Zijue sababu za jeshi letu JWTZ kutokutoa kichapo kingine kwa M23, kama tulivyotoa mwaka 2013 hadi 2014

Zijue sababu za jeshi letu JWTZ kutokutoa kichapo kingine kwa M23, kama tulivyotoa mwaka 2013 hadi 2014

Hizo ni taratibu za askari wanaofanya kazi ya kulinda amani (Peace Keeping) ila ingekuwa ni vita rasmi,siku nyingi sana M23 wangeita maji MMA
Wewe unaujua ukweli mkuu. Sio hao chawa wa Kagame.
 
Hata hao M23, nao nidhaufu sana, niliona kipande kidogo cha front line kule TikTok ( nadhani mambo wao Ali live stream kimakosa Ile scene), nao wako disorganized, na wanatumia watoto wadogo vitani!
Kama M23 ni dhaifu mbona wameteka Goma ?
 
Hizo ni taratibu za askari wanaofanya kazi ya kulinda amani (Peace Keeping) ila ingekuwa ni vita rasmi,siku nyingi sana M23 wangeita maji MMA
Screenshot_20250202-160118.jpg
Screenshot_20250202-160130.jpg

Hao wajeda wetu mateka walikuwa usingizini wakati wanatekwa?
 
Kwa sasa hiyo M23 ya Sultan Makenga ni sehemu tu ya AFC ambacho ni combination ya makundi kibao ya waasi yenye silaha huko Mashariki ya DRC.

Zaidi ni kuwa kiongozi wa AFC hii ya jana tu bwana Nangaa Yubeluo anaweza kuwa na backup hata ndani ya DRC ukizingatia alikuwa Rais wa Tume Huru ya uchaguzi ya DRC yaani CENI tena juzi tu 2015-2021.

Kwa kifupi hii ya sasa siyo M23 ni AFC,sema M23 inatajwa sana sababu ndiye ITV yaani Super brand huko Mashariki.
 
Umeandika hadithi nzuri sana mkuu ila fanya utafiti kwanza hasa wa kiuchumi. Kwa maana ya faida ya DRC kwa Tanzania na Faida Ya Rwanda kwa Tanzania..

Mbingu Na Ardhi!!

Naamini ukimaliza kufanya utafuti utafuta hii post!!
Kumbuka DRC wanatumia pia bandari za Durban na Beira kwa kiwango kikubwa sana, the best way ni kutafuta namna ya kuvusha mizigo yao kupitia lake Tanganyika na siyo mpaka kuwe na nchi ya kati ya transit.
 
amani ya CONGO ni muhimu kuliko hata huo uhusiano wa kibiashara kati yetu na rwanda.
Muhimu kwa nani? Kama wao haoni umuhimu kuipigania kufa na kupona nchi yao sasa itakuwa muhimu kwa nani mwingine?
Kwetu hata wakichinjana 24/7 waendelee tu mpaka watakapoamua kuelewana.
 
Niaje waungwana

Kwanza kabla ya kuelezea sababu za jeshi letu kutokutoa kichapo kwa M23, naomba kwanza nianze kuwapa historia tukufu ya jeshi letu la JWTZ au TPDF kwa nchi mbali mbali za Africa na Dunia kwa ujumla.

JTWZ chini ya baba wa taifa letu hayati mwl. Julius K. Nyerere ndio iliyoongoza mapambano yasioshindwa ambayo kwa asilimia kubwa yalisaidia nchi za Zimbabwe, Msumbiji, Afrika Kusini, Namibia na Angola kuwa katika mikono salama, na amani ya kudumu mpaka leo.

Idi Amin alitaka kujichanganya eti aichukue Bukoba, matokeo yake imechukuliwa nchi yake mwenyewe, halaf yeye akatoka nduki.

JWTZ hiyo hiyo chini ya utawala wa hayati mzee Ally Hassan Mwinyi ndio iliyotoa kichapo kitakatifu kwa jeshi la Burundi ambalo lilitaka kuteka sehemu ya mkoa wa Kigoma, kwa kisingizio cha kuja kuwapiga waasi wa CNDD-FDD ambao walikuwa wakipambana na serikali ya Burundi chini ya uongozi wa raisi meja Pierre Buyoya (rip).

Ni kwamba Buyoya na serikali yake walikuwa wanadai kwamba serikali ya Tz imekuwa ikitoa msaada wa kuwahifadhi waasi hao katika maeneo ya mpakani mwa Mkoa wa Kigoma na Burundi. Hivyo dawa ya kukomesha jambo hilo ilikuwa ni kuivamia Tz (Buyoya sijui nani alimhadaa ashike moto kwa mkono), kuichapa na kuteka maeneo yote aliyodai yanatumiwa na waasi nchini kwetu kufanyia training na kupanga mipango ya kuingia Burundi kufanya maangamizi mara kwa mara.

