Ziara ya Ernesto Che Guevara Tanzania

Ziara ya Ernesto Che Guevara Tanzania

Kuna habari zinazosema kuwa Che na Castrol walikosana. Castrol akataka Che aondoke Cuba. Hivyo alivyosafiri, Castrol akaandika barua kama vile ni CHE ameandika ili kuwaaga watu wa Cuba kuwa hatarudi tena Cuba.

Hiyo ilipelekea jamaa kuanza kutangatanga hapa na pale. Maada ya kutoka Tanganyika, kuna kila dalili kuwa mipango yake ilikuwa imekaa ovyo na kwa hali ya kawaida, angelitaka kurudi NYUMBANI ambako ilikuwa CUBA. Ila kutokana na barua hiyo, ikawa ameshafungiwa tayari milango. Akaondoka kichwakichwa kuelekea Bolivia ambako hawa Wajinga wakiwa wameshapewa habari kuwa yupo pale kijijini kwao hoi, wakaenda na kumuuwa. Nasikia baadaye walijilaani sana kugunduwa wametumika kumuuwa mtu kama huyo.



aksante mkuu Sikonge ,ila niliwahi kuhudhuria kongomano la maadhimisho kama sikosei ya miaka 40 toka che guevara apite Tanzania lilifanyikia UDSM yalihudhuriwa na wanamapinduzi wengi sana na wanahistoria wengi mpaka balozi wa cuba aliyepigana na che wakati wa mapinduzi hayo na ushuhuda wa kitabu cha yule mwanamapinduzi wa zanzibara anaitwa Babu ila sikuwahi kusikia kitu kama hicho cha kugombana na Fidel.
 
Last edited by a moderator:
mkuu zile zilikua propaganda za wamarekani tu, che na castro hawakukorofishana kama inavyodaiwa. kimsingi che alijiuzulu uwaziri nadhani mwaka 1964 kwa lengo la kuingia vitani kuikomboa latin america na maeneo mengine ya third world. aliondoka cuba kuja tz, then congo akawa haonekani wala hasikiki kule cuba, USA ikaanza kutangaza propaganda kua che ameuawa na castro coz alikua threat kwake kitu ambacho si kweli

ikumbukwe wakati che anaongea kwa mara ya mwisho(siku ile aliyouawa) na yule wakala wa CIA aliyefanikisha kumkamatwa kwake(wakala wa CIA Felix Rodriguez), che alieleza wazi kua ni castro aliyeshauri waanze harakati za ukombozi katika nchi ya Bolivia then waende argentina.

pia ni castro huyo huyo aliyefanikisha kuutafuta, kuupata na kuurudisha nyumbani mwili wa che na macomrade wengine, kazi iliyochukua miaka 30 coz kaburi la che lilikua unspecified

ni castro huyo huyo aliyeanzisha utaratibu kwa wanafunzi wa cuba kuimba nyimbo za kumsifu che kila siku wawapo mstarini(assemble), yeye mwenyewe wala hakuagiza aimbwe au kutukuzwa.

ni castro pia ambaye alivunja mahusiano na Bolivia na kutishia kuivamia kijeshi baada ya kuuawa kwa che.

haya yote yanathibitisha namna gani hawa macomrade walivyopendana




Kuna habari zinazosema kuwa Che na Castrol walikosana. Castrol akataka Che aondoke Cuba. Hivyo alivyosafiri, Castrol akaandika barua kama vile ni CHE ameandika ili kuwaaga watu wa Cuba kuwa hatarudi tena Cuba.

Hiyo ilipelekea jamaa kuanza kutangatanga hapa na pale. Maada ya kutoka Tanganyika, kuna kila dalili kuwa mipango yake ilikuwa imekaa ovyo na kwa hali ya kawaida, angelitaka kurudi NYUMBANI ambako ilikuwa CUBA. Ila kutokana na barua hiyo, ikawa ameshafungiwa tayari milango. Akaondoka kichwakichwa kuelekea Bolivia ambako hawa Wajinga wakiwa wameshapewa habari kuwa yupo pale kijijini kwao hoi, wakaenda na kumuuwa. Nasikia baadaye walijilaani sana kugunduwa wametumika kumuuwa mtu kama huyo.

 
Last edited by a moderator:
Samahani Wakuu, labda nimeandika vibaya au nimeeleweka vibaya.

