Ngorunde
Platinum Member
- Nov 17, 2006
- 4,672
- 9,806
Hata NAPE alituarifu tujiandae kisaikolojia kuhusu wizi wenu wa kura.Kaishi tu huko porini, Ila jua mwakani ni KURA za kishindo kwa Samia
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata NAPE alituarifu tujiandae kisaikolojia kuhusu wizi wenu wa kura.Kaishi tu huko porini, Ila jua mwakani ni KURA za kishindo kwa Samia
Ninyi mpen TU za kishindo, ila ipo cku mtajua hamjuiKaishi tu huko porini, Ila jua mwakani ni KURA za kishindo kwa Samia
Acha hzo mkuu hii ni milele na mileleNinyi mpen TU za kishindo, ila ipo cku mtajua hamjui
Swali gani hili na wwUWT mlikuwa wangapi?
Hata panaposemwa hupajui Ila Uchawa unakusumbua. Acha TAKUKURU wafanye kazi uongo wangu utadhihirika.Unauhakika kuwa ww ni mwandishi wa habar?
Acha kutungua story mm npo hapa hayo unayasema ni uongo mtupu
sema tu umeumizwa na nyomi la watu kwenye ziara ya Mh. Rais wetu mpendwa Dr Samia Suluhu Hassan
Nchi ya kitu kidogo, nchi ya watu wadogo.Asubuhi ya Leo majira ya saa 5 hivi nimepishana na msafara wa Rais ukitokea mkoa wa Rukwa kuelekea Songwe. Binafsi kama Mwandishi wa habari za mazingira naelekea mwambao wa ziwa Tanganyika kikazi. Nilipofika Namanyere wilaya ya Nkasi nimeachana na basi niliyokuja nayo toka Mbeya maana inaendelea na Safari Hadi Mpanda Katavi nami kikazi naelekea tarafa ya KIRANDO hivyo nalazimika kuchukua usafiri mwingine kuelekea huko.
Wakati nasubiri usafiri hapa stendi Kuu Namanyere nimekutana na Stori ya ajabu ambayo sijawahi kuisikia maeneo mengine. Vijana wa Bodaboda na wapiga Debe wanahadithiana Jambo ambalo limefanyika hapa jirani na Stendi usiku wa July 14 kuamkia July 15 siku ambayo Rais Samia alianza ziara Mkoani Rukwa akitokea Katavi.
Kwamba tarehe 14 Julai kwenye kiwanja cha Wazi karibu na Stendi kilifanyika Sherehe iliyobatizwa jina la Mkesha wa Mama ulioandaliwa na viongozi wa Wilaya hii wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya. Katika Mkesha huo wa nje watu walisafirishwa toka Kata zote, kulikuwa na vinywaji vikali na baridi vya kutosha, Muziki wa kukodi, nyama choma ya Mbuzi na Nyamapori na pia waalikwa toka mbali pamoja na Viongozi walilipwa posho na Wageni kulipwa malazi.
Labda wenzangu mnieleze faida ya Aina hii ya mikesha. Yaani Mh. Rais kalala Mpanda, halafu Wananchi wa mkoa mwingine wanakesha wakinywa na kucheza Kwa gharama za serikali? Mh Rais amefika Namanyere akazindua mradi mmoja tu wa Hospitali ya wilaya na akasalimia Wananchi Kwa Muda mfupi Sana. Wengi tuliona maana TBC ilikuwa live. Kwa shughuli hiyo ya nusu saa ya Mh Rais ndo watu wakeshe usiku kucha wakila na kunywa kumsubiri?
Mbona Jambo hili halijafanywa Sumbawanga ambako Rais amelala siku 3 July 15-18?
Hapa hela ya Watanzania imepigwa Kwa Kisingizio cha Mkesha wa kumsubiri Mama.
Hivi ni utamaduni wa kabila gani nchi hii ukisikia kesho mgeni anakuja kwako wewe unalala nje ukila na kulewa na mgeni Huyo kwako anapita tu hata maji hanywi, Maana Mh Rais hakula wala kunywa hapa Namanyere.
TAKUKURU tafadhali, haya ni matumizi mabaya ya fedha za Umma, tunataka kusikia kiasi kilichotumika na kilitoka fungu gani.
Mji hauna maji ya uhakika halafu viongozi wanachukua fedha za Umma kugharamia matukio ya kujineemesha? HAPANA.
Wanakula wenzenu chadema wameshapewa bil. 2.7.
Kodi yenyewe leo umelipa sh ngapi mkuuWana siasa wote dugu moja. Wamekubaliana kula urefu wa kamba zao. Sisi tulipe kodi wao wale kwa urefu wa kamba zao 😂 😂 😂 😎 😎 😎 😎
Nimekunywa kahawa vikombe viwili kwa sh elfu 12. Nina risiti ya kielectronik. Kodi nyingine kubwa nalipa tarehe 20. Halafu mje kulialia haitoshi sababu ya kupigapiga misele na kula na kulaKodi yenyewe leo umelipa sh ngapi mkuu
Kwenye kamati zote huwa wapo hivyo siyo rahisi kujichunguzaWafanye uchunguzi ili wahongwe na wao.