Basi bwana Buyoya akaamuru jeshi lake lifanye ambush kupitia mipaka ya ardhini na majini. Aisee kilichotokea kwa upande wa Burundi mpaka leo ni hasara kwa nchi yao.

Kuna jamaa fulan Mrundi anasema kuwa sehemu hiyo iliyoangukiwa na kombora kutoka Tz mpaka sasa hapajawahi kuota chochote, na wala kujengwa chochote. Ni kama vile ardhi imeunguzwa hata kwa kutumia kutengenezea tofali za kuchoma haifai kudadeki. Baada ya lile tukio Buyoya na warundi wenzie wakawa wapole na askari waliokuwa wanalinda mipaka ya majini na ardhini kwa upande wa Burundi akawasogeza mbali mno kutoka mpakani.

Chini ya utawala wa raisi Kikwete kuna raisi alikuwa ashapinduliwa hapo Comoro, ikabidi aje kuomba msaada wa kumrudisha madarakani. Ni kitendo cha masaa tu raisi akarudishwa na wahuni waliopanga mapinduzi wakatiwa nguvuni.

Pia chini ya Kikwete raisi wa Burundi hayati Pierre Ngurunziza alikuwa ameshapinduliwa na kuambiwa abaki huku huku Tz alipokuwa amekuja kwa mkutano wa amani. Baada ya ujinga huo, Kikwete akatuma kikosi kidogo tu cha wanajeshi wa kumrudisha nchini kwake salama na kuwatia nguvuni wapuuzi wachache waliompindua raisi wao. Bila kuchelewa jeshi letu likamrudisha Ngurunziza, ila wapinduaji wakafanikiwa kutoroka na kukimbilia nchi jirani.

Chini ya utawala huo huo wa Kikwete jeshi letu lilitoa kipondo ambacho kilisababisha waasi wa M23 kutimkia Uganda na Rwanda. Na hii ni baada ya raisi wa Rwanda mhe. Paul Kagame kumletea dharau Kikwete na jeshi letu hali iliyosababisha Kikwete adili na kila kinachompaka Kagame jeuri. Alianza na wanyarwanda waliokuwa wanaishi nchini kinyume cha sheria, baadae akarukia Congo kuwafyeka M23 ambao waliaminika kuwa ni jeshi dogo la Rwanda. Kisha akasogeza jeshi mkoa wa Kagera kuwa tayari kuingia Kigali, sema hekima Za mzee Mwinyi na Mkapa zilichangia kumfanya Kikwete asivaamie Rwanda kumtoa adui yake.

Tukiachana na hayo. Tushapandikiziwa vikundi vya waasi kwa mgongo wa dini huko Tanga, Kibiti nk. Lakini jeshi letu halijawahi kucheka na kima wote tumewaangamizi kwa muda mfupi sana.

Hizo operations zote nilizoeleza hapo juu zilitekelezwa na TPDF bila kushindwa wala kurudi nyuma. Hivyo uwezo wa kumpiga adui toka miaka hiyo tulikuwa, tunao na tutaendelea kuwa nao. Huu ndio ukweli halisi.

Sasa tukija kwa hii vita ya sasa ya M23. Kuna watu wanajiuliza iweje M23 hii tulioichapa wakati wa Kikwete imetushinda wakati wa Samia!!

Ukweli ni kwamba jeshi letu lipo imara, vizuri na tayari kwa mapambano wakati wowote bila kujali ni nani aliepo madarakani. Kikubwa ambacho hufanyika ni kuliongezea jeshi silaha za kisasa, mbinu mpya za kijeshi, nguvu na morali zaidi za kulitumikia jeshi la wananchi. Pia jeshi letu hupambana kupitia amri ya amiri jeshi mkuu na wasaidizi wake. So kama amiri jeshi mkuu haoni tija yoyote ya jeshi letu kupambana huko Congo na kwengine basi jeshi letu halitopambana.

Sasa kinachoendelea Congo kwa sasa ni tofauti na kile kilichokuwa kinaendelea kipindi kile cha 2013 hadi 2014. Kipindi kile tuliingia vitani kivita kweli kweli, huku amiri jeshi mkuu wa Tz akiwa na lengo la kumshikisha adabu amiri jeshi mkuu mwenzake wa nchi jirani. Hivyo ilikuwa ni vita ya serious ndiomaana tuliwachapa M23 bila huruma hadi wakakimbia wenyewe na kuacha silaha zao.