Kwenye uongozi kila mtu huwa na njia zake anazoona zinafaa kufuata. Baada ya Cuba kuwa chini ya hawa jamaa, Castro alianza kutimiza mipango yake na Che akawa na yake. Hapo ndipo ukatokea mpingano wa mawazo na kila mtu akiwa na wake. Che akaamua kuondoka Cuba na kuendelea kupigana.

Sasa hapa ndiyo habari zinapishana. Wengine wanasema aliandika barua hiyo kwa sababu alikuwa kashapishana na Castro na Castro hakutaka jamaa arudi tena Cuba. Kuna dalili nyingi zinazoonyesha kuwa baada ya kutoka Tanganyika, alitaka sana kurudi Cuba ambako angelijipanga vyema kabla ya kuondoka kwenda Bolivia. Ile safari ya Bolivia ni kweli kuwa alikuwa hajajiandaa vizuri.
Habari ya pili ni kuwa ile barua ya kuaga kuwa hatarudi Cuba, ilikuwa inalengo na kumuweka pembeni Castro na Cuba kama ikitokea kuwa Che amekamatwa. Yaani hata angelikamatwa basi hayo mapinduzi yake au kushindwa kwake kusimuhusishe Catro.

Sasa ukweli ni upi? Ni ngumu kwangu kusema kwa sababu kila sababu inaweza kusimama na kujitetea.

Hivyo Mkuu Voice of Mtwara, nafikiri hapa wala USA tusiingize kwa sababu tunaongelea BARUA ambayo ni kweli ipo. Swali tu hapa ni kuwa: Barua aliiandika kweli Che mwenyewe/alitoa idhini iandikwe au aliandika Castro ili amruke Che ikitokea amekamatwa akipindua nchi? Waligombana au hawakugombana si muhimu sana na hilo linatumika tu kutaka kujua nani aliandika ile BARUA ambayo ni kweli ipo.

Ohh, mwisho ni kuwa hata Castro ni Mwana Siasa tu ambaye kubadilikabadilika ni jambo la kawaida. Alijua sana kucheza karata zake na ndiyo maana hadi leo bado yupo hai pamoja na kuwindwa sana na USA. Ila mwisho wa siku, unagundua kuwa kati ya Che na Castro, kwenye mioyo ya watu, ni CHE bado yupo hai. Castro alilijua hilo na alilitumia sana kisiasa.
aksante mkuu Sikonge ,ila niliwahi kuhudhuria kongomano la maadhimisho kama sikosei ya miaka 40 toka che guevara apite Tanzania lilifanyikia UDSM yalihudhuriwa na wanamapinduzi wengi sana na wanahistoria wengi mpaka balozi wa cuba aliyepigana na che wakati wa mapinduzi hayo na ushuhuda wa kitabu cha yule mwanamapinduzi wa zanzibara anaitwa Babu ila sikuwahi kusikia kitu kama hicho cha kugombana na Fidel.

mkuu zile zilikua propaganda za wamarekani tu, che na castro hawakukorofishana kama inavyodaiwa. kimsingi che alijiuzulu uwaziri nadhani mwaka 1964 kwa lengo la kuingia vitani kuikomboa latin america na maeneo mengine ya third world. aliondoka cuba kuja tz, then congo akawa haonekani wala hasikiki kule cuba, USA ikaanza kutangaza propaganda kua che ameuawa na castro coz alikua threat kwake kitu ambacho si kweli

ikumbukwe wakati che anaongea kwa mara ya mwisho(siku ile aliyouawa) na yule wakala wa CIA aliyefanikisha kumkamatwa kwake(wakala wa CIA Felix Rodriguez), che alieleza wazi kua ni castro aliyeshauri waanze harakati za ukombozi katika nchi ya Bolivia then waende argentina.

pia ni castro huyo huyo aliyefanikisha kuutafuta, kuupata na kuurudisha nyumbani mwili wa che na macomrade wengine, kazi iliyochukua miaka 30 coz kaburi la che lilikua unspecified

ni castro huyo huyo aliyeanzisha utaratibu kwa wanafunzi wa cuba kuimba nyimbo za kumsifu che kila siku wawapo mstarini(assemble), yeye mwenyewe wala hakuagiza aimbwe au kutukuzwa.

ni castro pia ambaye alivunja mahusiano na Bolivia na kutishia kuivamia kijeshi baada ya kuuawa kwa che.

haya yote yanathibitisha namna gani hawa macomrade walivyopendana
 
Sikuwahi kusikia kwamba alifika Tz ingawa alifika Kongo (Zaire) na kusaidia harakati za kivita.

