Zijue namba za Magari na maana zake

Zijue namba za Magari na maana zake

STK= Serikali ya Tanzania>gari toleo K
STN=Serikali ya Tanzania >gari toleo N(this is the current number plate)
SU=Shirika la umma mfano Tanesco, Dawasco, TRA
STL=Serikali ya Tanzania >gari toleo L
STM=Serikali ya Tanzania>gari toleo M
DFP=Donated Fund Project, hzi ni gari znatolewa nawafadhili wa miradi mbalimbali
DFPA=Donated Fund Project >gari toleo A
SM=Serikali za Mitaa
Safi👏👏👏👏
 
STK= Serikali ya Tanzania>gari toleo K
STN=Serikali ya Tanzania >gari toleo N(this is the current number plate)
SU=Shirika la umma mfano Tanesco, Dawasco, TRA
STL=Serikali ya Tanzania >gari toleo L
STM=Serikali ya Tanzania>gari toleo M
DFP=Donated Fund Project, hzi ni gari znatolewa nawafadhili wa miradi mbalimbali
DFPA=Donated Fund Project >gari toleo A
SM=Serikali za Mitaa
Asee nimeelewa vizuri.
STN naona ndio ma 300 serious mengi yana hizo namba sababu mapya nadhani. STK nyingi zilikuwa na zimo kwenye kilimo kwanza.
 
ST-Serikali ya Tanzania

Zilikuwepo STH, STJ, STK, STM na sasa ni STN haya ni matoleo tu upande wa serikali

Kama ilivyo kwa magari binafsi kuna namba A mpaka sasa ya karibuni ni E na serikalini ya karibuni ni STN
 
ST-Serikali ya Tanzania

Zikikuwepo STH, STJ, STK, STM na sasa ni STN haya ni matoleo tu upande wa serikali

Kama ilivyo kwa magari binafsi kuna namba A mpaka sasa ya karibuni ni E na serikalini ya karibuni ni STN
Shukhran kiongoz✅
 
1:Namba za Magari Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu
Namba za magari yanayitumika kumbeba Rais au Makamu wa Rais na Waziri Mkuu haziandikwi namba wale herufi katika kibao chake, bali huwa na nembo ya taifa ya Bwana na Bibi. Kwa Kiingereza magari haya hufahamika kama State Cars.

2. Spika wa Bunge la Tanzania na Naibu wake
Spika wa Bunge pia gari lake huwa halina namba kwenye kibao chake bali huwa na herufi S pekee. Gari la Naibu Spika nalo huwa na herufi NS pekee. Maana ya herufi S ni Spika na NS ni Naibu Spika.

3. Katibu Mkuu Kiongozi
Katibu Mkuu Kiongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatumia gari ambalo lina kibandiko chenye herufi CS pekee. Ikiwa maana ya CS ni Chief secretary

4. Jaji Mkuu wa Tanzania
Gari la Jaji Mkuu wa Tanzania huwa na herufi JM kwenye kibao chake

5. Mkuu wa Majeshi (CDF)
Gari la Mkuu wa Majeshi wa Tanzania katika kibao chake huwa hakuna namba wala herufi zozote bali kunakuwepo na Nyota nne kwenye kibao cha gari lake.

6. Waziri na Naibu Waziri wa Wizara mbalimbali
Magari ya Waziri na Manaibu wao huwa na herufi zinazoonyesha cheo (kama ni waziri au Naibu waziri) halafu hufuatia ana vifupisho vya majina ya Wizara zao. Gari la Waziri huwa na herufi W ikifuatia na kifupisho cha jina la Wizara yake. Gari la Naibu waziri huwa na herufi NW ikifuatiwa na kifupisho cha jina la Wizara yake

7. Gari za Serikali za Mitaa
Magari ya Serikali za Mitaa, yanayotumiwa kwenye Serikali hizo. Magari hayo kuwa na kibao chenye Herufi SM zikifuatiwa na namba tofauti tofauti.

8. Magari ya Shirika la Umoja wa Mataifa
Kibao hiki kinabeba maana kuwa gari husika linamilikiwa na moja ya shirika la umoja wa mataifa. Mfano shirika la Afya Duniani (WHO). Kibao chenye namba inayoanza na herufi T kufuatiwa na namba na herufi CD kisha namba tena.

