Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa Rose Tweve ameendelea na ziara yake katika Wilaya ya Mufindi, Kata ya Saohill ambapo ameshiriki kikao cha Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Upendo, Mufindi.
Ziara hiyo ni muendelezo wa kazi za Mbunge Tweve maeneo mbalimbali Mkoa wa Iringa kukagua shughuli za maendeleo na mikopo iliyotolewa kwenye vikundi vya wanawake.
Tweve amesema, Mwaka 2025 Rais ni Samia na wanawake wote wa Mufindi waendelee kuyasemea mema ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoyafanya Mufindi, Saohill.
Katibu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Saohill Wilaya ya Mufindi, Ndugu Rebecca Laurent Mwambusi amefurahishwa na utendaji wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa Shule ya Kata ya Saohill.
Ndugu Rebecca amesema, Rais Samia Suluhu Hassan amemtua ndoo kichwani mwanamke wa Kata ya Saohill kwani kwa sasa maji ni burudani katika Kata ya Saohill.
Ndugu Rebecca amesema kwa sasa Mbole inapatikana kwa bei nafuu, Elimu imeboreshwa katika Kata ya Saohill na Wilaya nzima ya Mufindi.
Ndugu Rebecca amesema wanawake wa Kata ya Saohill wanamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan na kuahidi kuwa mwaka 2025 watu wote wa Kata ya Saohill na Wana Mufindi wote kura za ushindi ni kwa Rais Samia Suluhu Hassan.
UWT Jeshi Imara
#KaziIendelee
Ziara hiyo ni muendelezo wa kazi za Mbunge Tweve maeneo mbalimbali Mkoa wa Iringa kukagua shughuli za maendeleo na mikopo iliyotolewa kwenye vikundi vya wanawake.
Tweve amesema, Mwaka 2025 Rais ni Samia na wanawake wote wa Mufindi waendelee kuyasemea mema ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoyafanya Mufindi, Saohill.
Katibu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Saohill Wilaya ya Mufindi, Ndugu Rebecca Laurent Mwambusi amefurahishwa na utendaji wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa Shule ya Kata ya Saohill.
Ndugu Rebecca amesema, Rais Samia Suluhu Hassan amemtua ndoo kichwani mwanamke wa Kata ya Saohill kwani kwa sasa maji ni burudani katika Kata ya Saohill.
Ndugu Rebecca amesema kwa sasa Mbole inapatikana kwa bei nafuu, Elimu imeboreshwa katika Kata ya Saohill na Wilaya nzima ya Mufindi.
Ndugu Rebecca amesema wanawake wa Kata ya Saohill wanamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan na kuahidi kuwa mwaka 2025 watu wote wa Kata ya Saohill na Wana Mufindi wote kura za ushindi ni kwa Rais Samia Suluhu Hassan.
UWT Jeshi Imara
#KaziIendelee