Ziara za Waziri Mkuu zinanitia mashaka, hasa ile ya Mwendokasi

Ziara za Waziri Mkuu zinanitia mashaka, hasa ile ya Mwendokasi

LICHADI

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2015
Posts
4,491
Reaction score
12,560
Kiukweli kati ya viongozi ambao siwaamini wa kwanza ni Mhe Majaliwa, kwa nini nasema hivi...

Miezi miwili iliyopita alifanya ziara pale Mwendokasi akakuta hali ni mbaya magari yamekufa pesa zinaibiwa, watu wanabanana kwenye magari yaani alikuta hali mbaya ila cha kushangaza ni miezi miwili sasa hali ipo vile vile.

Kumbukeni tulishawahi kuambiwa kuwa pale bandarini kuna basi za kutosha tu zimekaa pale zilizuiwa muda sana, sasa najiuliza kama waziri mkuu aliona hali ni mbaya pale alishimdwa vipi kuamuru gari zitoke bandarini zije ziondoe shida ya wananchi then hiyo kodi wangelipana tu maana mradi wa mwendokasi una pesa nyingi tu njia haina mpinzani ni ngumu kukosa kodi ya kukomboa magari bandarini.

Matokeo yake waziri mkuu kafanya ziara na kupotea miezi miwili sasa hakuna mabadiliko yoyote pale shida iko vile vile

Hizi ziara za waziri mkuu zinatusaidieje?

Au zipo kisiasa zaidi, nawasilisha
 
Usimlaumu kondakta wakati dereva yupo. Kweli PM si PM tunayemfahamu; na hii inatokana na sera ya dereva mwenyewe Bi Mkubwa aliwaambia sasa hivi mwendo ni kubembeleza na kulemba mwandiko. ^Fanya kama unapiga biti kidogo, lakini ruhusini raia wajiachie wenyewe^
 
Mambo yamebadilika mkuu,tz ya Sasa sio ya enz zile,naamini wazr ukionana nae chemba atakwambia ,natamani nichukue maamuz fulani lkn shda ni aliyepewa ulidhi wa familia anazingua.vumilieni hivyo hivyo ,hakuna namna!
 
Mambo yamebadilika mkuu,tz ya Sasa sio ya enz zile,naamini wazr ukionana nae chemba atakwambia ,natamani nichukue maamuz fulani lkn shda ni aliyepewa ulidhi wa familia anazingua.vumilieni hivyo hivyo ,hakuna namna!
Daah...
 
Back
Top Bottom