Zembwela katika Super mix

Ernesto Che

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2011
Posts
1,114
Reaction score
293
Habari wakuu,

Nimekuwa msikilizaji mzuri wa kipindi cha supa mix cha East africa Radio kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 7 mchana. Kipindi hiki kinatangazwa na Zembwela (mchekeshaji wa zamani) na mwanadada mwingine.

kinachonikera katika kipindi hiki ni upotoshaji mkubwa wa Zembwela, ambaye siamni kama ana elimu nzuri (kulingana na hoja zake) zaidi ya kuongea mambo asiyoyajua hovyo hovyo. Kazi yake kubwa ni kukebehi wabunge, serikali za mitaa n.k. bila kutoa uchambuzi yakinifu. Utangazaji huu haufai kwa maendeleo ya taifa kwani mtangazaji anatakiwa kuchambua jambo ambalo ana ufahamu nalo, na iwapo hana ufahamu wa kutosha basi aalike wataalamu wa fani husika ili watoe habari kwa kina.

Zembwela anaropoka ovyo kiasi cha kukera wasikilizaji makini,

Rai - Zembwela ulikuwa mchekeshaji mahiri, usikurupukie fani ambazo una uelewa finyu. Nakushauri uwe na busara ukufahamu kuwa unasikiliza na watanzania wenye uelewa tofauti, punguza uropokaji usio na tija.
 
yaani hicho kipindi toka yule nani aondooke akabaki zimbwila hakina mvuto kabiiisaaaaa. jamaa anajifanya anajua kila kila, alafu anawexa kumualika mgeni lkn chakushangaza yeye ndio muongeji sana juu ya hiyo mada kuliko mgeni, mara amfundishe mgeni, alafu anajifanya anajua sana kiswahili fasaha kumbe giza tuuu.
 
jamaa kabofoa nini tena.Hebu tupiamo tumfano tuone alivyokurupuka!
 
nilishaacha kusikiliza hicho kipindi, tatizo kubwa la huyu bwana mdogo ni kulazimisha mawazo yake finyu yawe ya watu wote hususani vijana, na anasifa ya uongo, mwanzo alipokuwa anariport kutokea field alikuwa anaeleza location nyingine wakati hayupo na watu wanamuona live akidanganya.
 
Hillary Daudi Mtuta aka Zembwela ametoka mbali sana.Mhurumieni bure tu. Lazima afanye hivyo ili aishi mjini. Lakini,atakayetukanwa naye yu huru kumshtaki
 
toka jana anakomaa na hospitali ya palestina. mlango ukifunguliwa unapiga kelele. we unamwona kituko ukisikiliza jumbe zinatotumwa super mix wapo wanaodiriki kusema anafaa kuwa raisi wetu. anavijua vituo vya mabasi kuanzia ubungo hadi morogoro.
 
kuna yule kijana alikuwa anatangaza kipindi cha uswazi EATV ndio alikuwa anakiweza kiasi
hivho kipindi watafute watangazaji mahiri wenye elimu stahiki.
 

Huku si mahala pake zumbukuku wewe.
 
Wenyeviti wa serikali za mitaa nyie nini? Pamoja na upotoshaji kama mnavyodai yako ya msingi anayoyazungumza
 
Kipindi kimemzidi uwezo!
Kipindi hiki kinahitaji mtu mwenye busara na anaejua kuchambua mambo kwa kina!
Tatizo la vyombo vyetu vya habari ukishakuwa tu na maneno mengi na uwezo wa kuchanganya changanya na vituko wanakupa vipindi
Sina uhakika kama jamaa ana elimu yoyote hata ya certificate ya utangazaji
Angebaki tu kwenye kuchekesha pale anafit
Tatizo wengi tulishazoea kumuona kwenye vichekesho,so sometime anajisahau anajua anachekesha hata kwenye vitu vya serious

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Kwani unaweza kuwa mtangazaji bila kusomea na kama alisomea mbona anavuka mipaka au bosi wake haoni.
 
Huyu jamaa ninachompendea anazungumzia matatizo yanayoizunguka jamii hasa ya Mtanzania

Keep up my bro!

Acha mapovu yawatoke wanafiki wanaojifanya ni wageni ktk nchi hii!
 
Ukijua tu kuongea unakuwa mtangazaji

Ni kama ilivyo kwa tasnia ya muziki yaani kila mtu anataka kuwa mwanamuziki, wao wanajiita eti wasanii, usisahau na wacheza filam huko ndo utacheka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…