!
Narejea tena! Niliwahi kuandika hapa iko siku mtu mmoja ataiharibu biashara ya utalii kwa kukosa weledi!
 
na watanzania pia hawataki ujinga wa meneja huyo kubandika stika hiyo
 
Hawa ni moja ya jamii ya watu wapumbavu sana.

Ogopa sana jamii ya watu isiyojifunza na kutaka kubadilika katika historia yake.

Wanapaswa kubadilika na kuachana na fikra zao za kijinga kijinga wasipofanya hivyo dunia itawa badilisha kwa nguvu.
Dunia ipi wakati dunia hii ni yao? Na wangemjua meneja wa gari hiyo wangemga nakoz za uso ashike adabu zake. Zanzibar sio gaza, huo upuuzi wake akaoneshe huko gaza
 
Unachanganya mifano yako unataka kuonesha Manager ana makosa wakati sio kweli.

Manager wa Hotel ni mtu mwenye Weledi mkubwa wa hiyo Biashara usitake kumfundisha hapa.
huyo meneja ni mpuuzi acha kutetea ujinga, inawezekana alionesha bango hilo kwa waisrael hao waka mind. Wangemshikisha adabu palepale endapo wangembaini ni mwenye gari hilo. Huo ushenzi haufanyiki kwa watalii wanaotalii bara, tukiona sie wenyewe tunalishughulikia kabla watalii walengwa hawajaliona, hatutaki mkosi/nuksi na uchuro huo kwa vivutio vyetu tunakopata fedha kwa maendeleo ya nchi yetu
 
[emoji16][emoji16]
 
Uko sahihi
 
Manager na watalii wote majuha.
 
Sahihi, wenzetu wakilipa pesa yao wanataka huduma bora, mtoa huduma ukizungua lazima mzinguane hapo hapo na hata hiyo pesa utaitapika.
Sisi tumezoea mfano unaenda hotel inasema naomba chakula wali kuku Kenya hoteli nyingi ulisema unaomba chakula wanaoweza kukufukuza kuwa hii hapa sio sehemu ya ombaomba sisi tunauza chakula.Wewe mwambie Lete chakula sio naomba chakula.

Mzungu anapolipa ananunua huduma hivyo anataka apate thamani ya alicholipia Sababu hiyo huduma kalipia sio.hisani na hahitaji kujikbakomba wakati kalipa.Ndio maana waliwaka wako pale hotelini wamejichokea na mavita Yao huko kwao wanaondoka kuja ku relax kuanzia hisia ,fikra na moyo halafu meneja anakuja na mgari wake na bango la free Palestine Lazima wawake.
 
Umetafakari kwa kina au umekurupuka kumbuka Hilo ni gari binafsi ni kama wewe ukiwa na gari yako ndani umeweka bendera ya Chadema afu ukalipaki kazini kwako afu wafuasi wa CCM walalamike
Hapo utashi wa Manager umekosesha mapato hotel na sio ajabu wasipate tena Wageni kutoka Israel.
 
Manager mjinga kabisa Asiyejua maana ya Biashara. Kuna interest zingine haziwekwi public unapokuwa Unafanya Biashara Zinazowagusa watu moja Kwa moja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