Alifika Tanzania. Alikaa kwenye ubalozi wa Cuba Dar es Salaam kabla ya kwenda DRC Congo. Walisafiri kwa gari toka Dar hadi Kigoma. Wakapita Ziwa Tanganyika kuingia DRC Congo. Baada ya mambo kushindakana kule, alirudi tena Tanzania. Akakaa kwa muda kabla ya kuondoka. Kipindi alichokuwa Congo akisaidia kuleta mapinduzi, kiongozi wa mapinduzi hayo Laurent Kabila alikuwa Dar es Salaam akila bata kama wanavyosema vijana wa leo. Ilikuwa moja ya sababu iliyomkatisha tama mwanamapinduzi huyo!
 
nilichogundua kwenye maelezo yako mkuu sikonge ni kwamba che hakurudi cuba alipotoka tz, ila ukweli wa mambo ni kwamba che alirudi cuba akajipanga kwa muda mfupi then akaondoka na jeshi lake la watu takribani 50 kwenda Bolivia.

kilichomwangusha che kwenye mission ile ni kusalitiwa na chama cha kikomunist cha bolivia ambacho hakikupenda mapambano ya silaha bali siasa, pili ni usaliti wa wanavijiji kule msituni ambako che alikua na vikosi vyake, wanavijiji hawa walivujisha siri kwa majeshi ya serikali kuhusu muelekeo na mienendo ya che na vikosi vyake, hii ilipelekea kuvamiwa mara kwa mara, tatu ni kukatika kwa mtambo wa mawasiliano kati ya che na Havana cuba, hivyo che akakosa msaada wa chakula na vifaa toka Havana




Samahani Wakuu, labda nimeandika vibaya au nimeeleweka vibaya.

Kwenye uongozi kila mtu huwa na njia zake anazoona zinafaa kufuata. Baada ya Cuba kuwa chini ya hawa jamaa, Castro alianza kutimiza mipango yake na Che akawa na yake. Hapo ndipo ukatokea mpingano wa mawazo na kila mtu akiwa na wake. Che akaamua kuondoka Cuba na kuendelea kupigana.

Sasa hapa ndiyo habari zinapishana. Wengine wanasema aliandika barua hiyo kwa sababu alikuwa kashapishana na Castro na Castro hakutaka jamaa arudi tena Cuba. Kuna dalili nyingi zinazoonyesha kuwa baada ya kutoka Tanganyika, alitaka sana kurudi Cuba ambako angelijipanga vyema kabla ya kuondoka kwenda Bolivia. Ile safari ya Bolivia ni kweli kuwa alikuwa hajajiandaa vizuri.
Habari ya pili ni kuwa ile barua ya kuaga kuwa hatarudi Cuba, ilikuwa inalengo na kumuweka pembeni Castro na Cuba kama ikitokea kuwa Che amekamatwa. Yaani hata angelikamatwa basi hayo mapinduzi yake au kushindwa kwake kusimuhusishe Catro.

Sasa ukweli ni upi? Ni ngumu kwangu kusema kwa sababu kila sababu inaweza kusimama na kujitetea.

Hivyo Mkuu Voice of Mtwara, nafikiri hapa wala USA tusiingize kwa sababu tunaongelea BARUA ambayo ni kweli ipo. Swali tu hapa ni kuwa: Barua aliiandika kweli Che mwenyewe/alitoa idhini iandikwe au aliandika Castro ili amruke Che ikitokea amekamatwa akipindua nchi? Waligombana au hawakugombana si muhimu sana na hilo linatumika tu kutaka kujua nani aliandika ile BARUA ambayo ni kweli ipo.

Ohh, mwisho ni kuwa hata Castro ni Mwana Siasa tu ambaye kubadilikabadilika ni jambo la kawaida. Alijua sana kucheza karata zake na ndiyo maana hadi leo bado yupo hai pamoja na kuwindwa sana na USA. Ila mwisho wa siku, unagundua kuwa kati ya Che na Castro, kwenye mioyo ya watu, ni CHE bado yupo hai. Castro alilijua hilo na alilitumia sana kisiasa.
 
