warumi
R I P
- May 6, 2013
- 16,218
- 18,440
Kupitia kwenye kipindi cha XXL kinachorushwa Clouds FM, msanii Diamond Platnums, amezungumzia uzinduzi wa Tv station yake binafsi atakayoizindua Mei 1 kwenye Party ya Zari inayofahamika kama Zari All white party itakayofanyika Mlimani City.
All the best kama sio kick.
=======
YALIYOJIRI KWENYE ONYESHO LA ZARI ALL WHITE PARTY - MLIMANI CITY HALL , DSM - TANZANIA (1/5/2015):
All the best kama sio kick.
=======
YALIYOJIRI KWENYE ONYESHO LA ZARI ALL WHITE PARTY - MLIMANI CITY HALL , DSM - TANZANIA (1/5/2015):
Live Stream Update
View attachment 248446
live streaming update.....ila hawa jamaa wa clouds yaonekana kwenye haya mambo ya live stream bado sana.picha ina stuck na sauti mbaya.
View attachment 248459
Ebwana hii ZARI ALLWHITE PARTY umemuacha hoi. Yani Chua alikuwepo, Minja alikuwepo, Matayo alikuwe, Msele alikuwepo, Mrema alikuwepo...na wengine wengi walikuwepo (in chagaz voice).
Bila kumsahau Bob junior ambae amemfurahisha sana Platnumz na mashabiki zake kwa hilo. Hii ikimaanisha hawana bifu tenaa. Mnyama TID mmemuona mapemaa. Ila mzee wa kufuta vumbi kiti Vp bwana......Mbona sikuoni? Why? Kwanini? Hakika unazidi kujitenga na wasanii wenzako huku Platnumz akiendelea kuwaongeza.
Msalimie na Mr. Wanjera
Binafsi nimeona kama nimemzulumu diamond na zari kwa 50,000 niliyotoa.haiwezekani raha zote za jana kuanzia burudani ya YAMOTO BAND,venessa , AKA, swaga za diamond na ney wa mitego,uchekeshaji ulienda shule wa Eric Omond, jamaa anachekesha saa zima na bado hadhira haitaki aondoke stejini.
Dah nimesahau kijana anayekuja kwa kasi shettah bila ya kumsahau bob junior yaani ilikuwa IMENUKA.
Mwisho kabisa shoo ya masaa 3 consecutive ya Diamond akisindikizwa na Khadija Kopa, Ney wa Mitego.
Kwa hakika kupata hivyo vyote kwa 50,000 ni dhuluma ya hali juu