Lakini hii vita ya sasa hivi Congo sisi hatukwenda ki serious kwa sababu raisi amegundua kwamba hii vita haina faida yoyote kwetu. Sana sana tunaweza kupata hasara zaidi kuliko faida.

Hii ni kwa sababu mfadhili mkubwa anaewafadhili hawa M23 ndio mtu wa kwanza au wa pili kupitisha mizigo yake katika bandari yetu na ardhi yetu. Analipa mabilioni ya ushuru kila siku au kila week.

Hivyo tukiingia kwenye vita na mtu huyu ni sawa sawa na kuukata mkono wako mwenyewe unaokulisha. Kumbuka kwamba mfadhili huyo ana ukaribu na amiri jeshi mkuu wetu haswa kuhusu maswala ya kibiashara , upitishaji wa mizigo na ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi yetu na nchi ya mfadhili. Sasa tukiwa serious kumtwanga itabidi atukimbie na kwenda kushirikiana na nchi nyingine kama vile Kenya nk.

Hizo ndio sababu kuu za sisi kutoiadhibu M23 kama kipindi kile. Serikali inaangalia hasara na faida inayopata kupitia vita hivi. Tukiwachapa basi hasara itakuwa kubwa kuliko faida. Lakini kwa vile sisi ni sehemu ya SADC na tumechaguliwa kwenda Congo. Basi acha jeshi letu litulie kule kujilia watoto wa kinyamulenge hadi muda ukapofika kurudishwa nyumban waruri kuendelea na maisha. But ukweli utabaki pale pale kwamba hapa East Africa hakuna jeshi wala kikundi cha wahuni kama hicho cha M23 ambacho kitaweza kupambana na JWTZ.
Pamoja na faida ulizozitaja ni vyema M23 wakapigwa kidogo ili kulinda heshima ya JWTZ heshima ya jeshi ni muhimu kuliko faida za muda mfupi za kiuchumi lazima ku balance ili hali Kagame anasema hahusiki na M23 bali watwangwe halafu tuone. Wanasema mpige mbwa halafu mwenye mbwa atajitokeza.
 
Pamoja na faida ulizozitaja ni vyema M23 wakapigwa kidogo ili kulinda heshima ya JWTZ heshima ya jeshi ni muhimu kuliko faida za muda mfupi za kiuchumi lazima ku balance ili hali Kagame anasema hahusiki na M23 bali watwangwe halafu tuone. Wanasema mpige mbwa halafu mwenye mbwa atajitokeza.
Ikibidi kuwajambisha kidogo M23, tutawajambisha tu mkuu.
 
Kwa sasa hiyo M23 ya Sultan Makenga ni sehemu tu ya AFC ambacho ni combination ya makundi kibao ya waasi yenye silaha huko Mashariki ya DRC.

Zaidi ni kuwa kiongozi wa AFC hii ya jana tu bwana Nangaa Yubeluo anaweza kuwa na backup hata ndani ya DRC ukizingatia alikuwa Rais wa Tume Huru ya uchaguzi ya DRC yaani CENI tena juzi tu 2015-2021.

Kwa kifupi hii ya sasa siyo M23 ni AFC,sema M23 inatajwa sana sababu ndiye ITV yaani Super brand huko Mashariki.
Ulichoandika kinaeleweka mkuu.
 
Kama tungeendelea kuwachapa basi wangekomaa na huu mpango pichani ili mizigo yao iwe inapitia huko kwa wenzetu.
Ndo uzwazwa huo. Unailenga Rwanda na mali za kuiba na kuiacha Zambia na jirani zake
 
Hata JWTZ ikijiingiza kichwa kichwa kwenye hiyo Vita vya huko Goma itajikuta inapoteza na kushindwa Vita.
Hao Waasi wa M23 Wanaungwa mkono na Watu wengi Sana waishio kwenye maeneo hayo yenye migogoro.
Aidha, hata baadhi ya Vigogo wengi sana waliopo ndani ya Serikali ya Congo DR pia wanawaunga mkono hao Waasi wa M23. Hivyo, hao Waasi wa M23 Wana Watu wao ndani ya Serikali ya huko na wamekuwa wakipata taarifa zote kabisa muhimu za kiintelijensia kutoka Serikalini kupitia kwa hao Mawakala wao.
Mbaya zaidi sana, ndani ya Majeshi yote kabisa ya Serikali ya Congo DR kuna Mamluki wengi sana ambao pia ni Wapiganaji wa Vikosi vya Waasi wa M23, that's why unaona kwamba kuna matukio mengi sana ya Uasi wa chini chini ndani ya Majeshi ya nchi hiyo.
Jeshi la Congo DR jinsi lilivyo ni sawa sawa kabisa na jinsi Jeshi la Nigeria jinsi lilivyo. Wanajeshi wengi sana wa Nigeria pia ni Wapiganaji wa Kundi la Boko Haram, na Wanajeshi wengi sana wa Jeshi la Congo DR pia ni Wapiganaji wa Vikosi vya Waasi wa M23.
Huna unalolifahamu
 