Che Guevara[John the Baptist] alifika Kigoma with 100 Cuban Revolutinaries. Lakini alisikitika sana kuona kwamba Waaafrika hawana mwamko wa kisiasa,akaondoka. Alikuja kwa madhumuni ya Kwenda Kongo. Halafu akaenda Bolivia,akauawa,akakatwa kichwa. Alipokuwa Dar es Salaam,nasikia favourite restaurent yake ilikuwa ni Zahir Hotel. Hii Zahir Hotel sijui kama bado ipo. Nimewahi kwenda pale siku moja kula biriyani.
nazidi kuikubali jamiiforums!
 
Ni kweli Che alikuja Tz 1964 akitokea Congo, ni kweli pia wapiganaji wa Congo walimkatisha tamaa kwa sababu kila ikifika jioni ni lazima wapate pombe, muziki na ngono. Lakini wapiganaji hao wa Congo walimpenda sana kutokana na ujasiri na umahiri wake wa mapambano, wakati anawaaga kwenda kwenye mapambano ya Bolivia walimpa kifurushi cha Almasi ili zikamsaidie kwenye mapambano ya Bolivia, lakini alikataa akawaambia "SIKUJA KUFANYA BIASHARA, NIMEKUJA KUPIGANA!" Alipotoka huko alipitia Dar, alikaa siku chache kabla kuelekea Bolivia alikokwenda kuuawa kikatili na CIA ya Marekani. Manowari ya Kimarekani iliegeshwa katika bahari ya Hindi katika fukwe za Tz zikiwa na vifaa maalum vya kumfuatilia nyendo zake ili kumnasa na kumuua, lakini msimamo wa Nyerere ulikuwa pamoja na wapigania uhuru hivyo hakuwapa ushirikiano wamarekani kabisa katika suala hilo (alikuwa kwenye orodha ya magaidi pamoja na kina Nelson Mandela kwa mtazamo wa Marekani) Hivyo Comrade Che Guevara alijisikia nyumbani alipokuwa Dar, hivyo inawezekana kabisa alikwenda kula biriyani pale Zahir Restaurant.
Marekani haikuunga mkono mapambano ya ukombozi dhidi ya Wakoloni, na mpaka leo Marekani haiungi mkono mapambano yoyote ya kujikomboa kiuchumi, hasa kwa nchi ndogo zenye rasilimali nyingi ambazo wao wanazihitaji, watazidumaza kwa misaada na kuwahonga viongozi wake ili zisijitegemee ili zisiwe na maamuzi yake yenyewe juu ya rasilimali hizo, bali maamuzi yawe ni yao wamarekani, ndivyo ilivyo kwetu Tz, hatutakuwa na maamuzi juu ya Gesi wala Urani yetu, hata wananchi wakipinga nguvu za ziada za kijeshi zitatumika dhidi yao, lakini kule South Africa kwa Mzee Madiba hali ni tofauti, viongozi wa Marekani hawapati mapokezi mazuri kutoka kwa wananchi zaidi ya yale ya kiserikali, rasilmali zao wanazipangia wenyewe, hata Obama hawakumshobokea bali waliandamana kupinga ujio wake na walitaka akamatwe na kushtakiwa kwa kukiuka haki za binadamu kunakofanywa na utawala wake sehemu mbalimbali duniani, hata familia ya Mzee Mandela ilimkatalia kwenda kumjulia hali Mzee Mandela hospitalini.
Che Guevara angekuwa hai leo, au kama huko aliko anaweza kutuona tunavyowashobokea Wamerakani, hakika angetulaani na kutuchukia kuliko alivyowachukia wapiganaji wa Congo!
Maelezo yako yanaeza kua na ukweli kwa kiwango fulani, lakini familia ya Mandela sidhani kama imezuia kwenda kwa sababu unazotaka kutuaminisha. Mwaka jana nadhani Michelle alienda kumtembelea Madiba na hata picha zipo kuthibitisha haya. Na hata kitabu cha Mandela cha mwaka 2011 , Conversations with Myself foreword yake ameandika Hussein Onyango, nadhani si vema kuongelea vitu tusivo na uhakika navyo/
 
Zahir Hotel bado ipo.


