Zijue fursa zinazopatikana Handeni mkoani Tanga ambazo zitakufanya uwe tajiri kwa muongo mmoja tu

Zijue fursa zinazopatikana Handeni mkoani Tanga ambazo zitakufanya uwe tajiri kwa muongo mmoja tu

Kazanazo

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2023
Posts
2,582
Reaction score
4,554
Nchi hii imejaa utajiri kila mahali leo nitakujuza fursa mbalimbali zinazopatikana Handeni mkoani Tanga

1. Uuzaji wa magogo na Mbao
Hii ni moja ya biashara kubwa sana itakayokuingizia kipato kikubwa kwa muda mfupi sana ilimradi uwe full kwenye vibali vya maliasili ili usisumbuane nao

Misitu mingi ni misitu asili ambayo serikali huzuia ukataji miti ovyo kwahiyo ukija na mbadala wa miti ya mbao utapiga pesa nyingi sana kwani karibia 60% ya wakaazi wa mji huo ni mafundi selemala

2. Umiliki wa machine za kuranda na kuchana mbao
Kama unaijua keko ya Dar es salaam ilivyo basi nenda Handeni, hasa maeneo ya Mkata, kabuku na Handeni mjini

Ukiweza kumiliki mitambo ya uchanaji mbao na ukaweza kupiga kazi usiku na mchana utapiga pesa ndefu sana. Wengi wanafanyaga kazi usiku kuogopa maliasili kwahiyo lazima uwe popo ili kupata wateja wa uhakika

3. Kama una uhakika wa soko la fernitures kawekeze kwa mafundi wadogo wadogo
Watakutengenezea ferniture nzuri kwa bei rahisi sana kisha ukauza kwa bei itakayokupa faida kubwa. Ukiwa wewe ndio boss wao watakutengenezea na kukupa ukauze ukija unawakatia chao cha muhimu uaminifu tu

4. Kuuza mbuzi wa kuchinja au kuwauzia wachinjaji
Hii ni biashara kubwa sana hasa maeneo ya mkata, aisee wajomba ni wanakula mbuzi balaa na wengine na vigari vyao vya laki mbili ni wanabeba kuja nazo mjini hii itakufanya uwe tajiri bila wewe mwenyewe kujua

5. Hardware au duka la vifaa jenzi
Miji kama mkata, kabuku, segera, Handeni mjini, Kilindi n.k inakua kwa kasi sana. Watu wanafumua mijengo ya maana ukiweza kuwa na hardware ya kuaminika na ukazoeleka haraka utapiga mpunga wa maana kwa muda mchache sana

Kwa leo nitaishia hapo tukutane part two kwa wale wenye vimitaji vya kuunga unga kama mimi

Part two
Kama hujaona fursa Handeni acha nikujuze, acha kuamini mazingahombwe wekeza na ufanye biashara kwa ukubwa upate pesa utoke kwenye umasikini. Kwa wenye mitaji midogo fursa ni kama zifuatazo

6. Kuuza kuku na mbuzi wa kuchoma na kukaanga

Hii biashara ukiifanya kwa weledi na ukaacha uvivu kwa siku waweza funga na 50k faida kwa mtaji mdogo tu. Uzuri wauza mbuzi pia wanakopesha ukishauza unawapa chao ukienda nao fuleshi

7. Kuuza kuku wazima

Hawa wanatoka mashambani ukiwa mzoefu hutakuwa na ulazima wa kuwafuata huko mashambani unatega tu njiani wanakuja na wakulima. Utanunua kwa bei ndogo kabisa na kuuza kwa bei kubwa

8. Kuuza maji kwenye matoroli au ukiweza unachimba kisima

Ukiweza kuchimba kisima ndio vizuri, utaagiza maji kwenye magari halafu unauza kwa dumu au ndoo. Handeni maji ni shida sana ukiwekeza vizuri kwenye supply ya maji utatoboa haraka

9. Kama una kigari cha mkopo kifanye tax au bolt

Hii kitu bado ngeni ukiwa muanzilishi utaokota hela za bure. Maeneo kama Mkata na Handeni mjini kuna vibosile wengi sana na mishangazi huwezi kukosa 50k per day

10. Fanya umachinga wa bidhaa ndogo ndogo

Ukiachana na usajili wa laini hii fursa wengi bado hawajaiona, ukifanya kama wafanyavyo dar na majiji mengine makubwa ya kutembeza vitu mbalimbali (umachinga) utapiga hela sana watu wengi siku hizi ni wavivu kwenda dukani au sokoni

Karibu mwana Handeni mwenzangu uongezee fursa wadau wapate kusaidika
 

Attachments

  • Screenshot_20241027-133918_1.jpg
    Screenshot_20241027-133918_1.jpg
    223.2 KB · Views: 13
Kule shida ni uchawi/ushirikina Aiseeh! Hayo maeneo ni komesha!