Niaje waungwana

Kwanza kabla ya kuelezea sababu za jeshi letu kutokutoa kichapo kwa M23, naomba kwanza nianze kuwapa historia tukufu ya jeshi letu la JWTZ au TPDF kwa nchi mbali mbali za Africa na Dunia kwa ujumla.

JTWZ chini ya baba wa taifa letu hayati mwl. Julius K. Nyerere ndio iliyoongoza mapambano yasioshindwa ambayo kwa asilimia kubwa yalisaidia nchi za Zimbabwe, Msumbiji, Afrika Kusini, Namibia na Angola kuwa katika mikono salama, na amani ya kudumu mpaka leo.

Idi Amin alitaka kujichanganya eti aichukue Bukoba, matokeo yake imechukuliwa nchi yake mwenyewe, halaf yeye akatoka nduki.

JWTZ hiyo hiyo chini ya utawala wa hayati mzee Ally Hassan Mwinyi ndio iliyotoa kichapo kitakatifu kwa jeshi la Burundi ambalo lilitaka kuteka sehemu ya mkoa wa Kigoma, kwa kisingizio cha kuja kuwapiga waasi wa CNDD-FDD ambao walikuwa wakipambana na serikali ya Burundi chini ya uongozi wa raisi meja Pierre Buyoya (rip).

Ni kwamba Buyoya na serikali yake walikuwa wanadai kwamba serikali ya Tz imekuwa ikitoa msaada wa kuwahifadhi waasi hao katika maeneo ya mpakani mwa Mkoa wa Kigoma na Burundi. Hivyo dawa ya kukomesha jambo hilo ilikuwa ni kuivamia Tz (Buyoya sijui nani alimhadaa ashike moto kwa mkono), kuichapa na kuteka maeneo yote aliyodai yanatumiwa na waasi nchini kwetu kufanyia training na kupanga mipango ya kuingia Burundi kufanya maangamizi mara kwa mara.

Basi bwana Buyoya akaamuru jeshi lake lifanye ambush kupitia mipaka ya ardhini na majini. Aisee kilichotokea kwa upande wa Burundi mpaka leo ni hasara kwa nchi yao.

Kuna jamaa fulan Mrundi anasema kuwa sehemu hiyo iliyoangukiwa na kombora kutoka Tz mpaka sasa hapajawahi kuota chochote, na wala kujengwa chochote. Ni kama vile ardhi imeunguzwa hata kwa kutumia kutengenezea tofali za kuchoma haifai kudadeki. Baada ya lile tukio Buyoya na warundi wenzie wakawa wapole na askari waliokuwa wanalinda mipaka ya majini na ardhini kwa upande wa Burundi akawasogeza mbali mno kutoka mpakani.

Chini ya utawala wa raisi Kikwete kuna raisi alikuwa ashapinduliwa hapo Comoro, ikabidi aje kuomba msaada wa kumrudisha madarakani. Ni kitendo cha masaa tu raisi akarudishwa na wahuni waliopanga mapinduzi wakatiwa nguvuni.

Pia chini ya Kikwete raisi wa Burundi hayati Pierre Ngurunziza alikuwa ameshapinduliwa na kuambiwa abaki huku huku Tz alipokuwa amekuja kwa mkutano wa amani. Baada ya ujinga huo, Kikwete akatuma kikosi kidogo tu cha wanajeshi wa kumrudisha nchini kwake salama na kuwatia nguvuni wapuuzi wachache waliompindua raisi wao. Bila kuchelewa jeshi letu likamrudisha Ngurunziza, ila wapinduaji wakafanikiwa kutoroka na kukimbilia nchi jirani.

Chini ya utawala huo huo wa Kikwete jeshi letu lilitoa kipondo ambacho kilisababisha waasi wa M23 kutimkia Uganda na Rwanda. Na hii ni baada ya raisi wa Rwanda mhe. Paul Kagame kumletea dharau Kikwete na jeshi letu hali iliyosababisha Kikwete adili na kila kinachompaka Kagame jeuri. Alianza na wanyarwanda waliokuwa wanaishi nchini kinyume cha sheria, baadae akarukia Congo kuwafyeka M23 ambao waliaminika kuwa ni jeshi dogo la Rwanda. Kisha akasogeza jeshi mkoa wa Kagera kuwa tayari kuingia Kigali, sema hekima Za mzee Mwinyi na Mkapa zilichangia kumfanya Kikwete asivaamie Rwanda kumtoa adui yake.

