Zifahamu mbinu wanazotumia Mataifa makubwa kufanikiwa

Zifahamu mbinu wanazotumia Mataifa makubwa kufanikiwa

Mr Why

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2019
Posts
2,235
Reaction score
4,252
Ndugu zangu tunapozungumzia Mataifa makubwa tunawalenga Marekani, Ujerumani, Wiingereza, Japan, China, Korea nakadhalika.

Haya ni mataifa makubwa yalifanikiwa tangu zamani na wakati mwingine mataifa mengine yanajiuliza ni mbinu gani wanazotumia kufanikiwa.

Jambo la kushangaza ni kuwa mbinu wanazotumia kufanikiwa sio nyingi ni chache sana ikiwemo kuchagua viongozi wenye akili kubwa wanaochukia ujinga.

Haya mataifa huwa hayachagui viongozi wajinga, wavivu, wenye tamaa, masikini, wanaokumbatia ufisaidi, wasio na maono ya Taifa, vichaa kwa vyovyote vile ilimradi viongozi wa hovyo.

Hivi vigezo huwa wanakuwa makini kuhakikisha kuwa hao viongozi wanaochaguliwa hawana kasoro hizo kwasababu wanafahamu madhara ya viongozi wajinga huwa wanasababisha matatizo kwa wananchi wao.

Sifa ya kwanza kabisa watatazama elimu yao ni ya kiwango gani, uerevu wao, hali yao ya kiuchumi, wanaothamini utu, ukakamavu na ndio maana viongozi ni lazima wawe wamefuzu mafunzo ya jeshi, viongozi wanaochukia ujinga, tamaa, wenye maono ya Taifa lao.

Viongozi wa Mataifa hayo makubwa wakishakuwa na vigezo hivi basi wataongoza Taifa hilo na wataleta mafanikio makubwa sana kwa Wananchi wao ndio maana tunaona Marekani, Ujerumani, Wiingereza, Japan, China wakipiga hatua kwa kiasi kikubwa.

Wananchi wa Taifa lolote wanapaswa kutambua kuwa viongozi wajinga huleta matatizo kwa wanachi wao, hivyo basi wachague viongozi werevu, wanaochukia ujinga, wenye elimu kubwa, wanaothamini utu na wenye maono kwa Taifa lao ili matatizo ya Wananchi yapungue ama kukoma kabisa.
 
Msitupie lawama viongozi pekee hapa kwetu. Wananchi pia wanachangia saaana. Mtu anapewa wadhifa basi kitu cha kwanza anafikiria ni deals atakazo piga hapo mpaka taasisi ife. Uvivu, kutojituma, ulevi, ngono za nje nk ndio vipaumbele.
Hata ukikuta mtu ana Phd bado hamnazo.
 
Msitupie lawama viongozi pekee hapa kwetu. Wananchi pia wanachangia saaana. Mtu anapewa wadhifa basi kitu cha kwanza anafikiria ni deals atakazo piga hapo mpaka taasisi ife. Uvivu, kutojituma, ulevi, ngono za nje nk ndio vipaumbele.
Hata ukikuta mtu ana Phd bado hamnazo.
Swala la uongozi ni tatizo ndugu kwa hali hii hatutafika.
 
Kama viongozi wetu ni wajinga ina maana jamii yetu ni wajinga pia maana wametoka miongoni mwetu.

Mtu hadi kuwa kiongozi ina maana kapita changamoto zote hadi kutoboa, in short ndo mwenye akili kati yenu ndo maana anawaongoza.

Kama unajua Juma hajui kuendesha gari utakubali akuendeshe? Ukikubali hapo nani mjinga wewe au yeye? It comes down to that.
 
Nishasema humu kua.. Tanzania haiwezekan kupata maendeleo na kukuza uchumi, hii ni kwasababu adui mkubwa wa maendeleo na ukuzaj wa uchumi ni UFISADI, WIZI, UBADHIRIFU, UHUJUM WA RASILIMALI ZA TAIFA!! Vitu ambavyo kwa tz vipo activated na huez chukuliwa hatua!
 
Nishasema humu kua.. Tanzania haiwezekan kupata maendeleo na kukuza uchumi, hii ni kwasababu adui mkubwa wa maendeleo na ukuzaj wa uchumi ni UFISADI, WIZI, UBADHIRIFU, UHUJUM WA RASILIMALI ZA TAIFA!! Vitu ambavyo kwa tz vipo activated na huez chukuliwa hatua!!
Ndugu yangu hii laana ndiyo inayotafuna hili Taifa
Kila Mwananchi azingatie kuwa asipokuwa makini kuchagua Kiongozi mwenye sifa zinazotakiwa basi yeye ndiye atateseka badae
 
Back
Top Bottom