9. Magari ya balozini Mbalimbali nchi Tanzania
Magari ya Ubalozi nchini Tanzania huanziwa na herufi T kufuatiwa na namba na kisha herufi CD kisha namba. Pia namba hizi hutumiwa na wafanyakazi wa ubalozi husika hata kama ni watanzania. Mfano wa Ubalozi ni Marekani

10. Shirika la Umma. Mfano; TANESCO, EWURA
Magari yanayotumiwa na mashirika ya Umma huwa na kibao (Plate Number) ambazo huanziwa na herufi SU na kufuatiwa na namba tofauti tofauti kwenye vibao hivyo

11. Magari kwa ajili ya matumizi ya Miradi inayofadhiliwa na watu to nje ya nchi
Magari yanayotumika kwenye miradi inayofadhiliwa kutoka nje ya nchi kuwa na kibao chenye herufi DFP (Donor's Fund Project) ikifuatiwa na namba tofauti tofauti. Pia tofauti na DFP utakuta mengine yana DFPA

12. Magari ya Police wa Tanzania
Magari ya Polisi nchini Tanzania huwa na kibao chenye kuanziwa na herufi PT (Polisi of Tanzania) halafu hufuatiwa na namba tofauti tofauti mbele yake

13. Magari ya Jeshi la Wananchi Tanzania
Magari ya Jeshi la Tanzania huwa na kibao chenye kuanziwa na namba kadhaa kisha hufuatiwa na herufi JW kisha hufuatiwa na namba tena.

14. Magereza Tanzania
Magari ya Magereza ya Tanzania huwa na kibao chenye kuanziwa na herufi MT kisha hufuatiwa na namba kadhaa mbele yake kwenye kibao cha magari hayo

15. Serikali ya Tanzania
Serikali ya Tanzania ina gari zake tofauti tofauti ambzo hutumika kwa mfano Wilayani au hata kwenye halmashauri. Magari haya huwa na kibandiko chenye Herufi za mwanzo STK au STJ au STL na baada ya hapo hufuatiwa na namba kadhaa mbele

16. Magari ya Wakuu wa Mikoa
Wakuu wa mikoa wote nchi huwa na magari ambayo huwana plate number ka tofauti. Gari la mkuu wa mkoa huwa na kibandiko ambacho kuanza na herufi RC na kisha hufuatiwa na herufi ambazo ni kifupi cha mkoa wake. Herufi RC humaanisha Regional Commisioner. Mfano; RC NJB- Mkuu wa Mkoa Njombe

17. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Serikali ya mapinduzi Zanzibar hutumia magari yenye kibao chenye kuanziwa na herufi SMZ kisha kufuatwa na tarakimu kadhaa. Magari haya hutumika kwenye shuguli za kiserikali hivyo hupewa viongozi wa serikali katika ngazi fulani.

18. JR- Jaji wa Mahakama ya Rufaa

19. JK- Jaji Kiongozi

20. J- Jaji wa Mahakama Kuu

21. CGP-Commissioner General of Prison(Mkuu wa Magereza)

22. CAG - Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali

23. Magari ya watu binafsi
Magari ya watu binafsi nchini Tanzania huwa na kibao chenye kuanza na herufi T kisha tarakimu tatu hufuata na baada ya hapo herufi tatu hufuata. Magari haya ya binafsi yanaweza kuwa ya biashara au la.

Pia kwenye magari ya binafsi ambayo sio ya biashara kunauwezekano kuwa na kibandiko ambacho kina jina mtu binafsi lkn kuna gharama za kulipia kila mwaka.
Sawa lakini huu muda wa kujua no za magari unaupata wapi
Hii nchi Ina jobless wengi.
 
Babu kumbe upo..

Umepotea sana humu, wajukuu tutapotezwa na Gen Z kwa kukosa nasaha zako kwa muda mrefu[emoji2][emoji2]
Niko bhana.... Mashangazi yalinificha kwa muda. Nimefanikiwa kutoroka
 
Niko bhana.... Mashangazi yalinificha kwa muda. Nimefanikiwa kutoroka
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Unajilia vinono sana, ebu achia na wajukuu bana wapate raha ya Ulimwengu
 
Msaada tafadhali, Jana kuna gari ilinipita ilikuwa Land cruiser V8 nadhani, ile imeandikwa mbele TOYOTA kama ile alipewa Mabeyo ni mpya kabisa. Kilicho nishangaza ina usajili wa herufi A badala ya E kwa sasa hivi. Hiyo ina maana ipi?
Usalalama wa taifa hilo
 
Screenshot_20240505-100707.png
 
Back
Top Bottom