Shariff Ritz,

Vipi na ile Al Kefak pale Mkunguni Str. nafikiri ilikua zamani ndo inashindana na hiyo Zahir kwa Mishikak,bokoboko/mandi na Sekela Tikka,Nan bread na vikorombwezo vinginevyo vingi mno...

wakti ule Nyerere alikua kafungia takriban kila kitu! Dah! yaani yule mtu alikua muhuni saana!ahaha!!

Nakumbuka sehemu ya Ice Cream ilikua moja tu mji mzima pale Snow Cream,wakti huo Bakhressa maskini hata mitambo ya Ice Cream hajawa nayo!?

Wenzetu Kenya walitutangulia kwa mengi...nakumbuka pale Nairobi zamani mno walikua na ile Malindi Dishes!

Yaani Wana-Mzizima tumetokea mbali mno!ahaha!!

Ahsanta.
 
Shariff Ritz,

Vipi na ile Al Kefak pale Mkunguni Str. nafikiri ilikua zamani ndo inashindana na hiyo Zahir kwa Mishikak,bokoboko/mandi na Sekela Tikka,Nan bread na vikorombwezo vinginevyo vingi mno...

wakti ule Nyerere alikua kafungia takriban kila kitu! Dah! yaani yule mtu alikua muhuni saana!ahaha!!

Nakumbuka sehemu ya Ice Cream ilikua moja tu mji mzima pale Snow Cream,wakti huo Bakhressa maskini hata mitambo ya Ice Cream hajawa nayo!?

Wenzetu Kenya walitutangulia kwa mengi...nakumbuka pale Nairobi zamani mno walikua na ile Malindi Dishes!

Yaani Wana-Mzizima tumetokea mbali mno!ahaha!!

Ahsanta.

Al Habiby gombesugu,

Unanikumbusha mbali sana Al Kefak, hawapo siku hizi kuna Al Uruba, na wenyewe hatari kwa biriyani basmat, Mbuzi, Maziwa ya Ngamia, na Faluda.
 
Last edited by a moderator:
Kuna habari zinazosema kuwa Che na Castrol walikosana. Castrol akataka Che aondoke Cuba. Hivyo alivyosafiri, Castrol akaandika barua kama vile ni CHE ameandika ili kuwaaga watu wa Cuba kuwa hatarudi tena Cuba.

Hiyo ilipelekea jamaa kuanza kutangatanga hapa na pale.
Maada ya kutoka Tanganyika, kuna kila dalili kuwa mipango yake ilikuwa imekaa ovyo na kwa hali ya kawaida, angelitaka kurudi NYUMBANI ambako ilikuwa CUBA. Ila kutokana na barua hiyo, ikawa ameshafungiwa tayari milango. Akaondoka kichwakichwa kuelekea Bolivia ambako hawa Wajinga wakiwa wameshapewa habari kuwa yupo pale kijijini kwao hoi, wakaenda na kumuuwa. Nasikia baadaye walijilaani sana kugunduwa wametumika kumuuwa


mtu kama huyo.



Maelezo yako yana walakin, kwanza Che kwao sio Cuba bali ni Argentina, alienda Cuba kuwasaidia kina Castro kuikomboa Cuba, baada kuikomboa Cuba alipewa uwaziri wa Viwanda na Biashara, wazo la kuwa Waziri wakati nchi nyingine bado zimo kwenye mapambano hakuliafiki, ndipo alipoondoka kwenda kupambana katika nchi nyingine duniani kama vile Vietnam, Cambodia, Congo nk hata kule ambako hakufika kama vile South Africa, Mozambique nk aliwafundisha wapiganaji wao mtindo wake maarufu wa
kupigana wa "Guerrila Warfare" ambao uliwasumbua sana watawala wa kikoloni na ulileta ushindi sehemu nyingi.
 
Last edited by a moderator:
Al Habiby gombesugu,

Unanikumbusha mbali sana Al Kefak, hawapo siku hizi kuna Al Uruba, na wenyewe hatari kwa biriyani basmat, Mbuzi, Maziwa ya Ngamia, na Faluda.



Wallahi,Shariff Ritz...tumetokea mbali mno!ahahaa!

Al Uruba napajua pale,napenda ile mikarangizo yao ya Hargeisa!ahahaa!!...nafikiri ipo Mkunguni Opp. na Chura!?

Naikumbuka ile Ice Cream ya zamani tuko Primary ikiitwa "Chachamao"!ahahaa!

