Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
ZIARA YA SIKU YA KWANZA TARAFA YA SUBA KATA NYAMUNGA KIJIJI CHA MKENGWA
Leo tarehe 03/07/2025, Mh Mbunge kaanza ziara tarafa ya Suba kwa kuzungumza na wananchi wa kijiji cha mkengwa juu ya agenda tatu:-
1. Uchaguzi wa Seriakali za vijiji na vitongoji
2. kujiandikisha daftari la kudumu la mpiga kura.
3. Kuelezea ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi.
Mh mbunge amezungumzia juu Shule ya msingi mpya iliyojengwa Mkengwa ya zaidi ya 540mil wakati wa kipindi chake cha ubunge.
Kazungumzia juu ya Shule ya Sekondari mpya iliyojengwa Mkengwa ndani ya miaka mitatu yeye akiwa kama mwasisi wa shule hiyo, na kwa sasa shule hiyo inatumika kwa kuwapunguzia adha ya watoto kusafiri zaidi ya 20km kwenda Nyamunga Sec na kusababisha watoto wa kike kutomaliza masomo yao kwa sababu ya umbali.
Ziara ya Mh Mbunge inaendelea na kesho atakuwa tarafa ya Girango kata ya Ikoma akiambatana na madiwani wa jimbo la Rorya na viongozi mbali mbali wa chama.
Imetolewa
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Rorya
#maendeleokwanza
03/07/2024.