Labda hiyo Biashara ya Mbuzi ndo imekaa vizur sana maana unawatoa huko unawaleta mjini! Pia biashara ya kuku kuleta mjini! Lakini kusema ufanyie biashara au ufungue huko huko Aiseeh ni changamoto sana (uchawi/ushirikina)
 
Kule shida ni uchawi/ushirikina Aiseeh! Hayo maeneo ni komesha!

Labda hiyo Biashara ya Mbuzi ndo imekaa vizur sana maana unawatoa huko unawaleta mjini! Pia biashara ya kuku kuleta mjini! Lakini kusema ufanyie biashara au ufungue huko huko Aiseeh ni changamoto sana (uchawi/ushirikina)
Mkuu mbuzi hata ukiuzia kule kule zinaenda balaa ile barabara ni kubwa watu kutoka mombasa pia wanapita pale wananunua mbuzi

Huo uchawi ni visa kale hivyo acha kuvipa muda kawekeze utoke kwenye umasikini
 
Mkuu mbuzi hata ukiuzia kule kule zinaenda balaa ile barabara ni kubwa watu kutoka mombasa pia wanapita pale wananunua mbuzi

Huo uchawi ni visa kale hivyo acha kuvipa muda kawekeze utoke kwenye umasikini
Biashara niliyoplani tokea Tanga ni hiyo ya Kuku na Mbuzi!
 
Handeni hii au handeni nyingine na magogo zamani ndio yalikua dili lakini siku hizi kipengele jela nje nje
 
Ukiskia handeni kinachofuata kuskia ni ushirikina. Na wazee wetu walishatuambia ni vigumu sana kupata pesa sehemu ambayo ushirikina umeshamiri.
Hizo ni ngano tu kama tulivyoaminishwa wahehe wanakula mbwa na kujinyonga

Mkuu kwenye pesa fikra potofu weka pembeni
 
Handeni hii au handeni nyingine na magogo zamani ndio yalikua dili lakini siku hizi kipengele jela nje nje
Wengi hawafuati sheria ila ukifuata sheria na ukakata vibali utafanya biashara kwa uhuru kabisa
 
Kama una weza wekeza kwenye afya pia mfano zahanati, kituo cha afya au hospital kabisa! Hizi ndo zina hela maana vituo vya afya vya serikali wanatoa huduma mbovu mno! Nina pharmacy kwenye moja ya kijiji cha handeni kila siku wateja wananiambia nifungue hospital maana wamechoka na mateso ya vituo vya afya vya serikali🤣! Kuhusu uchwawi hayo ni maneno tu(stereotype) watu tunapiga hela fresh tu! Cha maana huku uwe na nidhamu kwa wateja wako basi unawin💵
 
Kama una weza wekeza kwenye afya pia mfano zahanati, kituo cha afya au hospital kabisa! Hizi ndo zina hela maana vituo vya afya vya serikali wanatoa huduma mbovu mno! Nina pharmacy kwenye moja ya kijiji cha handeni kila siku wateja wananiambia nifungue hospital maana wamechoka na mateso ya vituo vya afya vya serikali🤣! Kuhusu uchwawi hayo ni maneno tu(stereotype) watu tunapiga hela fresh tu! Cha maana huku uwe na nidhamu kwa wateja wako basi unawin💵
Hongera sana mkuu nina imani ukiwa na nidham nzuri utatoka na kitu kijijini hapo, Handeni ni wilaya yenye watu wengi sana wazigua wanazaliana kama utitili ukiwekeza lazima upige pesa

Halafu mimi nashangaa sana na zama hizi vijana wameelimika ila bado wanaamini mazingahombwe sijui shida iko wapi au mfumo wa elimu yetu uko chini sana?
 
Hongera sana mkuu nina imani ukiwa na nidham nzuri utatoka na kitu kijijini hapo, Handeni ni wilaya yenye watu wengi sana wazigua wanazaliana kama utitili ukiwekeza lazima upige pesa

Halafu mimi nashangaa sana na zama hizi vijana wameelimika ila bado wanaamini mazingahombwe sijui shida iko wapi au mfumo wa elimu yetu uko chini sana?
Bado watu wana imani za kizamani sana!
 
Back
Top Bottom