Zijue baadhi ya koo za Kizaramo, asili na maana yake

Zijue baadhi ya koo za Kizaramo, asili na maana yake

Inawezekana kwa sababu kwa kawaida watu wengi wa bara( wabara, ni neno la kiluguru/zaramo/kwere maana yake wa kuja, au asiye na asili na makabila ya pwani), walipokuja mikoa ya moro, pwani na dar ( jimbo la mashariki) waliweza kulowea na kuoa au kuolewa na kushindwa kurudi makwao ( mikoa ya tabora, mwanza, kigoma n.k) kwa hiyo wakafahamiana na watu wa pwani na wakahesabiwa kuwa miongoni mwa makabila haya ya pwani, kwa mfano leo hii kuna majina ya kina mganga uluguruni, ambayo kiasili ni kina maganga wa tabora. Kwahiyo kuna wa manyema, wanyamwezi, warundi,wakongo na makabila mengine mengi yaliyokuja pwani kama manamba au watumwa au wafanyabiashara, wakaishi kuoa na kuolewa na watu wa pwani na kizazi chao kikasahau asili ya kwao na kujitambulisha kama wazaramu au wakwere au waluguru. Yaani wamekuwa wazaramu kwa kuzaliwa au kutokujua asili ya kwao, ila chimbuko halisi la wazaramo ni uluguruni,na uziguani.Kwahiyo hao wa manyema walikuja na kuwakuta wenyeji ambao ni wazaramu,waluguru,wakwere,wandengereko, wakami, wakutu na wakakaribishwa na kuwa miongoni mwao, pia vizazi vyao vilijitanabaisha kama wazaramo. Kwahiyo wakawa wazaramu wa kuzaliwa….! Kimsingi hata mngoni ambaye atahamia ngerengere au tununguo au mlandizi, vizazi vyake baadaye vinaweza kujitambulisha kama kutoka kabila la wakwere/waluguru. Kwahiyo uhusiano ulipo ni kwamba, wa manyema walihamia maeneo ya pwani na kutekwa na utamaduni wa wenyeji, na kuwa wazaramu ila wazaramu si wa manyema na wala wa manyea si wazaramu.
Shukran

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wanao tokea upande wa morogoro ni waongeaji sana kumbe zao moja na wapwani,waluguru+wandengereko,+wazaramo
 
Mhh, ahsante
Nimevutiwa na ukoo namba 5, ule wa chuma kimejilegeza na majina yao kwa jinsia. Nzuri
 
Inawezekana kwa sababu kwa kawaida watu wengi wa bara( wabara, ni neno la kiluguru/zaramo/kwere maana yake wa kuja, au asiye na asili na makabila ya pwani), walipokuja mikoa ya moro, pwani na dar ( jimbo la mashariki) waliweza kulowea na kuoa au kuolewa na kushindwa kurudi makwao ( mikoa ya tabora, mwanza, kigoma n.k) kwa hiyo wakafahamiana na watu wa pwani na wakahesabiwa kuwa miongoni mwa makabila haya ya pwani, kwa mfano leo hii kuna majina ya kina mganga uluguruni, ambayo kiasili ni kina maganga wa tabora. Kwahiyo kuna wa manyema, wanyamwezi, warundi,wakongo na makabila mengine mengi yaliyokuja pwani kama manamba au watumwa au wafanyabiashara, wakaishi kuoa na kuolewa na watu wa pwani na kizazi chao kikasahau asili ya kwao na kujitambulisha kama wazaramu au wakwere au waluguru. Yaani wamekuwa wazaramu kwa kuzaliwa au kutokujua asili ya kwao, ila chimbuko halisi la wazaramo ni uluguruni,na uziguani.Kwahiyo hao wa manyema walikuja na kuwakuta wenyeji ambao ni wazaramu,waluguru,wakwere,wandengereko, wakami, wakutu na wakakaribishwa na kuwa miongoni mwao, pia vizazi vyao vilijitanabaisha kama wazaramo. Kwahiyo wakawa wazaramu wa kuzaliwa….! Kimsingi hata mngoni ambaye atahamia ngerengere au tununguo au mlandizi, vizazi vyake baadaye vinaweza kujitambulisha kama kutoka kabila la wakwere/waluguru. Kwahiyo uhusiano ulipo ni kwamba, wa manyema walihamia maeneo ya pwani na kutekwa na utamaduni wa wenyeji, na kuwa wazaramu ila wazaramu si wa manyema na wala wa manyea si wazaramu.


Kuna wadoe....ni wanyamwezi hao
walikuja kupigana..wanaitwa wadoe kwa maana ya kudoea
walikuwa wanadoea kwa wazaramo
 
Kumbe ndio maana hata lugha wanasikiana kati ya waluguru, wakwere na wazaramo
 
Kuna wadoe....ni wanyamwezi hao
walikuja kupigana..wanaitwa wadoe kwa maana ya kudoea
walikuwa wanadoea kwa wazaramo
okayy..shukrani mkuu kwa maelezo, nitaifanyia kazi historia yao nikirudi dutumi...
 
Mkuu Bwana Banzi asante kwa historia hii mujarabu. Umenikumbusha zamani sana marehemu bibi alivyonihadithia kwamba zamani hali ilipokuwa ngumu walienda Kolelo kwenye mizimu yao kuomba wakitokea Pwani au Dar es salaam. Ebu nipe historia hili koo za Hongo,Shomvi,Kawambwa na Kinyamkera kama una habari zake. Maana naona linatumika kwa Waluguru na Wazaramo
 
Mkuu Bwana Banzi asante kwa historia hii mujarabu. Umenikumbusha zamani sana marehemu bibi alivyonihadithia kwamba zamani hali ilipokuwa ngumu walienda Kolelo kwenye mizimu yao kuomba wakitokea Pwani au Dar es salaam. Ebu nipe historia hili koo za Hongo,Shomvi,Kawambwa na Kinyamkera kama una habari zake. Maana naona linatumika kwa Waluguru na Wazaramo
sawa mkuu, nitajaribu kufuatilia nijue historia kwa undani...ahsante kwa nyongeza
 
Hahaaa hata warangi na wajita wanaongea haraka.Uharaka katika lugha ulioimaster inategemea na lugha yako ya kwanza.Kama lugha yako ya awali iko slow pia itaathiri lugha ya pili.
 
Wazaramo nawakubali sana kwa kuongea.
 
Back
Top Bottom