Mimi bakhti nzuri najua mpaka siku hiyo hapo Zahir, Che Guevara alipata Menu ipi!...na alikua na nani.

Ahsanta.
 
Wewe mburula kaa kimya hujui kitu kama babayako; alifika Kigoma ,Tanganyika hakwenda Zenj!!!


Alifika Zanzibar,lakini kwa siri mno...watu walompokea/ma-Comrades wenzie na kumfikisha huko wako hai mpaka kesho hapo hapo D'Salaam...na picha za ukumbusho zipo!

Kama unabisha hili kamuulize Salim Ahmed atakufahamisha uzuri mno!

Cc;Ritz
 
Maelezo yako yanaeza kua na ukweli kwa kiwango fulani, lakini familia ya Mandela sidhani kama imezuia kwenda kwa sababu unazotaka kutuaminisha. Mwaka jana nadhani Michelle alienda kumtembelea Madiba na hata picha zipo kuthibitisha haya. Na hata kitabu cha Mandela cha mwaka 2011 , Conversations with Myself foreword yake ameandika Hussein Onyango, nadhani si vema kuongelea vitu tusivo na
uhakika navyo/

Sikutoa sababu za familia hiyo kumkatalia Obama kumuona Madiba kama alivyotaka, bali nimeunganisha mtiririko wa matukio yanayo indicate kutomuafiki Obama, hata Rais Jacob Zuma hakwenda kumpokea Obama Airport bali alikwenda Waziri wake wa mambo ya nje (ingawa pia inawezekana ikawa ndio protokali yao ya kawaida!)
 
Hata Castro siyo M-Cuba ila ni M-Spain na ndugu zake wa Spain wanafahamika. Baba yake alizaliwa Spain na huko kuhamia tu kwenye mizunguko ya maisha.

Hapa bado tunaongelea ile barua kama ni kweli aliandika au hakuandika. Alikozaliwa au hakuzaliwa siyo muhimu.
Maelezo yako yana walakin, kwanza Che kwao sio Cuba bali ni Argentina, alienda Cuba kuwasaidia kina Castro kuikomboa Cuba, baada kuikomboa Cuba alipewa uwaziri wa Viwanda na Biashara, wazo la kuwa Waziri wakati nchi nyingine bado zimo kwenye mapambano hakuliafiki, ndipo alipoondoka kwenda kupambana katika nchi nyingine duniani kama vile Vietnam, Cambodia, Congo nk hata kule ambako hakufika kama vile South Africa, Mozambique nk aliwafundisha wapiganaji wao mtindo wake maarufu wa
kupigana wa "Guerrila Warfare" ambao uliwasumbua sana watawala wa kikoloni na ulileta ushindi sehemu nyingi.
 
Wallahi,Shariff Ritz...tumetokea mbali mno!ahahaa!

Al Uruba napajua pale,napenda ile mikarangizo yao ya Hargeisa!ahahaa!!...nafikiri ipo Mkunguni Opp. na Chura!
Naikumbuka ile Ice Cream ya zamani tuko Primary ikiitwa "Chachamao"!ahahaa!

Mimi bakhti nzuri najua mpaka siku hiyo hapo Zahir, Che Guevara alipata Menu ipi!...na alikua na nani.

Ahsanta.
Yakhe Gombesugu una taabu kwelikweli weye,
watukumbusha "chachamao" na umri huu?
Je zile "ice cream coco" za senti 10? (ukiwa na senti 5 ile ya tundu au baadae ya samaki unakatiwa nusu!)
Kisha pale Al Kefak nje palichomwa mishkaki ya finyango 3 ambayo ladha yake haipatikani tena sehemu yoyote!
Mkabala na Al Kefak palikuwa na shule yetu ya msingi ikiitwa Mohammadiya Pr Sch kisha ikataifishwa 1967 ikaitwa Jamhuri Pr/ Sch sikuhizi naskia imekuwa Jamhuri Sec/ Sch. Naskia Cameo Cinema haipo tena. Tulikuwa tukiangalia matangazo ya sinema pale Cameo (karibu na Zahir) wenzetu wakatuambia kuna Wacuba wanajichana hapo Zahir, tukaenda tukajifanya tumekwenda kunywa maji (si unajua maji yalikuwa ni bure na haikatazwi) ndipo tukamwona tunaedhani alikuwa Che Guevara na wenzake kama watatu hivi na waswahili wawili, walikuja na Landrover 109 (macho ndani) ya kijivu, walikaa meza ya kushoto kabisa ukiingia mlangoni. Hatukumjua kwa wakati ule bali
tuliposikia habari zake baadae tukahisi atakuwa ni yeye, ndio maana nikasema inawezekana kabisa alikuwa akienda Zahir Restaurant kula biriyani na ile mikate ya ufuta!
Lakini sasa wewe Gombesugu mbona sikuhizi lile Gombesugu lenyewe original linalopigwa pamoja na exhaust pipe ya Leyland Albion skuizi halipigwi tena? Twaona michiriku na minanda tu?
 