Tukiachana na hayo. Tushapandikiziwa vikundi vya waasi kwa mgongo wa dini huko Tanga, Kibiti nk. Lakini jeshi letu halijawahi kucheka na kima wote tumewaangamizi kwa muda mfupi sana.

Hizo operations zote nilizoeleza hapo juu zilitekelezwa na TPDF bila kushindwa wala kurudi nyuma. Hivyo uwezo wa kumpiga adui toka miaka hiyo tulikuwa, tunao na tutaendelea kuwa nao. Huu ndio ukweli halisi.

Sasa tukija kwa hii vita ya sasa ya M23. Kuna watu wanajiuliza iweje M23 hii tulioichapa wakati wa Kikwete imetushinda wakati wa Samia!!

Ukweli ni kwamba jeshi letu lipo imara, vizuri na tayari kwa mapambano wakati wowote bila kujali ni nani aliepo madarakani. Kikubwa ambacho hufanyika ni kuliongezea jeshi silaha za kisasa, mbinu mpya za kijeshi, nguvu na morali zaidi za kulitumikia jeshi la wananchi. Pia jeshi letu hupambana kupitia amri ya amiri jeshi mkuu na wasaidizi wake. So kama amiri jeshi mkuu haoni tija yoyote ya jeshi letu kupambana huko Congo na kwengine basi jeshi letu halitopambana.

Sasa kinachoendelea Congo kwa sasa ni tofauti na kile kilichokuwa kinaendelea kipindi kile cha 2013 hadi 2014. Kipindi kile tuliingia vitani kivita kweli kweli, huku amiri jeshi mkuu wa Tz akiwa na lengo la kumshikisha adabu amiri jeshi mkuu mwenzake wa nchi jirani. Hivyo ilikuwa ni vita ya serious ndiomaana tuliwachapa M23 bila huruma hadi wakakimbia wenyewe na kuacha silaha zao.

Lakini hii vita ya sasa hivi Congo sisi hatukwenda ki serious kwa sababu raisi amegundua kwamba hii vita haina faida yoyote kwetu. Sana sana tunaweza kupata hasara zaidi kuliko faida.

Hii ni kwa sababu mfadhili mkubwa anaewafadhili hawa M23 ndio mtu wa kwanza au wa pili kupitisha mizigo yake katika bandari yetu na ardhi yetu. Analipa mabilioni ya ushuru kila siku au kila week.

Hivyo tukiingia kwenye vita na mtu huyu ni sawa sawa na kuukata mkono wako mwenyewe unaokulisha. Kumbuka kwamba mfadhili huyo ana ukaribu na amiri jeshi mkuu wetu haswa kuhusu maswala ya kibiashara , upitishaji wa mizigo na ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi yetu na nchi ya mfadhili. Sasa tukiwa serious kumtwanga itabidi atukimbie na kwenda kushirikiana na nchi nyingine kama vile Kenya nk.

Hizo ndio sababu kuu za sisi kutoiadhibu M23 kama kipindi kile. Serikali inaangalia hasara na faida inayopata kupitia vita hivi. Tukiwachapa basi hasara itakuwa kubwa kuliko faida. Lakini kwa vile sisi ni sehemu ya SADC na tumechaguliwa kwenda Congo. Basi acha jeshi letu litulie kule kujilia watoto wa kinyamulenge hadi muda ukapofika kurudishwa nyumban waruri kuendelea na maisha. But ukweli utabaki pale pale kwamba hapa East Africa hakuna jeshi wala kikundi cha wahuni kama hicho cha M23 ambacho kitaweza kupambana na JWTZ.
soko la Kongo ni kubwa kuliko la Rwanda ni swala tu la kukaa mguu sawa.
kibaya zaidi ubinafsi wa viongozi wetu unatuletea tabu kubwa kwetu.
ifike sehemu nafikiri Mama kwa heshima kabisa apumzike.
ukipoteza askari wawili kati ya mia ni kwamba umepoteza 2% ya askari ulionao lakini familia imepoteza 100% ya mzazi au mtu waliyemtegemea katika maisha yao hivyo kama anaona haina tija na inaguza maslahi binafsi na yuko tayari kula haramu kwakuwa ni DAMU ZA WATU wasio na hatia basi ajiunge moja kwa moja m23tuwapige wakongo vinginevyo wanaokufa pia ni waafrika wenzetu kwa mali zao.
 
Back
Top Bottom