Hata Castro siyo M-Cuba ila ni M-Spain na ndugu zake wa Spain wanafahamika. Baba yake alizaliwa Spain na huko kuhamia tu kwenye mizunguko ya maisha.

Hapa bado tunaongelea ile barua kama ni kweli aliandika au hakuandika. Alikozaliwa au hakuzaliwa siyo muhimu.


Sikonge,

Niwie radhi ndugu yangu kuingilia kiduchu haya majadiliano yenu.

Nafikiri hivyo unavyomtaka jamaa akujibu,nakhis utakuwa kama vile "unamuonea"!?

Maana hiyo barua hata kama "aliandika"/hypothetical....lakini tunajua kabisa;kutokana yakuwa zile harakati zao ziliambatana na fitna,ugaidi,ujasusi na uzandiki mwingi mno...kwa hiyo itakua ngumu mno pia kupata authenticity ya hiyo barua!?

Maana hata ikiwepo hiyo barua,au hata "ushahidi" ukiwepo kuwa kweli aliandika na labda wanae au Serikali ya Cuba "wakathibitisha"...bado pia itakua haitoshi kuwa ati ndo uthibitisho wa kukubalika kitaaluma.

Kumbuka wakti huo ilikua ni Cold War...nchi nyingi khasa za Eastern Block ndo zilikua zinaongoza kwa forgery ya kila kitu na kila aina,khasa Stassi.

Na upande mwingine kuna maharamia wa Western World waliokua wakiongozwa na CIA,MOSSAD,MI6 na wengineo wengi mno.

Khalaf pia kulikua na zile local/internal politics za pale Habana...ambazo nazo pia zilikua very complex khasa wakti ule.

Inasemekana huyo Che,hakuwahi kuamini mtu yeyote hata vimada zake/Mke wake!?...

Pia tunajua wakti aliokua na mikwaruzano kiduchu na Castro,yakuwa Family yake ilikua chini ya fadhila na instructions takriban zoote toka kwa kina Castro/Serikalini!?

Kwa kifupi,ingekua/ itakua ni vigumu hivi leo hii, kwa Wanataaluma au watu wenye akili zao timamu kuamini hata kile watakachokhadith au kuonyeshwa na hata hiyo family ya Che Guevara mwenyewe bila ya kujiuliza motive/s zao!?

Niwie radhi kwa hayo maelekezo yangu kiduchu,nataraji msamaha wako kama kuna lolote labda unakhis sifahamu au nimekukera!?

Ahsanta.

Cc;MgungaMiba
 
Hata Castro siyo M-Cuba ila ni M-Spain na ndugu zake wa Spain wanafahamika. Baba yake alizaliwa Spain na huko kuhamia tu kwenye mizunguko ya maisha.

Hapa bado tunaongelea ile barua kama ni kweli aliandika au hakuandika. Alikozaliwa au hakuzaliwa siyo muhimu.
Barua ni barua tu, inawezekana aliiandika au hakuiandika, lakini hakuna dalili kwamba walikosana na Castro kama ambavyo CIA walitaka kuuaminisha ulimwengu, kwani base yake ya operation ilikuwa ni Cuba, hata alipokuwa Tz alifikizia ubalozi wa Cuba, Hata wakati anaenda Bolivia, alifikia kwanza Cuba kisha ndio akaelekea Bolivia, kule alikuwa akitumia mawasiliano ya Radio call kuwasiliana na Cuba, CIA kwa kutumia mitambo yao waliintercept kisha kudisrupt mawasiliano hayo na kufanikisha kumkamata kwa kutumia vibaraka. Sasa huo ugomvi na Castro umetokea wapu?
 
Back
Top Bottom